Waziri wa Elimu amtangaza Dkt. Mpango kuwa Mgeni Rasmi Tuzo za Taifa za Mwalimu Nyerere ya Uandishi Bunifu

Waziri wa Elimu amtangaza Dkt. Mpango kuwa Mgeni Rasmi Tuzo za Taifa za Mwalimu Nyerere ya Uandishi Bunifu

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
4,783
Reaction score
14,975
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango, kuwa mgeni rasmi katika hafla ya utoaji wa Tuzo ya Taifa ya Mwalimu Nyerere ya Uandishi Bunifu, itakayofanyika Aprili 13, 2025 Jijini Dar es Salaam.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, Aprili 7, 2025 ambapo ameongeza kuwa hafla hiyo inalenga kutambua na kuenzi mchango wa Waandishi Bunifu katika kukuza lugha, utamaduni, na fikra za maendeleo nchini.

Tuzo hiyo, iliyopewa jina la Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, ni ishara ya kumuenzi kutokana na mchango wake mkubwa katika Uandishi Bunifu.

Prof. Mkenda amesema kuwa maandalizi ya hafla hiyo yamekamilika na kwamba ni heshima kubwa kwa Sekta ya Elimu kuwa na ugeni huo wa juu unaoonyesha namna ambavyo serikali inatambua mchango wa uandishi bunifu katika kukuza lugha ya Kiswahili, maarifa, na utamaduni wa taifa.


Amesema kuwa Tuzo ya Mwalimu Nyerere ya Uandishi Bunifu ni miongoni mwa njia bora za kuenzi fikra, falsafa na maono ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, ambaye aliweka msingi wa matumizi na ukuzaji wa lugha ya Kiswahili kama nyenzo ya elimu, umoja na maendeleo ya jamii ya Watanzania.

“Tuzo hii ni heshima kwa Mwalimu Nyerere lakini pia ni jukwaa mahsusi kwa waandishi chipukizi na wakongwe kuonyesha umahiri wao katika nyanja mbalimbali za uandishi kama vile riwaya, ushairi, hadithi za watoto na tamthiliya,” amesema Prof. Mkenda.

WhatsApp Image 2025-04-07 at 13.14.57_d71f93f9.jpg

Upande wa Mwenyekiti wa Kamati ya Tuzo ya Taifa ya Mwalimu Nyerere ya Uandishi Bunifu, Profesa Penina Mlama, ametangaza majina 10 ya waandishi wa kazi bunifu zilizokidhi vigezo kwenye nyanja nne za tuzo hiyo.

Profesa Mlama alitangaza majina na kazi zilizokidhi vigezo, mbele ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda jijini Dar es Salaam leo Aprili 7, 2025 wakati wa mkutano na waandishi wa habari kwenye ofisi za Taasisi ya Elimu Tanzania (TET).
WhatsApp Image 2025-04-07 at 13.16.14_97d8c55a.jpg

WhatsApp Image 2025-04-07 at 13.15.47_5eac0a3c.jpg
Amesema huu ni msimu wa tatu wa utoaji wa tuzo ya Mwalimu Nyerere ya uandishi bunifu ambapo zawadi kwa mshindi wa kwanza ni Tsh. Milioni 10, wa pili Tsh. Milioni 7 na watatu Tsh. Milioni Tano.

Ameeleza tuzo hizo zimegawanyika kwenye nyanja nne ambazo ni ushairi, riwaya, hadithi za watoto na tamthiliya.

“Kama tunavyofahamu, tuzo hii ilianzishwa na serikali chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na inaratibiwa na Taasisi ya Elimu Tanzania… huu ni mwaka wa tatu wa utoaji wa Tuzo hii.
WhatsApp Image 2025-04-07 at 13.16.58_2bf92ba7.jpg
“Mchakato wa uendeshaji wa Tuzo hii umejumuisha upokeaji wa miswada na usomaji wa miswada hiyo na jopo la majaji. Mchakato huu umeendelea kwa kipindi cha mwaka mzima,” alisema Profesa Mlama na kusisitiza kwamba utoaji wa tuzo ya mwaka huu utafanyika Aprili 13, 2025 kwenye Ukumbi wa The Super Dome uliopo Masaki, Dar es Salaam.”

Pia soma ~ Hafla ya Utoaji Tuzo ya Taifa ya Mwalimu Nyerere ya Uandishi Bunifu, Aprili 13, 2025
 
Back
Top Bottom