We Condemn: Calling for A National Day of Mourning

We Condemn: Calling for A National Day of Mourning

Serikali yetu na jeshi la Polisi hawajifunzi nchi nyingine kuhusu haki ya kuandamana? mi nadhani MIBANGi wanayovuta hawa so called ffu ndiyo inawafanya wajichukulie sheria mkononi na kupiga watu na kuua bila kosa..kuna haja ya kulijenga upya jeshi letu lijitegemee kwa misingi ya sheria siyo kutumiwa na watawala. watu kama akina andengenye sijui? (AR rpc) hawapaswi kuwepo kwenye hili jeshi yeye ndiyo kabisa MIBANGE maana hajui anafanyanya yeye kabaki tu YES SIR...!! yes sir my A$@*%^#s:A S-confused1::A S-confused1::A S-confused1:
 
Mchungaji Slaa na wenzake lazima wawe prscuted kwa kupinga order ya police na kusababisha vifo vya innocent civilians pia waadhibiwe kwa kwa kuvunja public order

Hawa chadema ni hatari sana tulisema siku nyingi hapa jf, nichama kinaongozwa na vilaza wasiokuwa na uzoefu wowote wa kuongoza hata idara ya kijiji

Chadema isipo dhibitiwa mapema italeta majanga zaidi hapa nchini, Jiulize kwa nini maandamano yamefanyiwa Arusha ? huko ndo kuna kabila la chama chao na makanisa yanyo endeshwa kwa tamaa na papara za kuingia Ikulu.

Chadema ni sawa na cancer lazima idhibitiwe

Bull,

Hivi una uhakika na ulichoandika hapa? Au umekurupuka tu usingizini na kuanza kuandika. Fuatilia ujue ni kwa nini Chadema waliamua kuandamana. Kwa udikiteta tulio nao Tanzania, uamuzi wa Chadema ulikuwa sahihi. Damu zilizomwagika zitakuwa juu ya JK, Makamba na huyo anayejiita mkurugenzi wa Halmiashauri hapo Arusha. Mwema na Andengenye masikini wao ni bendera fuata upepo tu!!!

Tiba
 
hakuna taarifa za kiinteligensia. NONE. Unafikiri kesho Chadema wakitangaza maandamano Mwema atazuia au atakubali.. I bet you atakubali kwa asilimia 100.

Kazi za Polisi ni kulinda mali na usalama wa raia. Maandamano na mikutano ni haki ya msingi ya kila raia,kama ilivyo kucheza mpira au kukusanyika kuangalia michezo. Si kazi ya polisi kuchambua maudhui ya mikutano ya siasa. Kova wa DSM aliwahi kusema CUF hawana sababu ya kuandamana kwa kuwa suala la katiba keshaliongelea waziri mkuu. Hii si kazi ya polisi bali ushabiki.
Polisi ilitakiwa itumie taarifa za intelejensia kuzuia uhalifu kama ulikuwepo. Sasa tujiulize taarifa hizo zimesaidia vipi jeshi la polisi, na je waliouawa ndio waliokuwa katika taarifa ya intelejensia. Kama angekuwepo gaidi polisi ingesubiri aandamane kwanza. Hili neno intelejensia ni UONGO kwa kukosa majibu.
 
Naomba utoe mfano wa chanzo kimoja huru cha habari kilichoanisha kuwa Polisi walizidiwa "nguvu na raia". Naomba uweke kimoja tu na walizidiwa nguvu kabla ya kujaribu kuvunja maandamano au baada ya jaribio la kijinga la kuvunja maandamano halali?







Swali hili linaweza kuwa na hekima kidogo lakini ukiliangalia halizingatii ukweli. Watu 100 wenye manati wanalinganishwa vipi na mtu mmoja mwenye SMG? Je askari mia moja wenye SMG unaweza kulinganisha na wananchi 100 ambao hawana silaha?


Tatizo ni kuwa hawa wananchi hawakuwa hata na manati! Hakuna aliyekamatwa na kisu wala fimbo. Walikuwa mikono mitupu. Now u tell me kuna ulinganifu gani kati ya mikono mitupu na SMG, magari ya maji ya upupu, bastola, mabuti, virungu n.k? Really? Yaani unalinganisha wananchi wasio na silaha ya yote na jeshi la Polisi lenye udhaifu wa muda mrefu na silaha bwelele?



hapana hii si hoja ya msingi; kwani hakukuwepo na wenye manati! walikuwwepo watu wenye mikono mitupu. Sasa hiyo ni hoja ya msingi..

