Anheuser
JF-Expert Member
- Mar 23, 2011
- 1,944
- 665
Itatusaidia sana tukijenga utamaduni wa kuchunguza systemic flaws za mfumo mzima wa uendeshaji mambo badala ya kuangalia symptoms za tatizo tu....Sitta ana kashfa ya kutumia mabilioni ya fedha kujenga ofisi ya spika jimboni kwake Urambo kana kwamba alitarajia atakuwa spika wa maisha, na mrithi wake atatoka Urambo.
Sitta hana password ya safe box la Hazina, kuna mtu alimpa hizo hela, nani huyo, kwa nini hakuuliza kama makao makuu ya kudumu ya Spika yanahamia Urambo, kiasi gani alimpa, kwa nini, kabla ya kutoka zilikuwa earmarked kwa bajeti gani, Sitta alisema anaenda kufanyia nini, sheria inasemaje, makaratasi yako wapi, mfumo mzima ukoje? Ultimately, si kosa la Sitta kuomba hela na kupewa.