Waziri Mkuu wa Ivory Coast, Hamed Bakayoko afariki hospitalini Ujerumani

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,011
9,879
1615443317459.png

Hamed Bakayoko enzi za uhai wake

Waziri Mkuu wa Ivory Coast, Hamed Bakayoko, amefariki dunia katika hospitali moja nchini Ujerumani, mamlaka imesema.

Bakayoko, aliyekuwa akipata matibabu ya saratani, alifariki dunia Jumatano siku chache tu baada ya kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa ya 56.

Aliteuliwa kama waziri mkuu mnamo mwezi July kufuatua kifo cha mtangulizi wake Amadou Gon Coulibaly.

Rais Alassane Ouattara amemuelezea Bwana Bakayoko kama kiongozi bora, mfano wa kuigwa kwa vijana na mwenye uaminifu usio kifani".

Bwana Bakayoko alipelekwa nchini Ufaransa mnamo mwezi Februari kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu na baadaye akahamishwa hadi nchini Ujerumani kwasababu afya yake ilikuwa inaendelea kuzorota.

Waziri mkuu huyo ambaye alikuwa mkurugenzi mtendaji wa vyombo vya habari alitekeleza jukumu kubwa katika maridhiano nchini Ivory Coast wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe kipindi cha mwongo wa kwanza wa karne.

"Alikuwa mshikadau mkuu katika siasa na maridhiano," amesema msemaji wa upinzani wa chama cha Ivorian Popular Front Issiaka Sangare, katika shirika la habari la AFP.

Mbali na jukumu lake kama waziri mkuu, Bwana Bakayoko pia alikuwa waziri wa ulinzi nchini humo.

Patrick Achi ameteuliwa kama waziri mkuu wa muda huku Tene Birahima Ouattara, huku kaka mdogo wa rais akitajwa kama waziri wa ulinzi wa muda.

Chanzo:
BBC
 
Kwa wale wapenzi wa CONGO DRC Rhumba,Soukous,Dance, sebene lingala nk watakuwa wamemsikia sana huyu jamaa akitajwa hasa kwenye ngwasuma.

BAKAYOKO ALIKUWA NANI HASA!

Hamed Bakayoko (8 Machi 1965 - 10 Machi 2021) alikuwa mwanasiasa wa Ivory Coast ambaye aliwahi kuwa Waziri Mkuu wa Cote d'Ivoire kutoka 8 Julai 2020 hadi kifo chake mnamo 10 Machi 2021. Hapo awali alikuwa amewahi kuwa Waziri wa Teknolojia Mpya, Habari wa nchi hiyo. na Mawasiliano, Waziri wa Mambo ya Ndani na Waziri wa Ulinzi.

NINI KIMEONDOA UHAI WAKE
Bakayoko alitangazwa mnamo 6 Aprili 2020 kwamba alikuwa na maambukizi ya COVID-19, alipona awali kisha baadaye alipata maambukizo ya pili ya coronavirus na malaria kali. Alipata matibabu ya muda mrefu huko Ufaransa mara mbili mwanzoni mwa 2021. Mnamo Machi 6, 2021, alihamishiwa Kituo cha Matibabu cha Chuo Kikuu cha Freiburg kwa matibabu zaidi. Bakayoko alikufa mnamo 10 Machi 2021, akiwa na umri wa miaka 56.

UMAARUFU WAKE
Bendi za muziki za Congo nyingi zikienda Ivory Coast zilipenda kwenda mji wa Abidjan na kwa kuwa wakati fulani jamaa alikuwa Meya wa mji huo alikuwa akipenda muziki wa Congo na kuwatuza vilivyo...hivyo majamaa kumuimba sana.

WIKIPEDIA
 
Papaa musofe, Kama ndama mutoto ya ng'ombe, Papa amosi makala
 
BBC News
menu

Hamed Bakayoko: Ivory Coast's PM dies in Germany​

  • Hamed Bakayoko
Image captionHamed Bakayoko was appointed prime minister in July, following the sudden death of his predecessor
The Prime Minister of Ivory Coast, Hamed Bakayoko, has died in a hospital in Germany, authorities say.

Bakayoko, who was receiving treatment for cancer, passed away on Wednesday, just days after his 56th birthday. He was appointed prime minister in July, following the sudden death of his predecessor Amadou Gon Coulibaly. President Alassane Ouattara described Mr Bakayoko as a "great statesman, an example to young people and a man of exemplary loyalty". Mr Bakayoko was flown to France in February for medical tests and was later transferred to Germany due to his deteriorating health.

A former media executive who turned to politics, he played a prominent mediation role in Ivory Coast's civil war during the first decade of the century.

"He was a key player in the political game and a major player in reconciliation. It's a true shame," Issiaka Sangare, spokesman for the opposition Ivorian Popular Front told AFP news agency.

Aside from his role as prime minister, Mr Bakayoko was also the country's defence minister. Patrick Achi has been appointed as interim prime minister, while Tene Birahima Ouattara, a younger brother of the president, has been named interim defence minister
 
Back
Top Bottom