Wazo la kukopa fedha benki

Wazo la kukopa fedha benki

Kaka muda wa kumiliki gari ni huu nina miaka 45 bado 15 nistafu.Haitakuwa vizuri nimiliki gari baada ya miaka hiyo
Unakaa mkoa gani labda tuanzie hapo..mfano kuna badhi ya maeneo maisha ni nafuu..hapo ndio nitajua pakuanzia....kuna vyanzo vya mapato tofauti na mshara ?
 
Ukikopa 22m watakupa 20m then 2m watakata kwa ajili ya processing etc

Baada ya apo watakukata kila mwezi almost 360k, kwa miaka tisa utalipa kama milion 42 hivi.

So ni kama unawalipa mara mbili ya hela uliokopa.

Mimi sipo kwa ajili ya kukushauri ukope au usikope, me nakuelezea tu pesa utakayowalipa in case kama ulikua hujui namna wanavo calculate.

Maamuzi ni yako

Asante
 

Attachments

  • IMG_0332.png
    IMG_0332.png
    498.9 KB · Views: 23
Nina wazo la kununua gari ndogo ya kutembelea.Nataka kukopa benki ili nipate fedha za kununua gari hiyo.Natakiwa nikope kama milioni 22 .Hili wazo la kukopa fedha ili ninue gari toka japani mnalionaje ni zuri au baya.Mshahara wangu ni kama laki 600000 kwa mwezi
We kama unataka kununua gari, Kwa kuanzia usinunue gari ya bei kubwa hivyo. Tafuta Fundi mzuri (wapo) nunua gari zilizotumika hapa nchini. Achana na gari kubwa (Alphad), nunua gari ndogo ya watu 5 yenye chini ya 1,700cc, mf. Toyota Raum unaweza ipata ya 6M yenye Hali nzuri kabisa, ukafanya marekebisho kidogo ukaendelea kula maisha.
Kwan hiyo familia utakuwa unaipeleka shule Kila siku?
Hili gari itakuwa na low running cost. Epuka magari unique, nunua gari common.
Usichukue mkopo wa muda mrefu chukua at least 3-5 yrs.
Ukibahatisha gari nzuri ya mkononi unaweza usione tofauti na alieagiza Japan baada ya mwaka 1.
"Kula Raha ukiwa na nguvu, warithi hawana huruma"
(Haya ni mawazo yangu ya kimaskini)
 
Nina famili jumla tuko watano.Kwa kiasi hicho cha pesa itanibidi nikope kwa muda wa miaka 9.Najua ni muda mrefu nawafaidisha benki lakini sina namna.Moyo unataka gari mpya toka Japani.Alphard,Wishi au yoyote yenye siti saba au nane
Izo gari zitakutesa sana kwani cc ni kubwa sana kama alfard 2000cc na wish 1990 maguta utamudu?kwa mshahara huo achana kabisa na wazo la gari nunua pikipiki utamudu na utanishukuru baadaye

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Nina famili jumla tuko watano.Kwa kiasi hicho cha pesa itanibidi nikope kwa muda wa miaka 9.Najua ni muda mrefu nawafaidisha benki lakini sina namna.Moyo unataka gari mpya toka Japani.Alphard,Wishi au yoyote yenye siti saba au nane
Hapo kwa mm mzoef wa mikopo, chukua milion 8 kwa muda wa miaka 3, baada ya hapo data chuma kwa mtu tena chukuq raum, ist runs au allex, utanishukuru baadae. Miqka 9 no mongi sana kwa mtumiahi af mwenye familiar kubwa hvyo utajutia.
 
Ukikopa 22m watakupa 20m then 2m watakata kwa ajili ya processing etc

Baada ya apo watakukata kila mwezi almost 360k, kwa miaka tisa utalipa kama milion 42 hivi.

So ni kama unawalipa mara mbili ya hela uliokopa.

Mimi sipo kwa ajili ya kukushauri ukope au usikope, me nakuelezea tu pesa utakayowalipa in case kama ulikua hujui namna wanavo calculate.

