Waziri Sospeter Muhongo On People’s Power

Waziri Sospeter Muhongo On People’s Power

Kwa mtazamo wangu Prof Muhongo anateswa na peoples power lakini kwa kifupi sana ni kuwa 'Muslim' wana msemo wao Takbir kisha wanaitikia Allaaaaaah Akbar.

Msemo huo una sehemu zake za kuutumia.

Hivyo hivyo peoples power una sehemu zake na wala hauhitaji nyongeza.

Nitarudi baadae kujazia mada hii.
 
Hongera sana EMT, umeeleza vizuri sana kitu nilichokuwa nafikiria. Kama pia alivyosema BAK, Waziri Muhongo anatakiwa aongelee nishati na madini kwa taifa. kazi ya kuchambua CHADEMA na people's power awaachie akina Nape. nadhani ni mbinu ya kupambana na CHADEMA kwa kutumia mtu ambaye anaonekana analeta mabadiliko. kwa kuwa Muhongo ameonekana kuwa mchapa kazi, basi anaweza kutumika kama fimbo kwa CHADEMA. lakini pia anaonekana anajipigia debe sana si ajabu ana malengo ya kisiasa huko mbele. anataka aonekane kwamba amekuja na mbinu mbadala ya kupambana na CHADEMA bila kutumia mabomu wala maji ya kuwasha. nadhani approach yake ni very naive. ingekuwa kama ya Mwakyembe nadhani. Mwakyembe anaongea majukumu yake tu. na kwa kufanya hivyo anajijenga kisiasa pia tena kwa njia bora zaidi kuliko ya Muhongo.
 
Duh!Huyu Muhongo kumbe naye mwizi tu na mtapeli wa kisiasa?Mbona walimsifia sana humu kwamba eti si mwanasiasa?Karibia niingie mkenge ati! Kongosho i blame you kwani niliamini kwamba huyu si mtu wa "mambo jambo",kumbe naye mtapta tu!


Ooohh... No hell no....!!!

Political myopia is killing u ....
First... Prof. Muhongo hakupinga People's power....he said it must be broaden to large spectrum...!!! He went far explaining that broadness i.e must be PEOPLES' CENTERED......

PEOPLES' CENTERED NOT ONLY POLITICALLY like u cdm ur doing right now....!!!

SOCIALLY & ECONOMICALLY...!!!

So ur blaming, and attacking Prof. for ur political shortminded to cdm only....!!!

AFTER ALL.... ULITEGEMEA PROF. aisifie cdm....!!???

then u will be a kid, baby, child in politics....

Tena yupo fair sana, a hardworking, respectable & top cream kama hujui....hafanyi kazi kwa mazoe ya cdm or ccm... of course he must lean CCM... He is ccm...!!

So where are u at...!!?? Think aloud..!!
 
Last edited by a moderator:
Kama ilivyo kawaida yetu, tunajadili source (Mwana CCM) badala ya content (Broad Spectrum of Peoples' Power). Huu ni udhaifu mkubwa tulionao wana JF! Ni bahati mbaya sana kwamba humu jamvini kuna watu ambao kwao hata kama CCM ita-prove beyond reasonable doubt kwamba inaweza kuifikisha nchi yetu kwenye nchi ya Ahadi; kwao hawapo tayari kuipa CCM nafasi hiyo.

In contrast, wapo pia wana CCM ambao hata kama CHADEMA wata-prove beyond reasonable doubt kwamba wana uwezo wa kuifanya Tanzania kuwa Marekani; bado kwao hawapo tayari kuipa nafasi hiyo (CHADEMA)!!! Hakika,watu wa aina hiyo ni sumu kwa mustakabali wa nchi simply because kwao wao; Chama ndicho kitu cha kwanza na Tanzania baadae!

Nikirudi kwenye mada.....binafsi naamini changamoto iliyotolewa na Profesa Muhongo ni very constructive Challenge kwa CHADEMA. Waswahili wanatuambia kwamba, Baniani Mbaya, Kiatu chake dawa! Ni bahati mbaya sana kwamba CHADEMA wamejipanga vya kutosha kuhakikisha wanaiondoa CCM madarakani ingawaje sizani kama wamejipanga vya kutosha kuiongoza nchi hii kwa mafanikio.

Ubaya wa kutojipanga kiuongozi utasababisha CHADEMA kutumia staili ile ile ya African Politics pindi chama cha upinzani kinapopata ridhaa ya wananchi kushika dola. Staili hiyo ni ile ya Utawala Mpya kuanza kamatakamata ya viongozi waliopita kwa tuhuma mbali mbali; hususani UFISADI! At the end of story; wanajikuta dhamira ya kamatakamata imefikia tamati na kwavile wanakuwa hawakujipanga kiuongozi;

wanabaki wakiwa hawana jipya la kuushawishi umma uwape nafasi nyingine ya kubaki madarakani! Jambo kama hilo limepata kutokea Zambia.

Kwavile Fredrick Chiluba na chama chake hawakujiandaa kuongoza; walijikuta wakishindwa kuendelea kubaki madarakani baada ya staili yao ya "nitoke vipi" kuwa imeshachuja!

CHADEMA wakiacha kutumia changamoto zinazotolewa na wadau mbali mbali, basi ambayo yalipata kutokea Zambia hata hapa Tanzania yanaweza kutokea.

Mathalani, ikiwa CHADEMA itapata ridhaa ya wananchi hapo 2015, basi salama yao ni kuona CCM inasambaratika baada ya uchaguzi wa 2015 lakini endapo CCM watatasimama pamoja hata baada ya kushindwa hapo 2015; basi (CCM)watakuwa na uwezo mkubwa wa kurudi tena 2020.

Kwamba Peoples' Power iwe in Broad Spectrum ni jambo ambalo halipaswi kupuuzwa na CHADEMA hata kidogo.

Wanapaswa waonyeshe in advance kwamba, si tu wana uwezo wa kuindoa CCM madarakani, bali pia wana uwezo wa kuongoza kwa vitendo! Mathalani, sera ya CHADEMA inayowatofautisha na vyama vingine vya kisiasa ni ile sera yao ya Majimbo.

Hata hivyo, bado wameshindwa kuitekeleza sera hiyo kwa vitendo kwa kutumia mazingira waliyonayo hivi sasa. Mathalani, sioni ni kwanini hadi leo CHADEMA wameshindwa kabisa kuitekeleza sera yao ya majimbo kujiimarisha kisiasa maeneo mbali mbali ya nchi.

Sioni sababu ni kwanini hadi leo hawana ofisi za kanda za chama chao jambo ambalo bila shaka lingeimarisha sana chama hicho kwenye maeneo mbalimbali ya nchi.

Kwamba, kunakuwa na CHADEMA Kanda ya Kusini, Mashariki, Magharibi na zingine sawa na hizo huku watendaji wakuu wa Kanda hizo wakiwa ni wale wenye influence kubwa kwa jamii! Kuna watu kama akina Ben Saa Nane, John Heche, Mnyika, Zitto Kabwe na wengine kama hao ambao wangefaa kabisa kuwa watendaji wakuu wa CHADEMA kwenye Kanda mbali mbali nchini huku makazi yao yakiwa huko huko! Sia ajabu, hadi watakapopata ridhaa ya wananchi; wangekuwa tayari wameshafahamu mapungufu na uimara wa sera yao ya majimbo.
 
