Tupo Imara!
Unyama na Ukatili wa Serikali ya Jakaya Kikwete umevuka mipaka. Polisi walichokifanya Arusha ni unyama mtupu, wameua raia bila huruma..risasi za moto kwa raia wasio na hatia..Inauma sana..mimi ni mkazi wa Arusha na nimeshuhudia kwa macho yangu ubabe na unyama waliotumia. Haya yote yasingetokea ni pale polisi walipoamua kuua raia. Sasa wanasema watu wawili..Hebu tembelea hospitali ya Mount Meru ujionee mwenyewe, watu walivyopigwa risasi, idadi kamili ya awali ilikuwa watu nane waliouwawa na polisi, na hii inaweza kuzidi zaidi kutokana na majeruhi walio katika hali mbaya.
Sasa Kikwete furahia kama ulivyofurahia kupongeza mayor wako wa CCM Arusha tarehe 17 December 2010 pale Kibo Palace Hotel..Haya yote yana mwisho..Saidi Mwema Arusha tupo imara njooni tena, TUPO TAYARI KUFA KWA KUDAI HAKI YETU..sasa tumezidi kuwa imara, na nguvu mmetupa ujasiri ambao hatuogopi kifo tena..Mngeufuta ushauri wa mwenzenu Edward Lowassa, anafahamu wananchi wa Arusha vema. Kwako Makamba, Heri kijana mwenye busara, kuliko mzee mpumbavu...figure this out. Andengiye..huna tofauti na polisi wa kikaburu wa kimabavu wa Afrika Kusini..unatumiwa na hao makaburu wa Ikulu, Kikwete and his fellow crooks.
Kikwete acha unafiki, Madaraka yamekushinda achia nchi, achia wenye uwezo..Hujui unachokifanya..Elewa haki ya watu haipotei bali inachelewa. Hakika damu ya watu iliyomwagika Arusha itakulilia wewe na familia yako
Ndugu zangu wanatanzania tudai haki bila woga..kama watu wa Arusha!
Don't stay aside and let others fight for your rights..
It is time to wake up and fight for injustice anywhere in Tanzania..
Huyu Kikwete hatumtaki kabisaa natumaini anaelewa hilo kwa sasa..