Maamuzi ni yako

Asante
Ni kwel yaan aside na haraka achukue miaka mi 3 tena milion 8 au 9 achukue gar kwa mtu
 
Nina wazo la kununua gari ndogo ya kutembelea.Nataka kukopa benki ili nipate fedha za kununua gari hiyo.Natakiwa nikope kama milioni 22 .Hili wazo la kukopa fedha ili ninue gari toka japani mnalionaje ni zuri au baya.Mshahara wangu ni kama laki 600000 kwa mwezi
Kijana, wakianza kukukata hela yao walio kukopa, haitapungua 350 makato ya mkopo, na hapo hapo utaiona hiyo gari kama ina gundu. Ukumbuke laki 6 ni sawa na laki 2 yakipita makato yote.(Paye, Nssf,Nssf, etc) Sasa hiyo gari itahitaji kuhudumiwa service, mafuta, na kuna hapa na pale umepigwa pasi na wahuni wamekushona bampa wamekimbia. Soon Utaichukia hiyo kazi utakosa morale ya kazi utaanza kuwa mwizi utapata stress. Sikukatishi tamaa ya kununua gari, nakupa matokeo ya baada ya huo mkopo ambao nao hautapata hiyo 22 utapewa 19. Na mwezi huo huo wanaaza kukufyatua kwenye s.slip
 
Weka akiba kila mwezi ya kiasi cha tsh 300,000 hadi 400,000

Ukiweka akiba ya 300,000 toka ktk mshahara wako kwa miezi 12 utakuwa na kiasi cha tsh. 3,600,000.

Kwa miaka 9 hadi 10 ya mkopo utakuwa na akiba ya 32,4000,000. Kwa miaka 9 na kwa miaka 10 utakuwa na akiba ya 36,000,000

Hapa unakuwa umebakisha miaka 5 uachane na ajira. Una nunua gari kali


Ikiwa utawekeza akiba ya 400,000 kila mwezi.

Kwa miezi 12 ni 4,800,000.

Kwa miaka 9 ni 43,200,000

Kwa miaka 10 ni 48,000,000

Hapa unakuwa umebakisha miaka michache ya kuachana na ajira, unarudi ktk matumizi ya 600,000 yako au unaweza kuta mshahara umeongezeka mara dufu na vyeo vya kumwaga na maposho bila idadi
Hizo hesabu nzuri ukiwa unandika script ya movie yani ukiigize ila kiuhalisia ngumu sana
 
Wengine tumejitahidi na tumeweza kwa zaidi ya 78% mpaka sasa. Bado hatujatoka katika malengo
Kwa watumishi sisi tunajua ni vigumu sana kuweka pesa kaka na ndio maana tunakimbiliaga mikopo. Japo kua tunatakiwa kua na elimu bora juu ya mikopo. Mikopo ya chini ya miaka 3 hua ni rafiki sana, pia usitake jambo kubwa kwa haraka, kama mtoa maada anataka kuagizq,, namshauri aanze tu kununua gari kwa mtu na ni gari ndogo, ili aweze ku enjoy maisha ya kua na gari
 
Nina wazo la kununua gari ndogo ya kutembelea.Nataka kukopa benki ili nipate fedha za kununua gari hiyo.Natakiwa nikope kama milioni 22 .Hili wazo la kukopa fedha ili ninue gari toka japani mnalionaje ni zuri au baya.Mshahara wangu ni kama laki 600000 kwa mwezi
600,000 × 12 = 7.2m ndiyo Net income yako per Year.
Mkopo wa mil 22 ni wa miaka si chini ya miaka 5.
Je utaweza kuishi na Sh 350,000 baada ya makato?
HIyo gari kwa mwezi itakula si chini ya 100,000.
Je utaishi na net ya 250k kwa mwezi?

Kama una income nyingine fine, othewise achana na huo ujinga.

Nakushauri kopa 10m tafuta shamba heka 5 ( si kiwanja) utanikumbuka baada ya miaka 10.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom