Lady Whistledown
JF-Expert Member
- Aug 2, 2021
- 1,024
- 1,612
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula ameagiza kuondolewa kwa Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) wa wizara hiyo, Venance Mwolo akisema hatoshi katika majukumu hayo.
Waziri Mabula ametoa maelekezo hayo kwa Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Dk Allan Kijazi leo Jumanne, Septemba 6, 2022 mbele ya waandishi wa habari.
"Mkurugenzi wa Tehama simtaki katika wizara ya ardhi, ameshindwa kutekeleza majukumu yake. Katibu Mkuu (Dk Allan Kijazi), wasiliana na utumishi wafanye utaratibu wa kuleta mtu mwingine," amesema.
Ametaka mkurugenzi atakeyeletwa kuifanya kazi hiyo ahakikishe anaendana na kasi ya Serikali katika matumizi ya Tehama.
Chanzo: Mwananchi
Waziri Mabula ametoa maelekezo hayo kwa Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Dk Allan Kijazi leo Jumanne, Septemba 6, 2022 mbele ya waandishi wa habari.
"Mkurugenzi wa Tehama simtaki katika wizara ya ardhi, ameshindwa kutekeleza majukumu yake. Katibu Mkuu (Dk Allan Kijazi), wasiliana na utumishi wafanye utaratibu wa kuleta mtu mwingine," amesema.
Ametaka mkurugenzi atakeyeletwa kuifanya kazi hiyo ahakikishe anaendana na kasi ya Serikali katika matumizi ya Tehama.
Chanzo: Mwananchi