Waziri Ummy: Bima ya Afya (NHIF) inakaribia kufa

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,120
1662020908898.png

Wakati mikakati ya kuboresha huduma za afya ikiendelea kuwekwa, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amebainisha dalili za kufa kwa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kutokana na kulemewa na madeni ya matibabu ya wanachama wake.

Akifungua mkutano wa siku tano wa kikanda wa kuwajengea uwezo kuhusu ugonjwa wa kipindupindu jijini hapa jana, Waziri Ummy alitaja magonjwa yasiyoambukiza ndiyo sababu kuu ya gharama kubwa.

“Kuongeza uelewa ni jambo la msingi, kwa mfano bima yetu ya afya (NHIF) inakaribia kufa kwa kuwa umeelemewa na ongezeko la madai yanayohusu NCD (magonjwa yasiyoambukiza),” alionya Ummy.

Magonjwa yasiyoambukiza yanajumuisha moyo, saratani, mfumo wa upumuaji na kisukari yanayochangia asilimia 71 ya vifo vinavyotokea duniani ambapo ni sawa na watu milioni 41 kila mwaka.

Akisisitiza kuhusu uelewa wa dalili za magonjwa na jinsi ya kujikinga nayo, Waziri Ummy alisema “fanyeni kuwa jukumu la msingi ili kuzuia kuenea kwa maambukizi, najua tutafanikiwa kupambana na kipindupindu katika nchi zetu.”

Kutokana na hali hiyo, waziri huyo ameiagiza NHIF kuachana na utaratibu iliouanzisha hivi karibuni wa kudhibiti idadi ya wagonjwa wanaohudhuria vituo vya afya.

Taarifa ya NHIF

Akizungumza na waandishi wa habari Agosti 11 jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Bernard Konga alisema wametumia Sh99.09 bilioni mwaka 2021/22 kulipia magonjwa yasiyoambukiza.

Alisema kiasi hicho ni sawa na asilimia 18 ya fedha zote zilizolipwa huku dawa za saratani na huduma ya kusafishwa figo (dialysis) zikitumia fedha nyingi zaidi. Alisema magonjwa yasiyoambukiza ni mzigo mkubwa kwa mfuko huo.

“Dawa za saratani zinaila zaidi NHIF. Haya ni magonjwa yanayotokana na mtindo wa maisha, kuna huduma ya kusafishwa damu kwa wagonjwa wa figo, tunatumia Sh35.4 bilioni kwa mwaka,” alisema.

Konga, alisema mpaka sasa mfuko huo una wanachama 4,831,233 sawa na asilimia nane ya Watanzania wote huku asilimia sita wakihudumiwa na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) huduma nyingine za bima zikihudumia asilimia moja. Hata hivyo, alisema kuna udanganyifu mwingi unaofanywa na watoa huduma hali inayouumiza mfuko huo lakini wanapambana na hali hiyo.

“Udanganyifu upo na tumekuwa tukichukua hatua, tutasitisha mikataba itakayoonekana inahatarisha uendelevu wa mfuko. Tumekuwa tukichukua hatua ikiwamo kupiga faini, kuwaripoti wahusika katika mabaraza yao kuhakikisha tumelipia huduma halali kulingana na miongozo,” alisema Konga.

Taarifa ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ya mashirika ya umma ya Machi 2022, inaonyesha NHIF ilipata hasara ya Sh109.71 bilioni.

Pia Soma: Waziri Ummy: Magonjwa yasiyo ambukiza yanauelemea mfuko wa bima ya afya

Chanzo: Mwananchi
 
Waziri anakosea anapokiri bima ya afya NHIF inakaribia kufa, kwanini wasitafute njia mbadala itakayowawezesha kumudu hayo mazingira ya kuongezeka gharama za matibabu?

Kuna watu wanaweza kupoteza ajira zao hapo kutokana na kufa kwa hicho kitengo, wasiwe wepesi kukiri kushindwa bila kwanza kutafuta majibu ya changamoto zinazoukabili huo mfuko.

Mfano, kama inapoonekana gharama za matibabu anazopata mwanachama ni kubwa zaidi ya kile anachochangia mwanachama, kwanini NHIF wasigawane gharama za matibabu na mwanachama 50/50 ili kuepuka tatizo la mfuko kuzidiwa na gharama mwishowe kutengeneza madeni?

Hili nimeona linatokea kwa bima nyingine za afya, licha ya wanachama kulipiwa na mifuko hiyo, bado hutakiwa kutoa sehemu nyingine za gharama ya matibabu yao toka mifukoni mwao ili kufidia nyongeza ya kile wasichochangia kwenye bima zao za afya.

Kama hilo lisipowezekana, basi nashauri kiasi cha pesa anazochangia mwananchama ambaye ni mgonjwa wa hayo magonjwa makubwa yasiyoambukiza kiongezwe ili kuendana na gharama halisi za matibabu yao.
 
Hii ni moja ya mashirika yaliyoanzishwa bila upembuzi yakinifu.

Serikali ijifunze toka serikali ya Awamu ya Tatu chini ya Benjamin William Mkapa.

Mkapa alianzisha kwa weledi mkubwa TANROADS na TRA ya sasa.

Tunashindwa nini kujifunza na tuna ma PhD yanaozea vichwani mwa kina Mwigulu.
 
Watanzania tuwe waelewa hakuna tatizo lisilo na jibu..nature ya matatizo ya kufilisika be it kampuni, mtu binafsi, kikundi nk ni poor planning na uwezo mdogo kwenye usimamizi..! Ni mambo ya ajabu kabisa taasisi ya aina ya NHIF inaongozwa na watu wenye uwezo mdogo kiuongozi na usimamizi..

Huwezi kuwa kiongozi ikiwa umeshindwa kuona dalili za taasisi kulemewa mapema kabisa na ukashindwa kuchukua hatua kuokoa hali hiyo, lakini unasubiri kuja kulalamika hadharani kwamba taasisi imelemewa.. Ukifika hatua hiyo ni bora uondoke hapo sababu umekiri kushindwa tayari.. Bodi ya NHIF na Mkurugenzi wake hawastahili kubaki hapo tena.
 
Waziri anakosea anapokiri bima ya afya NHIF inakaribia kufa, kwanini wasitafute njia mbadala itakayowawezesha kumudu hayo mazingira ya kuongezeka gharama za matibabu?

Kuna watu wanaweza kupoteza ajira zao hapo kutokana na kufa kwa hicho kitengo, wasiwe wepesi kukiri kushindwa bila kwanza kutafuta majibu ya changamoto zinazoukabili huo mfuko.

Mfano, kama inapoonekana gharama za matibabu anazopata mwanachama ni kubwa zaidi ya kile anachochangia mwanachama, kwanini NHIF wasigawane gharama za matibabu na mwanachama 50/50 ili kuepuka tatizo la mfuko kuzidiwa na gharama mwishowe kutengeneza madeni?

Hili nimeona linatokea kwa bima nyingine za afya, licha ya wanachama kulipiwa na mifuko hiyo, bado hutakiwa kutoa sehemu nyingine za gharama ya matibabu yao toka mifukoni mwao ili kufidia nyongeza ya kile wasichochangia kwenye bima zao za afya.

Kama hilo lisipowezekana, basi nashauri kiasi cha pesa anazochangia mwananchama ambaye ni mgonjwa wa hayo magonjwa makubwa yasiyoambukiza kiongezwe ili kuendana na gharama halisi za matibabu yao.
Pesa ya kumudu na kuendesha kwa ubora ipo sema mipangilio ndo mibovu
 
Mfano, kama inapoonekana gharama za matibabu anazopata mwanachama ni kubwa zaidi ya kile anachochangia mwanachama, kwanini NHIF wasigawane gharama za matibabu na mwanachama 50/50 ili kuepuka tatizo la mfuko kuzidiwa na gharama mwishowe kutengeneza madeni?
Bima haina maana kwamba unapata sawa na kile unachochangia. Kama hujaugua kabisa hupati au huhudumiwi chochote. Lakini ukiugua utahudumiwa Kwa gharama hata mara kumi ya mchango wako. Hiyo ndiyo maana na faida ya bima. Hata kwenye mali unazowekea bima, eg. gari, unaweza lipia bima sh. 500,000=/, gari ikipata ajali unalipwa gharama ya matengenezo, labda milioni Tano au zaidi au gari nyingine, na pia kama Kuna majeruhi ktk ajali hiyo analipwa.
 
Back
Top Bottom