Tatizo ni kuwa kwako wewe umefumba macho hutaki kuona makosa ya serikali; kwa kufumba kwako macho uko tayari kuacha serikali ifanye lolote kwa mtu yoyote si kwa sababu ni haki au ni sawa bali ni kwa sababu ni serikali. Wakati wa utawala wa ...makaburu kulikuwa na watu waliotaka ANC wasiupinge utawala huo na kuwasihi wakubaliane nao au wauelewe. Ndicho ninachokiona unachokifanya. Kwako wewe, serikali haiwezi kufanya jambo baya. Mawazo yangu yaweza kuwa ni ya unafiki, lakini msimamo wako ni wa hatari kwa taifa letu na ni wajibu wa watu wenye dhamira zao kuwapinga.[/QUOTE
Mzee Mwanakijiji!
Hakuna hata siku moja ambayo sijaona makosa ya serikali au kufumbia macho makosa hayo lkn kukosoa serikali ni kwa njia ya maandamano tu ambayo hatima yake ni kupoteza maisha ya binadamu wenzetu?Hivi unataka kuniambia hakuna njia ambazo zinaweza kutumika zaidi ya maandamano kuishinikiza serikali iliyopo madarakani kutekeleza yale umma wa Tanzania wanayoyataka? tumeona hivi karibuni moto wa kutoka ndani ya bunge kwa amani umeweza kufanikisha mjadala wa katiba kupata muelekeo mpya.Tusilazimishe lile tunalolitaka ndiyo lifanyike hata kama linahatarisha maisha ya binadamu wenzetu,Maisha ya binadamu yanapopotea hamna anayeweza kuyarudisha hivyo pale tunapoweza kuepusha upotevu wa maisha ya binaadamu au kupoteza amani ni bora tukazingatia hilo na kutafuta taratibu mbadala za kutupeleka salama.Mfano wa Afrika ya kusini na hali ya Tanzania tuliyonayo sasa nitofauti kabisa na hali iliyokuwa sauzi haijafikia hata robo ya uhuru wa watanzania walionao ktk nyanja mbali mbali.tusishabikie machafuko ktk nchi tunayoipenda kwa jina la kuleta mabadiliko naamini busara inapotumika mabadiliko tutayapata kwa njia salama na kuyafaidi mabadiliko hayo kwa amani bila ya madhara.
You fool n coward. Can u give as an example of a country that got change without risking the life of patriot? Who gona give it to you peacefully? That is just a token there is a lot more to come if you realy want change. Is either you risk your life to be free or stay silent to become slave in your own mother land.