Waziri wa fedha hawezi kutamka neo TRILIONI

Jambo la muhimu ni sabstance ya yale aliokuwa anasoma na sio pronounciation!! After all yeye ni Mnyalukolo first and foremost!!

sawasawa mkuu pronunciation sio ishu...kazi na matokeo chanya ndo kinahitajika!!
 
kama ilivyo kwenye lugha ya kiingereza.....kuna kiingereza cha marekani, jamaika,india,naijeria.......kiswahili nacho ni hivyohivyo....cha kichaga, kisukuma,kihehe,kimakonde nk......msishangae sana
 
Halafu wanamsema Profesa Shivji na wanataka kumjua kama ni mtanzania? Ukishangaa ya !!...utayaona !!...
 
Budget Tanzania Tsh trillioni 13. Budget Kenya Ksh triliioni 1.4=Tsh trilionn 26. All things being equal Kenya wanapiga hatua mbili mbele Tanzania hatua moja.
Hivi % inayotoka kwa wafadhili kwenye hiyo budget ya Kenya ni kiasi gani? Nakumbuka waliwahi kususiwa lakini wakasonga mbele kama hakuna kilichotokea.
 
Nakubaliana na wewe umesema kweli!!!, yeye kabisa hilo ni tatizo la Kihehe tu ila cha msingi je mada anaijua anayoiwasilisha au nako ndiyo hakuna kitu? Ila kwa ujumla sijaipenda budget hii haijaenda shule. Bajeti ya kuongeza kodi kwenye petty things kama drinks, sigara etc wanaacha madini na bidhaa chungu nzima na misamaha ya kutupwa katika kodi na bila kuziba minya ya upotevu wa fedha pale bandarini na kwenye, weigh bridges, TRA etc . Nadhani mawaziri wa CCM wote siyo creative hebu tusikie budget mbadala ya CDM J3 I hpo that will address issues better.
 
naona watu sijui huwa hampambanua mambo kabla ya kuleta thread zenu hapa. Hivi unajua maana ya neno trillioni?
wala Mgimwa hajakosea yupo sahihi kabisa maana trillioni ni millioni millioni moja, mathalani tarakimu hii 700,000,000 husomeka kama millioni mia saba,700,000,000,000 kama millioni elfu saba n.k.
 
Hapa JF ni sawa na google. Kila alilokosea kulitamka vizuri limewekwa.
 
Kuthibitisha kuwa amesoma zamani wakati fedha ina thamani na ma figure makubwa sana walikuwa hawayatumii waziri wa fedha Dk William Mgimwa ameshindwa kutamka neno trilioni hata mara moja wakati anasoma vifungu vya bajeti na kuishia kusema milioni laki moja... au bilioni elfu moja...

My Take: huyu jamaa hajazoea mahela yenye figure kubwa na digit nyingi kama akina Shimbo tukiskia tu ameagiza ma Vogue mengi kama Mkullo tutajua ni hela yetu imekwapuliwa

ktk kufisadi kwake bado hajafisadi kiasi kikubwa namna hiyo so subiri baada ya muda akishafikisha wizi kama huo ataweza kutamka fresh tu.
 
Tujaribu kua critical thinkers. Budget aliyoiwakilisha Waziri hajaiandaa yeye, mchakato wa kuandaa budget unaanza mwezi January yeye kateuliwa hivi karibuni tusitegemee kuona matokeo makubwa sana kutokana na inputs zake labda kwa budget itakayokuja
 
huyo ni Dr aliyeipatia through diploma, sio degree, unapiga kwanza certificate, unapiga diploma, unapiga advanced diploma, then unajifanya sawa na mtu wa masters, unapiga udoctor sasa.....namshauri awe makini kwasababu watu wana matumaini makubwa sana juu yake kwamba yeye ni mzuri kuliko mkulo...sasa akifanya mchezo watu wakapoteza imani kwake ataona iyo ofisi aliyokalia ni chungu.
 
Kama wewe mwazisha thread huwezi neno ""NENO"umeandika "NEO"...yale yale asiyekuwa na dhambi awe wa kwanza kurusha jiwe....
Acheni mambo ya ajabu umepost kwenye jukwaa la Siasa bora uke post kwenye jukwaa la viroja tungechangia kwa misingi ya viroja na utani.Hapa discuss substance ya alichosema
 
sure jamaa ana tatizo la mother tongue,ni mhehe wa kalenga huyu bwana. nyie subirini tu akianza ziara za kwenda kusaini mikataba feki atarudi mother toungue kwishiney
 
Bengi badala ya Bank ni mother tongue imemkaa sana ila tumpe muda labda ni mzuri atasadia na uzoefu wake alionao!!
 
Back
Top Bottom