,

Yaani silaha zote hizo na unaniambia walizidiwa nguvu? Really, wangezidiwa nguvu maandamano yangefika mwisho. Polisi hawakuzidiwa nguvu bali waliwazidi nguvu wananchi wasio na silaha na kusababisha mauaji. Thats is a fact.




Nice try. Hakukuwa na fujo yoyote kabla ya jeshi la polisi lenye mwelekeo wa udhalimu lilipoamua kuingilia maandamano yaliyokuwa yanasonga mbele. Haki ya kulinda uhai unaita mtu yeyote anayeshambuliwa kujitetea hata ukishambuliwa na Polisi. Wananchi walikuwa wanaandamana vizuri tu hadi pale POlisi walipoona maandamano kweli yanafanikiwa wakaamua kuingilia kati. Hakuna vurugu yoyote kabla ya polisi kuingilia kati.


msisitizo wa neno lako ni "kama".



Nadhani ungetazama kinyume chake. Tusiruhusu watawala kutumia nguvu dhidi ya raia pale ambapo njia nyingine zingeweza kutumika. Tusiruhusu kwa kisingizio cha kuwaridhisha wanasiasa wa chama tawala Jeshi la POlisi linavunja haki za msingi za kiraia. Hiili tusiliruhusu.



Unachosahau ni kuwa huko kote POlisi hawakujipeleka kimbelembele kuzuia wananchi kufanya kazi zao za kisiasa. Huko kote jeshi la POlisi halikusitisha shughuli za Chadema kinyemela kama walivyofanya Arusha.



Hapana, kuna wakati wananchi wanapokosa imani na vyombo vyao vya dola wana haki ya kuwakataa watawala wao kwa njia mbalimbali za kiraia. Haki hii haiwezi kuondolewa kwa vitisho. Nyerere mwenyewe alisema vizuri kabis akuwa wananchii wanapokosa imani na serikali yao na serikali hiyo inapokuwa ya kibabe dhidi yao, basi wananchi wana haki ya kuiondoa serikali hiyo kwa nguvu. Lakini kabla ya kufika huko wananchi wana haki ya kuipinga serikali hiyo na kuikataa pale inapotishia haki zao za msingi. Hii ndiyo falsafa iliyosababisha tuunge mkono ANC, FRELIMO, n.k. Ni muhimu kuelewa dhana hii ya kisiasa.

Serikali haiwezikuwa juu ya wananchi wake na viongozi wake hawawezi kutenda with impunity kwa sababu ni "serikali". Ni lazima kutambua kuwa haki ya kutawala inatoka kwa wananchi sasa serikali can not hold its citizens hostage or in contempt as it seems the Tanzanian government is doing now.





Hapana, tatizo ur trying to create a moral equivalency kati ya Jeshi la Polisi na wananchi wasio na silaha. You can not find that.



Usianze kunisingizia katika hilo; mimi ni muumini wa demokrasia na njia za kidemokrasia za kuwatumia ujumbe watawala. NInaamini kuwa hoja ndiyo njia ya kwanza kabisa ya kuwashawishi watawala. Lakini watawala wasiosikia la pili ni kuwapinga hadharani kwa njia halali za kiraia na kidemokrasia. Hizi ni njia za kisiasa, siyo makosa kama unavyoashiria. I'm proud to support the cause of democracy.



Lengo la maandamano lilikuwa kuipinga Serikali mkoani Arusha. Hayo mengine naona umekuja nayo tu. Maandamano yalikuwa ni ya kupinga serikali.



ajenda ilikuwa kupinga vitendo vya kuingilia uchaguzi wa meya wa Arusha na kupigwa kwa mbunge wa Arusha mjini. usisahau hilo.[/QUOT
Mzee Mwanakijiji!
Muda kwangu ni mchache na unanikwaza kujibu kila hoja lkn ninasema endeleni kuwahamasisha viongozi wa chadema watie watu mitaani kwa kila wasilokubaliana na serikali na waendelee kuwahamasisha watanzania kuandamana maana maandamano ndiyo mkakati mzuri wa kuleta mabadiliko.Mimi nalani kilichotokea Arusha na ninakubali kutokubaliana nawe kwenye hili kwani msimamo wangu pande zote mbili zina hisa juu ya kilichotokea Arusha.Mnaweza mkaspini mnavyoweza kwa kufikiri hatuelewi ni kwanini mlichagua maandamano badala ya mkutano na kwanini mlikubali hata watu watolewe kafara, Its all about media camera and attention deficit Disorder!
 
Jamani hii hivi ni tanzania au imekuwa burundi maana naanza kukumbuka enzi za akina bahima kwamba kikwete, mwema labda ni watusi na hawaogopi machafuko
 
Mzee Mwanakijiji!
Muda kwangu ni mchache na unanikwaza kujibu kila hoja lkn ninasema endeleni kuwahamasisha viongozi wa chadema watie watu mitaani kwa kila wasilokubaliana na serikali na waendelee kuwahamasisha watanzania kuandamana maana maandamano ndiyo mkakati mzuri wa kuleta mabadiliko.Mimi nalani kilichotokea Arusha na ninakubali kutokubaliana nawe kwenye hili kwani msimamo wangu pande zote mbili zina hisa juu ya kilichotokea Arusha.Mnaweza mkaspini mnavyoweza kwa kufikiri hatuelewi ni kwanini mlichagua maandamano badala ya mkutano na kwanini mlikubali hata watu watolewe kafara, Its all about media camera and attention deficit Disorder!

Kwa kiasi fulani Chadema wafanikiwa kupata media attention na possibly mtaji wa kisiasa; lakini at what cost? kama mchezo wnyewe ndio huu wa kutoana kafara huku wao viongozi wakijilengesha wakamatwe na polisi lakini wakibakia salama salmini?

Wanamageuzi wa mwanzo akina Mapalala, Mtikila, Marando na hata Mrema waliijaribu mbinu hii lakini watanzania wengi ni waoga na kila mambo yanapoharibika siku nyingine hutawaona.

Tutaendelea kuwaunga mkono kwenye keyboard za computer zetu lakini barabarani kwendeni wenyewe; hadi itokee kiongozi mmojawapo atolewe kafara nasi tumtangaze shujaa wa taifa!
 
Mzee Mwanakijiji!
Mnaweza mkaspini mnavyoweza kwa kufikiri hatuelewi ni kwanini mlichagua maandamano badala ya mkutano na kwanini mlikubali hata watu watolewe kafara, Its all about media camera and attention deficit Disorder!

Nakubaliana na wewe, kama Dr. Slaa alikuwa anaamini skuwa solution ya kwenda kuwatoa viongozi wenzake kituo cha polisi kwa nguvu ni sahihi, basi angewaongoza vijana wale kuelekea huko, ila kwa kuwa alijua gharama ya kitendo hicho yeye na wenzake wakaenda zao hotelini na kuwaacha vijana wale kwenda huko peke yao na matokeo yake wote tunayafahamu, huu ni ubinafsi usiokubalika kwa vipimo vyote vya ubinadamu.
Kwa kiasi fulani Chadema wafanikiwa kupata media attention na possibly mtaji wa kisiasa; lakini at what cost? kama mchezo wnyewe ndio huu wa kutoana kafara huku wao viongozi wakijilengesha wakamatwe na polisi lakini wakibakia salama salmini?

Wanamageuzi wa mwanzo akina Mapalala, Mtikila, Marando na hata Mrema waliijaribu mbinu hii lakini watanzania wengi ni waoga na kila mambo yanapoharibika siku nyingine hutawaona.

Tutaendelea kuwaunga mkono kwenye keyboard za computer zetu lakini barabarani kwendeni wenyewe; hadi itokee kiongozi mmojawapo atolewe kafara nasi tumtangaze shujaa wa taifa!

Katu hawapo tayari kwa hilo, kwao maisha yao ni bora zaidi kuliko waliotoka roho zao katika mpambano huo, kinachowauma zaidi wao ni kudharirishwa na polisi kwa kuwekwa selo kuliko kuuawa kwa vijana wale maskini, ebu tazama hapa mbunge wao anachosikitikia...

Mimi pia tatizo langu ni hawa Polisi kuwakamata viongozi wetu na kuwalaza selo.Hivi kweli wameshindwa kuwa na busara hata kidogo?Hivi wangekuwa ni viongozi wa CCM wangewakamata na kuwaweka selo?IGP,Andengenye mngefanya hivi kweli?Hivi kweli upolisi ni kutumia nguvu tu,hakuna kutumia akili?Mmelidhalilisha jeshi la polisi.Mbona mataifa yaliyoendelea hayafanyi hivi?hivi polisi maana yake nini?

Shame on you.
 
when police confrots unarmed demonstraters (armed with stones, sticks etc) and they use LIVE AMMUNITIONS instead of rubber bullets,tear gas etc etc, wakitumia virungu vyao kupiga vichwani badala ya ugokoni au miguuni, that is purely MURDER and criminal ASSAULT na wajue watalijibu hili baadae, siku za mungu si nyingi!
 
Nakubaliana na wewe, kama Dr. Slaa alikuwa anaamini skuwa solution ya kwenda kuwatoa viongozi wenzake kituo cha polisi kwa nguvu ni sahihi, basi angewaongoza vijana wale kuelekea huko, ila kwa kuwa alijua gharama ya kitendo hicho yeye na wenzake wakaenda zao hotelini na kuwaacha vijana wale kwenda huko peke yao na matokeo yake wote tunayafahamu, huu ni ubinafsi usiokubalika kwa vipimo vyote vya ubinadamu.


Katu hawapo tayari kwa hilo, kwao maisha yao ni bora zaidi kuliko waliotoka roho zao katika mpambano huo, kinachowauma zaidi wao ni kudharirishwa na polisi kwa kuwekwa selo kuliko kuuawa kwa vijana wale maskini, ebu tazama hapa mbunge wao anachosikitikia...



Shame on you.

Yule mgombea ubunge wa CCM aliyemfyeka mtama OCD ndani ya kituo cha polisi huko MASWA, hakuchukuliwa hatua yeyote!hili halina mjadala kuwa POLISI ni kampuni ya Chama gani!fedha za walipa kodi zimetumika kununua mavifaa tele tele ya kutuliza ghasia kwanini wang'ang'anie kutumia risasi za moto!na kwanini virungu vyao waelekeze vichwani na kuwashika makalio waandamanaji wa kike! they will pay for these crimes!
 
Hakuna mahali demokrasi inapofundisha watu wavunj sheria. Demokrasi gani iliyokuwa hakuna Tanzania?

Wamevunja sheria viongozi wa Chadema na hawa Raia masikini ya Mungu wameuliwa kwa kufata mkumbo, leo hii hata Chadema wawe ndio wanaongoza nchi hii, watawasaidia nini hawa raia? au Chadema wana miujiza ipi ya kuwarudishia roho zao hawa raia wanao wadanganya?

Watu kama wewe ni hatari sana katika jamii,huwa mnaandika bila kujuwa wala kufikiri,mradi ukae kwenye keyboard ukandamize utumbo wowote unaokujia kichwani baada ya kupata majani.

Mmmmmh hata South Africa kuna weusi walikuwa wanawatetea makaburu
 
Mchungaji Slaa na wenzake lazima wawe prscuted kwa kupinga order ya police na kusababisha vifo vya innocent civilians pia waadhibiwe kwa kwa kuvunja public order

Hawa chadema ni hatari sana tulisema siku nyingi hapa jf, nichama kinaongozwa na vilaza wasiokuwa na uzoefu wowote wa kuongoza hata idara ya kijiji



Chadema isipo dhibitiwa mapema italeta majanga zaidi hapa nchini, Jiulize kwa nini maandamano yamefanyiwa Arusha ? huko ndo kuna kabila la chama chao na makanisa yanyo endeshwa kwa tamaa na papara za kuingia Ikulu.

Chadema ni sawa na cancer lazima idhibitiwe

Ukienda na statement hii mahakamani umeshashindwa kesi kabla haijaanza. Utaulizwa swali, unasema kuwa hao citizens walikuwa innocent? Utajibu, ndio kama ulivyosema hapo mwanzo.

Watakuuliza unajua waliuawa na nini? Utasema risasi za moto. Watakuuliza, ni nani waliowapiga risasi? Obviously utasema ni polisi. Sasa kwa kuwa umekubali kuwa ni innocent civilians na wamepigwa risasi na polisi then ushahidi wako unakuwa ni msaada mkubwa kuwafunga hao askari wako including Said Mwema.
 
Kasheshe kubwa halikuwa wakati wa kuzuia maadamano; pamoja na kukamatwa viongozi wa Chadema, bali ni pale watu walipoamua kuandamana kuelekea Central na wahanga wengi wa fujo hizi ndipo walipotokea.



Hii ilikuwa suicide mission!
Pamoja na viongozi wa Chadema kukamatwa, hakuna hata mmoja wao aliyeumia katika vurugu hizo, mie naona wananchi wa kawaida tunatolewa kama kafara kutafutia mtaji wa kisiasa.
Na katika hili Chadema wamefanikiwa kwani serikali wanaelekea kukubali kurejea mezani kuzungumzia uchaguzi wa u-Meya wa Arusha.

Nadhani utakubaliana na mimi kuwa polisi walikuwa wanapiga watu hata waliokuwa kwenye magari wanaenda mkutanoni. Polisi walikuwa wanavunja vioo vya magari na kuwatoa watu na kuanza kuwapiga. Hebu niambie ni kweli jeshi la polisi lilikuwa na nia thabiti ya kulinda amani?
 
Nyi ndio mnataka mfike? Sisi tushaanza, tukiona tu, wavunja amani tuna fire.

I am not surprised, ni serikali inayoongozwa na Kikwete hii, ni lazima atafanya hivyo. Hana tofauti na Idd Amin, in my book!
 
Pasco!
Tatizo limesababishwa na pande zote mbili na hili sijalifumbia macho lkn kuwapa polisi walioko underground lawama wakiwa na wao walikuwa wanajihami kupoteza maisha yao vile vile si busara.Kwanini Mh. Dr Slaa ktk hali tata kama hiyo aliamua kuingiza watu wenye hasira mtaani na kibaya zaidi kwenda kituo cha polisi kutaka kutumia nguvu kuwatoa wenzao hivi kama wangefanya mkutano baadae wakaenda kuwatoa kwa njia zinazokubalika kiutaratibu kusingeepusha haya yaliyotokea.Mara nyingine matakwa na matamanio ya kutimiza malengo yao wanasiasa yanakwanza utumikaji wa busara ktk kufanikisha hio na yanatoa mwanya kwa udhaifu wa maamuzi kuchukua mkondo na kilichotokea Arusha kimesababishwa na hili.

You are lying sir, hakuna watu ambao walikuwa kituo cha polisi kuwatoa waliokamatwa kwa nguvu na kama ingekuwa hivyo polisi wa Arusha wasingeweza kuuzuia ule umati. Na sidhani kama kuna polisi angebaki kwenye hicho kituo, wote wangekimbia. Polisi walikuwa wanawapiga watu risasi za moto far off from the police station.

Unachotaka kufanya hapa ni kujustify un armed citizens kupigwa na kuuwawa na polisi. Hilo la kuuwa na kupiga watu hapa Tanzania lipo sana tu usijifanye hujui. Jeshi la polisi la Tanzania ni moja kati ya majeshi yenye uonevu na kutokufuata sheria hapa duniani. I was in Zimbabwe na walishangaa sana kusikia kuwa Tanzania unaweza kuiba kuku ukapewa kesi ya mauaji. Pamoja na uozo uliopo huko hili liliwashangaza sana!

So please be honest, polisi hawakuwa na justification yoyote ya kupiga na kuua watu mpaka waliokuwa kwenye magari kwa kuvunja vioo na kuwatoa ndani ya magari. Tell me hao waliokuwa kwenye magari wanaenda mkutanoni huku vioo vya magari vimefungwa walikuwa wanaleta fujo gani.
 
wewe Selemani naona huelewi hoja ya MM; kwani polisi ni nani kukuamulia usiandamane? Kazi ya polisi si kuua watu bali kulinda...kabla ya polisi kuingilia hakuna mali wala mtu aliyekuwa amekufa au kupigwa....kifo cha watu watatu ni matokeo ya polisi kuingilia maandamano ya amani!

We are a land of laws, rules, and regulations. This is an example of disgruntled politicians, using their rhetorical prowess to push the public to the limit and argue them to disobey the law.

Kama polisi walisema maandamano hakuna, kwanini muandamane?

Inalilahi waina lillah rajiun (Hakika sisi ni wa Allah, na kwake tutarejea)
 
Tupo Imara!

Unyama na Ukatili wa Serikali ya Jakaya Kikwete umevuka mipaka. Polisi walichokifanya Arusha ni unyama mtupu, wameua raia bila huruma..risasi za moto kwa raia wasio na hatia..Inauma sana..mimi ni mkazi wa Arusha na nimeshuhudia kwa macho yangu ubabe na unyama waliotumia. Haya yote yasingetokea ni pale polisi walipoamua kuua raia. Sasa wanasema watu wawili..Hebu tembelea hospitali ya Mount Meru ujionee mwenyewe, watu walivyopigwa risasi, idadi kamili ya awali ilikuwa watu nane waliouwawa na polisi, na hii inaweza kuzidi zaidi kutokana na majeruhi walio katika hali mbaya.

Sasa Kikwete furahia kama ulivyofurahia kupongeza mayor wako wa CCM Arusha tarehe 17 December 2010 pale Kibo Palace Hotel..Haya yote yana mwisho..Saidi Mwema Arusha tupo imara njooni tena, TUPO TAYARI KUFA KWA KUDAI HAKI YETU..sasa tumezidi kuwa imara, na nguvu mmetupa ujasiri ambao hatuogopi kifo tena..Mngeufuta ushauri wa mwenzenu Edward Lowassa, anafahamu wananchi wa Arusha vema. Kwako Makamba, Heri kijana mwenye busara, kuliko mzee mpumbavu...figure this out. Andengiye..huna tofauti na polisi wa kikaburu wa kimabavu wa Afrika Kusini..unatumiwa na hao makaburu wa Ikulu, Kikwete and his fellow crooks.


Kikwete acha unafiki, Madaraka yamekushinda achia nchi, achia wenye uwezo..Hujui unachokifanya..Elewa haki ya watu haipotei bali inachelewa. Hakika damu ya watu iliyomwagika Arusha itakulilia wewe na familia yako



Ndugu zangu wanatanzania tudai haki bila woga..kama watu wa Arusha!
Don't stay aside and let others fight for your rights..
It is time to wake up and fight for injustice anywhere in Tanzania..


Huyu Kikwete hatumtaki kabisaa natumaini anaelewa hilo kwa sasa..




 
Tulia kidogo huu ndo ukubwa. Pole sana kwa unyama ambao nami umenigusa. Tuko wote hapa mjini mkuu na mabomu yalinizingira nikafikiri kiama kimefika.

Mimi nina hasira ya ku.#%$@ mtu haswa andengenye na OCD Zuberi. ningeweza kujifanya inzi au panya hawa jamaa wasingekuwepo.!!!!

Damu walizomwaga na kusingizia CHADEMA Mungu ndiye aliyeona na sisi. Fujo walizosababisha na kusingizia CHADEMA Mungu ndo anajua.

Andengenye anatafutwa na Zuberi ili wawajibu wana Arusha kisa cha kuwaua ndugu zao na marafiki zao .

Hasira hizi hazitaisha ila watu wamejipanga next time polisi watakapoingilia ili wafe na polisi

An injury to one is an injury to all haya ndio machungu wana arusha waliyo nayo.
Mungu asaidie polisi wasijaribu tena kwani kosovo itakuwa sifuri
 


What I am condemning is that one power, with a president [Jakaya Kikwete] who has no foresight, who cannot think properly, is now wanting to plunge our Tanzania into a civil war and political unrest..He always loughs even for serious issues. I think he is always happy to see fellow citizens are suffering what happened in Arusha he is 100% responsible


He should by now know, Tanzania is starving for democracy and respect for human rights, a country freed from the horrors of poverty, hunger, deprivation and ignorance. And his administration is not ready to take our country forward. New constitution and fresh election is what we need.. With this current administration from till 2015 is a very tough road ahead. He has to let others who are capable to run the country.

 
Back
Top Bottom