Kama ni mtu makini utagundua kwa urahisi tu Pro. muongo anapiga bla bla tu, na kuna kitu kiko nyuma yake ambacho kimejificho hivyi anaona kupitia people's power mapema atakuja kuumbuka, na sipendi mtindo wake wa kuongea ni kama anatafuta sana huruma kwa wana nchi. nilitegemea mtu kama yeye aongee fact zaidi. na pia People's power yeye hamuhusu wala hiyo si slogan ya kufanyi a maendeleo hiyo ni kuwa adabisha mafisadi...aache upuuzi afanye kazi mpaka leo hii umemem ni tatizo, ukiwa makini jama ana boa vibaya sana... hakuna kitu pale!
 
Hata yeye jana alitoa takwimu tata, almost took him for mulugo, momentarily though. Eti 'makusanyo toka migodini yameongezeka kutoka trilioni 75 (2010) hadi trilioni 180 (2011).

How can that be? Si tungefunga biashara zote tuhamie huko.Kisha akatueleza kuwa juhudi zake kuboresha mapato ya serikali yatokanayo na madini yamezaa matunda kwani sasa mrabaha umeongezeka kutoka 3% hadi 4%.

A mere increment of 1%? And you dare go public and brag about it? Is that some kinda silly prank prof, or were you simply tryna pull the string and see how mad people can really be? Cut the **** old man and get us some real money from our heritage, or else you will go down the annals of history no different than your predecessors!
 
JokaKuu,
Binafsi siamini kabisa kwamba tatizo la Tanzania ni kiongozi kuwa mwanasiasa! Hakuna popote panapothibitisha kwamba, as far as you're a plitician, basi wewe utakuwa fisadi, mla rushwa, mtu usyewajibika na mambo mengine mabovu sawa na hayo!

Tatizo kuu la nchi hii ni ukosefu mkubwa wa maadili uliotapakaa miongoni mwa Watanzania bila kujali kama MTanzania huyo ni mwanasiasa, kiongozi wa dini au mwanataaluma! Hawa wote, kwa wingi wao wana upungufu mkubwa wa maadaili! NI nani atakayebisha kwamba wanataaluma nao ni mafisadi? Ni nani atakayebisha kwamba viongozi wa dini nao ni mafisadi? Ni nani atakayebisha kwamba watu wa sanaa nao ni mafisadi? Hivyo basi, hata yale madai kwamba Mawaziri wasitokane na wabunge katu haliwezi kuwa suluhisho la matatizo yetu! Juzi juzi hapa jizi na fisadi moja toka TANESCO liitwalo Mhando limeachishwa kazi!! Ni mwanasiasa huyu?!

Wabunge wamekuwa wakilalamika kwamba baadhi ya Mawaziri wamekuwa wakiyapendelea majimbo yao! Je, unataka kuniambia endapo Mawaziri hawatatokana na wabunge; hao wapya nao hawatapendelea maeneo wanayotoka? Kwani kuna gharama gani kwa mtu kama Muhongo leo hii kuamua kupendelea anakotoka?! Leo hii JK anipe uwaziri wa fedha, unataka kuniambia nitashindwa kuipendelea Mchinga kwavile tu mimi sio mbunge?!

Hivyo basi, kinachotakiwa hapa ni mwarobaini wa kweli utakao-shape maadili ya Watanzania....kama ambavyo nimepata kuandika mara kwa mara hapo nyuma; mwarobaini huo katu hauwezi kuwa Utawala Bora Wa Kimagharibi kwani nao unatumika kama kichaka cha wahalifu!!! Mwarobaini wa kweli ni Katiba Ya Kidikteta (Approved Dictatorship Constitution) itkayoondoa Western Good Governance na kuinguiza Approved Dictatorship Governance na hiyo ndiyo itakuwa good governance from our political perspective.

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
Great thinkers. I really like you guys for your good positive postings and comments. For those concerned I advice them to pick all the relevant points and try their level best to improve the life of Tanzanians. In the ruling party some individuals are struggling to show that it can be done! However a majority ni ulaji tu. The current system is very hard to change that's why wananchi have come up with the peoples power. Furthermore we need some critical practicable plans of how this power is gonna liberate the walalahoi. CDM come up with that practicable plan of which I am sure CCM cannot copy it!
 
Falsafa ya Nguvu ya Umma au Peoples Power, inalenga kuwaweka wananchi au watu kuwa centre ya maamuzi na maendeleo ya nchi, hii na pamoja na kutimiza ibara ya 8 ya katiba inayosema wananchi ndo msingi wa mamlaka yote na serikali itabapa madaraka yake toka kwa wananchi, kudown play role ya nguvu ya umma ni siasa tu lakini ukweli unabakia pale pale! Lakini pia ni vema Waziri angejikita kuchambua itikadi ya chama chake ya ujamaa na kujitegemea, kuliko kuanza kuizungumzia CHADEMA!
 
Ulimsikiliza jana??

Alieleza mengi mazuri, ila komenti ya peoples power inavuruga hata mie sikumwelewa.

Duh!Huyu Muhongo kumbe naye mwizi tu na mtapeli wa kisiasa?Mbona walimsifia sana humu kwamba eti si mwanasiasa?Karibia niingie mkenge ati! Kongosho i blame you kwani niliamini kwamba huyu si mtu wa "mambo jambo",kumbe naye mtapta tu!
 
Asitujaze upuuzi wake. Kama yeye ni Prof kweeeli alitakwa atambue kuwa BILA "POWER" hayo yote hayawezekani. First u must have power to control or manage your enviroment. Hayo yote anayosepa ni PRODUCTS zinzoweza kupatikana kama watu wana mamlaka juu ya nchi yao!
 
I watched that interview..and I was disappointed by the way Prof Muhongo become the likes of Nape-Wassira-Mwigulu type of CHADEMA haters! Aliishambulia slogan ya 'people's power' bila kuelewa au kuchambua filosofia yake...thats too low for a Professor!
 
Ulimsikiliza jana??

Alieleza mengi mazuri, ila komenti ya peoples power inavuruga hata mie sikumwelewa.

Akiwa kama mwalimu inawezekana alikuwa anawafundisha watu juu ya nguvu ya umma kama walimu wengine wanavyofanya mashuleni na vyuoni.

CHADEMA wanasema:

".....CHADEMA inaamini katika falsafa na itikadi ya nguvu na mamlaka ya umma. Sasa tumeamua kuweka bayana falsafa yetu na itikadi yetu. CHADEMA tunaendelea kuwa na falsafa ya nguvu na mamlaka ya umma. Huu ni msimamo wetu wa asili: Kwamba falsafa ya CHADEMA ni kuamini katika "Nguvu na Mamlaka ya Umma" (People's Power) katika kumiliki, kuendesha, kubuni na kuendeleza mawazo, raslimali, uchumi na siasa za nchi.

Aidha, falsafa ya nguvu na mamlaka ya umma ndiyo msingi na chimbuko la kuundwa kwa dola ya nchi na kuwa umma ndio wenye madaraka ya mwanzo na mwisho katika kuamua hatma ya nchi na taifa pasipo kuingiliwa, kudanganywa, kutakrimiwa au kughilibiwa na viongozi, watawala au wageni....

...hivyo basi, falsafa ya "nguvu na mamlaka ya Umma" ndiyo njia ya msingi ya kubadilisha fikra na uongozi unaokandamiza umma, ili kuibua fikra mpya na kuweka uongozi unaoweza kumilikiwa, kuhojiwa, na kuwajibishwa na umma kwa kutumia vyombo vinavyopatikana kwa utashi wa wengi kupitia chaguzi huru na haki. Hii ni falsafa tuliyokuwa nayo ambayo tunaiendeleza." Chanzo: Marekebisho ya Katiba ya CHADEMA

Mafundisho ya CHADEMA kuhusiana na tasinifu ya nguvu ya umma hayana tofauti yoyote na mafundisho yanayotolewa na walimu wa sekondari na wakufunzi wa vyuo wanapokuwa wanafundisha madarasani. Kwa mfano, tasinifu ya nguvu ya umma imo katika kitabu kiitwacho "Mwongozo wa Somo la Uraia Kwa Ajili ya Walimu wa Sekondari na Wakufunzi wa Vyuo" (2002) kilichoandikwa na Dk. Naomi B. Katunzi.

Katika kitabu hiki, tasinifu ya nguvu ya umma imejadiliwa katika somo la 11 na 12 kuanzia ukurasa wa 45 hadi 51. Kwa namna fulani basi, Taasisi ya Elimu Tanzania, Walimu wa Sekondari na Wakufunzi wa Vyuo wanaofundisha somo la uraia, wanafanya kazi ya kueneza itikadi ya CHADEMA? Kama ni hivyo, inawezekana hii ndiyo sababu iliyoifanya CHADEMA kupata mteremko katika siasa zake za hivi karibuni hasa kwa vijana? Siyo kwamba Muhongo, kama mwalimu, alikuwa anazawazisha mambo tuu hapo juu ya people's power kama wanavyofanya walimu wengine?
 
Muhongo asitake kuchepusha treni kwa falsafa uchwara. CHADEMA wako sahihi kabisa kupigia chapuo peoples' power wakati huu ambapo unatakiwa uongozi unaofuata utashi wa umma - sio huu uliopo unaojitumikia na kuwatumikisha wananchi kujineemesha. Kwanza, hakuna kitu kama people's performance.

Wananchi siku zote wanachakarika kujitafutia maisha. Ufanisi wao unaathiriwa kwa uzuri au ubaya na ubora/udhaifu wa mifumo ya utendaji inayosimamiwa na serikali.

Ni serikali ndiyo inatakiwa iwe na performance ikisimamiwa na umma wenye power. Wananchi wakirejeshewa nguvu yao kama wanavyopigania CHADEMA ndipo peoples' progress na peoples prosperity vitakapowezekana; kinyume cha hapo ni ndoto za saa sita mchana.
 
Hujaiweka alivyosema yeye kasema people's power inachochea vurugu .......kasema juzi alikubaliana na ndugu zake watanzania wa Moshi kuhusu people's power vs aliyosema, hajui kuwa bila people's power leo asingekuwa waziri na badala yake angeendelea kugombania kiwanja kati ya yeye kama kiongozi wa kanisa la Mennonite na Nimrod Mkono , .......kule musoma ....

People's power itamtaka siku moja aeleze alipokuwa chief geologist wa nchi hii ramani alizompa Jimmy Sinclair zilikuwa na faida gani kwa taifa....

Anajua kuna siku people's power itamtaka aeleze faida tunayopata kutokana na sera ya gesi na mafuta ambayo imekopwa na imeandaliwa na wataalam (consultants ) wa makampuni ya uchimbaji na utafutaji wa mafuta na gesi kutoka Uk, usa nk.......atapaswa kuwa na majibu......

Kuna siku people's power itamtaka majibu i kwanini IPTL inauzwa bei poa kwa kampuni moja la mafuta .....ili liendelee kuuzia Tanesco umeme wakati pendekezo la awali lilikuwa mitambo hiyo inunuliwe na serikali ili kupunguza gharama za umeme .......

Ndio maana anataka people's power iepukwe......

I can't add anthing more to what you have said mkuu na people's power ndo inaleta hayo mengine yote
 
Hiyo ni slogam tu na kuweka kuona watu na umma wa Tanzania unaelewa vizuri sana juu ya CHADEMa wanasema nini ila cha msingi ni chama kushuka kwenye glassroot toka chini na sio kuwa na base juu tu hivyo kuna umuhimu sana kuona jinsi gani ya kuimarisha chama kwa kipindi hiki kilichobaki na kuweka mikakati toka chini kabisa na kuweka centered hiyo ya watu
 
Back
Top Bottom