Kenyan
JF-Expert Member
- Jun 7, 2012
- 414
- 313
Maandamano ya Jumatano yalishuhudia uharibifu mkubwa zaidi ikilinganishwa na ya hapo nyuma huku waandamanaji wakiharibu barabara maarufu ya Expressway, ambayo ilikuwa ndio mradi mkubwa zaidi na wa mwisho aliofanikisha Rais mstaafu Uhuru Kenyatta.
Barabara hio ambayo watumiaji wake hulazimika kulipa ada Ili kutumia inaunganisha Uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta na eneo la Westlands.
Uharibifu wa leo umepelekea serikali kusitisha matumizi yake huku Waziri wa Uchukuzi Kipchumba Murkomen akiapa kuwadhiibu wahusika.
Kwenye taarifa iliyotumwa kwenye vyombo vya habari, Murkomen ametoa rai kwa IGP Japheth Koome, kuanzisha uchunguzi mara moja kwa kutumia kamera za CCTV zilizoko barabarani humo, kuwakamata waharibifu. Aidha Murkomen ametoa onyo kwa Viongozi wa Upinzani wakiongozwa na Raila Odinga kuwa iwapo uharibifu wa barabara utaendelea basi watachukuliwa hatua kisheria na kushurutishwa kugharamia uharibifu.
Maandamano ya leo yamepelekea vifo vya watu 7 huku wengine wakiuguza majeraha ya risasi katika hospitali mbalimbali.
Barabara hio ambayo watumiaji wake hulazimika kulipa ada Ili kutumia inaunganisha Uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta na eneo la Westlands.
Uharibifu wa leo umepelekea serikali kusitisha matumizi yake huku Waziri wa Uchukuzi Kipchumba Murkomen akiapa kuwadhiibu wahusika.
Kwenye taarifa iliyotumwa kwenye vyombo vya habari, Murkomen ametoa rai kwa IGP Japheth Koome, kuanzisha uchunguzi mara moja kwa kutumia kamera za CCTV zilizoko barabarani humo, kuwakamata waharibifu. Aidha Murkomen ametoa onyo kwa Viongozi wa Upinzani wakiongozwa na Raila Odinga kuwa iwapo uharibifu wa barabara utaendelea basi watachukuliwa hatua kisheria na kushurutishwa kugharamia uharibifu.
Maandamano ya leo yamepelekea vifo vya watu 7 huku wengine wakiuguza majeraha ya risasi katika hospitali mbalimbali.