Wazo lenye mantiki: Bil 5.4 zilizotaifishwa toka biashara haramu ya upatu zielekezwe wilayani Chato kuboresha huduma ya maji

Nyankurungu2020

JF-Expert Member
Oct 2, 2020
4,086
6,568
Natanguliza kutoa onyo kwa Watanzania kuacha wivu hasa kwa wakazi wa mkoa wa Geita linapokuja suala la maendeleo.

DPP ametumia mamlaka aliyonayo kisheria na kuteleza hukumu ya utaifishaji wa bil 5.4 ambazo zilipatikana kwa biashara haramu ya upatu.

Mimi kama mkazi wa mkoa wa Geita, eneo la Bukoli niliamua kwenda Chato kuwaona jamaa zangu, jambo lililonishangaza ni shida kubwa ya upatikanaji wa maji.

Ziwa lipo karibu sana hata Km mbili hazifiki, pamoja na mtandao wa maji kuwepo kwenye makazi ya watu, maji hayatoki kwenye mabomba na hutoka kwa mgao,nyakati zingine usiku wa manane.

Hivyo basi, naomba mbunge wa Chato achangamkie fursa ya hii pesa ambayo imepatikana, aombe ipelekwe Chato ili maji yawe yanatoka wakati wote. Maana inakuwa aibu kama vile Chato ni mbali na ziwa.

N.b: Chato ni sehemu ya Tanzania. Ndio maana zilipojengwa flyover Dar wakazi wa Geita wahakumaindi.
 
Kama ziwa lipo karibu basi nyinyi hamna shida ya maji, kuna maeneo hata hilo ziwa hawajawahi kuliona..
wanatakiwa waombe kuchimbiwa visima, sisi tunahitaji maji ya uhakika,suala la kuweka matank makubwa na kusambaza masaa 24.
 
Natanguliza kutoa onyo kwa watanzania kuacha wivu hasa kwa wakazi wa mkoa wa Geita linapokuja suala la maendeleo...
Mleta post nimekuelewa sana,

Lakini kila muomba chumvi anaombea chungu chake,

Mbona unaombea chungu Cha mwingine?

Hiyo ni akili au matope?

Unge hamasisha hizo pesa zilete maji kwenu, huoni hapo Bukoli na Segese na Kakola,mnavyochangia na mifugo kunywa maji ?

Sisi watu wa Chato tunaweza kuuza uwanja wetu wa Ndege na tukapata maji Safi na salama.
 
Kwanini isijenge madarasa ili wale wanafunzi walokosa kujiunga kidato cha kwanza kisa uhaba wa madarasa wapate kusoma
 
Back
Top Bottom