DOKEZO Waziri Ummy sisi Watumishi tuliohudumia Wagonjwa wa UVIKO-19 Amana Hospital hatujalipwa posho mpaka leo

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Nadhani mnakumbuka Hospitali ya Amana ilishiriki kuhudumia Wagonjwa wa COVID-19 hiyo ilikuwa kuanzia Mwaka 2020, sasa katika ile kazi kulikuwa kuna posho ambayo Watumishi na Vibarua ilitakiwa tupewe.

Makubaliano ya awali yalikuwa kulipwa Shilingi 50,000 kwa siku japo baadaye walishusha hadi kuwa 40,000 kwa siku bila makubaliano y pande mbili, tukaona poa tu.

Tulikaa muda mrefu bila kupata malipo hayo, baada ya kakuanza kulalamika kwa uongozi kish taarifa kufika hadi Wizara ya Afya, ndipo Machi 2023 malipo yakatolewa kwa watu 37 tu huku wengine wengi tukibaki hatujui hatima yetu, idadi kamili siiikumbuki kwa kuwa tulikuwa wengi na vitengo tofautitofauti.

Wale Watumishi ambao hatukupata tukasikia tutapewa mwezi unao fuata yaani baada ya Machi 2023 lakini mpaka leo tunauanza Mwaka 2024 hatujapewa na hatujui kama hilo litatokea.

Upande wa vibarua waliingia hasara ya kukopa vitu na hela wakiamini hela itaingia na watarejesha mikopo yao lakini haijawa hivyo.

Ukiulizia au kufatilia malipo hayo unaonekana mkorofi, kwa sisi vibarua ukiulizia yanakukuta makubwa, unasimamishwa kazi kabisa au unaweza kutengenezewa mazingira ya kufukuzwa.

Naomba ujumbe huu uwafikie viongozi wa juu Serikalini akiwemo Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu aone namna ya kutusaidia ili tupate haki zetu kwani baadhi wameshaacha kazi au wameachishwa bila kupata stahiki zao.
 
Nadhani mnakumbuka Hospitali ya Amana ilishiriki kuhudumia Wagonjwa wa COVID-19 hiyo ilikuwa kuanzia Mwaka 2020, sasa katika ile kazi kulikuwa kuna posho ambayo Watumishi na Vibarua ilitakiwa tupewe.

Makubaliano ya awali yalikuwa kulipwa Shilingi 50,000 kwa siku japo baadaye walishusha hadi kuwa 40,000 kwa siku bila makubaliano y pande mbili, tukaona poa tu.

Tulikaa muda mrefu bila kupata malipo hayo, baada ya kakuanza kulalamika kwa uongozi kish taarifa kufika hadi Wizara ya Afya, ndipo Machi 2023 malipo yakatolewa kwa watu 37 tu huku wengine wengi tukibaki hatujui hatima yetu, idadi kamili siiikumbuki kwa kuwa tulikuwa wengi na vitengo tofautitofauti.

Wale Watumishi ambao hatukupata tukasikia tutapewa mwezi unao fuata yaani baada ya Machi 2023 lakini mpaka leo tunauanza Mwaka 2024 hatujapewa na hatujui kama hilo litatokea.

Upande wa vibarua waliingia hasara ya kukopa vitu na hela wakiamini hela itaingia na watarejesha mikopo yao lakini haijawa hivyo.

Ukiulizia au kufatilia malipo hayo unaonekana mkorofi, kwa sisi vibarua ukiulizia yanakukuta makubwa, unasimamishwa kazi kabisa au unaweza kutengenezewa mazingira ya kufukuzwa.

Naomba ujumbe huu uwafikie viongozi wa juu Serikalini akiwemo Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu aone namna ya kutusaidia ili tupate haki zetu kwani baadhi wameshaacha kazi au wameachishwa bila kupata stahiki zao.
Eti wanamuita shujaa sijui legacy
 
Haya Nayo Maajabu Jamani Watu Hawajapewa Stahiri Zao Wakati Kuna Rundo La Viongozi
Waziri Wa Afya
Mganga Mkuu Wa Serikali
Katibu Mkuu Wizara Ya Afya
RMO
DMO




Kali Kuliko Yote Mabeberu Walitoa Pesa Kwaajili Ya UVIKO 19 Ugumu Ulikuwa Wapi Kuwalipa Chap Chap. TANZANIA Chachu Mno Kama Ndimu
 
Haya Nayo Maajabu Jamani Watu Hawajapewa Stahiri Zao Wakati Kuna Rundo La Viongozi
Waziri Wa Afya
Mganga Mkuu Wa Serikali
Katibu Mkuu Wizara Ya Afya
RMO
DMO




Kali Kuliko Yote Mabeberu Walitoa Pesa Kwaajili Ya UVIKO 19 Ugumu Ulikuwa Wapi Kuwalipa Chap Chap. TANZANIA Chachu Mno Kama Ndimu
Mm nadai pesa tangu 2016 mpaka leo sijalipwa
 
Back
Top Bottom