Wedding Anniversary

Wedding Anniversary

Hongeraaa Bibie!!!! Mi ushauri wangu ni NGANGANIA ZAIDI NA ZAIDI HAPO HAPO ZAIDI YA LUBA!!! Kitaa hali si shwariii! UKISHIKWA SHIKAMANA BIBI!!! Naomba wimbo wa Naomba kibao NO. 1 cha ENRIQUE IGLESIAS, END OF THE ROAD cha BOYS II MEN, Na MY HEART WILL GO ON cha CELINE DION VIWABURUDISHE SIKU YA LEO!!!!!

NANI KANUNAAAAAA!!!!!!!!! (NYUMBA NDOGO, VIMADA, SECRETARY, NA VIZABIZABINA WOTE MNAONGEJEA KITU KISAMBARATIKE!!!! HAKIVUNJIKIIII KITU!!! MPO HAPO! MTANGOJA MIAKA 1000000000000000000000000000000)

Chonde chonde shosti unganganie, sio hapa najitia SHABIKI MAANDAZI KUWEKWA AMIRA KIJIKO KIMOJA NA KUUMUKA BESENI ZIMA! Usije kusema humu Kitu Chaliiiii! LITANISHUKAJE!!!!!
he he heeeeeeeeeeee, shostito wala usijali mamiii, huwezi kuja kusutwa, yaani i am here to stay, so ondoa shaka.
Asante sana kwa nyimbo, na mawosia, lol!
 
Asante rafiki,
Umenichekesha sana unavyokumbuka mastori ya hapa na pale. kwa kweli haijawahi tokea tena, hata jana alikumbusha alivyonifanya nilie ile siku na kuijutia sana. kila mwaka siku kama ya leo, pamoja na mengi tunayoyafanya, huwa tunaulizana ni kitu gani ambacho uliwahi kumfanyia/kufanyiwa na mwenzio na uka-regret. Huwezi amini kila mwaka hiyo ndo regret yake............ Namshukuru Mungu kwa hilo
ooh jamani ni bahati sana kuwa na partner mwenye moyo wa kuona kosa na kukubali na kujutia..watu wengi tuna mioyo ya jeuri so inakuwa ngumu kusuluhisha na kusonga mbele.
kama watu wangekuwa wanakubali makosa yao na kutubu na kuacha tungekuwa mbali saaana
ndoa nyingi watu wana roho za jeuri jeuri na mambo yanakuwa magumu
 
Hongera sana rafiki hiyo ni hatua kubwa hivyo mna kila sababu ya kumshukuru Mungu. Mwenyezi Mungu na aendelee kuwabariki mzidi kudumu katika agano lenu, awajalie amani, upendo na afya njema siku zote za maisha yenu.
Amen mwaJ, Kwa kweli namshukuru Mungu kwa hilo.
Asante kwa kutuombea
 
Last edited by a moderator:
ooh jamani ni bahati sana kuwa na partner mwenye moyo wa kuona kosa na kukubali na kujutia..watu wengi tuna mioyo ya jeuri so inakuwa ngumu kusuluhisha na kusonga mbele.
kama watu wangekuwa wanakubali makosa yao na kutubu na kuacha tungekuwa mbali saaana
ndoa nyingi watu wana roho za jeuri jeuri na mambo yanakuwa magumu
Ni kweli kabisa..... unajua mtu anapokiri kosa na kulijutia unajua kabisa alifanya kwa bahati mbaya na hatarudia. jeuri inapoingia mimi huwa naamini huyo mtu hayupo tayari kuliacha hilo kosa, i.e. ataendelea nalo.
Kwa kweli namshukuru Mungu alinipa mume wa kukiri kosa. maana najua ingeniumiza sana. hata kwa watoto na watu ninaokaa nao wanajua wakifanya kosa wanasema ukweli na wanaomba msamaha sina tatizo, ila ukidanganya........
 
hakika mwastahili pongezi,miaka 13 ktk ndoa si mchezo,lakini kwenu imewezekana,mmebaki kuwa mwili mmoja na mmesimamia lengo lenu.upendo umekuwa chachu ya umri huu wa ndoa na kuvumiliana kumewajengea heshima katika jamii,hongereni sana!hakika ndoa iheshimiwe na watu wote nanyi mmekuwa dira ya kweli ktk kujenga heshima nasi twaiheshimu ndoa hii na kumwomba MWENYEZI MUNGU azidi kuwabariki,kuwapeni umri mrefu zaidi wa ndoa,afya njema ktk roho,miili yenu na afya njema ya ndoa,upendo uzidi kukua na katu msimuache anaewafanya kuwa ninyi ktk dunia hii.mbarikiwe sana na kila jema ktk safari yenu ya kupigiwa mfano.be blessed!
Amen Mgaya, nashukuru sana kwa hii post yako. Mungu akubariki pia
 
waaaaoh hongera sana FP am so proud of you! Ni wachache sana wanaoweza kukaa miaka hiyo bila kutetereka . Jambo la Kumshukuru Mungu na sababu ya kuparty leo kwa saaana tu!

Hawa wa siku hizi wakikaa mwaka mmoja miwili tayari mambo yameanza....bora 'siye wa zamani' lol
The Boss upo arifu?
Thank you Kaizer, kwa kweli namshukuru Mungu...... sisi watu wa zamani tulijaliwa uvumilivu na kujishusha
 
Last edited by a moderator:
happy anniversary FP . Mungu akuzidishie moyo mzuri na upendo kwenye ndoa yenu na muendelee kutimiza agano. you are an inspiration to us unmarried people
 
happy anniversary @FP. Mungu akuzidishie moyo mzuri na upendo kwenye ndoa yenu na muendelee kutimiza agano. you are an inspiration to us unmarried people.
Amen Blaine, nafurahi kuwa-inspire ambao bado hawajaingia huku, kila kitu kinawezekana kwa msaada wa Mungu
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom