Wazo la kukopa fedha benki

Wazo la kukopa fedha benki

  • Kila kitu kina umuhimu, na kuishi pia ni muhimu; kama umepangiwa kuishi miaka 3 ijayo na hukufaidi, inakuwa haina maana.
  • Chukua mkopo, weka chuma barabarani.
 
Nina wazo la kununua gari ndogo ya kutembelea.Nataka kukopa benki ili nipate fedha za kununua gari hiyo.Natakiwa nikope kama milioni 22 .Hili wazo la kukopa fedha ili ninue gari toka japani mnalionaje ni zuri au baya.Mshahara wangu ni kama laki 600000 kwa mwezi
Unafanyia nini gari?
Unaendea kazini?
Hauwezi kusave akanunua gari cash?

Jiulize haya maswali.

Binafsi ingekuwa mimi kwa mshahara huo nisingenunua gari kwa mkopo ningesave ninunue cash.....nachukia mawazo ya kulipa mkopo usioniingizia kitu.

Gari ukishaiendesha mwezi unaridhika na kugundua hukuwa na haja ya kulikimbilia kwa mkopo. Hakuna raha kama kuishi au kuendesha gari au biashara isiyo na mkopo.
 
Kwa kifupi. Kopa nunua gari.
Kopa chini ya miaka 4.
Usinunue gari Kwa mtu. Chukua used from Japan.
Chukua ndinga yenye cc chini ya 1500.
Gari Kampuni ya Toyota.
 
Nina wazo la kununua gari ndogo ya kutembelea.Nataka kukopa benki ili nipate fedha za kununua gari hiyo.Natakiwa nikope kama milioni 22 .Hili wazo la kukopa fedha ili ninue gari toka japani mnalionaje ni zuri au baya.Mshahara wangu ni kama laki 600000 kwa mwezi
Kwanini usikope kununua gari la biashara?
 
Nina wazo la kununua gari ndogo ya kutembelea.Nataka kukopa benki ili nipate fedha za kununua gari hiyo.Natakiwa nikope kama milioni 22 .Hili wazo la kukopa fedha ili ninue gari toka japani mnalionaje ni zuri au baya.Mshahara wangu ni kama laki 600000 kwa mwezi
Matunzo ya gari ni zaidi ya matunzo ya familia kazi kwako mkuu
 
Kaka muda wa kumiliki gari ni huu nina miaka 45 bado 15 nistafu.Haitakuwa vizuri nimiliki gari baada ya miaka hiyo
Duh,
Kama huna presha na kisukari ndo unavitafuta kwa bidii sasa.

Yaani ukatwe marejesho ya 400k ubakie na 200k, hapo hapo utoe gharama za mafuta, matengenezo ya gari, bima, nk, na bado una familia ya watu 5 !!

Labda kama una vyanzo vingine vya kipato ..
 
Mkuu kukopa kununua gari ni risk kidogo! Mimi nafikilia kukopa nianzishe biashara ya duka la madawa! Sasa wew kopa hrf anzisha hardware au duka la jumla la vyombo! Nipo paleee na kuzoom baada ya hiyo biashara ukizungusha ndinga kaliiiiiii na mamiloooo pemben
 
Jan japani wananafuu ya bei?
Screenshot_20250817-190950.png
Screenshot_20250817-190910.png
Screenshot_20250817-190826.png
 
chukua hela, kuna mwamba alikufa halafu salary slip yake kaina kirusi wakati wengine salary slip ni mkeka treni benki zimejaa cha msingi achana na mambo za top up
Top up mbaya sana bora kuanza mkopo mpya benki nyingine
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom