boyfriendy
JF-Expert Member
- Sep 9, 2012
- 1,988
- 1,034
Teh teh teh! Dah jf kwa kweli kiboko yaani nimecheka sana leo yaani aya mambo bana
Mara baada ya mkutano mkuu wa ccm uliofanyika dodoma, waziri mkuu hayupo ofisini, kuna tetesi toka kwa watendaji wa ofisi ya waziri mkuu wakidai kuwa mh. Pinda amesusa ofisi kutokana na kukatwa jina lake katika harakati za kugombea kuteuliwa kuwa mgombea wa ccm.
Pia ccm wasiangalie kususa kwa dr slaa hata kwao kuna wengi sana wamesusa.
Baada ya kukatwa na "Kitengo" kuashiria kuwa hana maadili unadhani atakuwa na moral authority ya kiutendaji tena kweli! Yaani kwa maadili kapitwa na naibu waziri Makamba halafu atamwongozaje? Mungu atuepushe lisitokee la kutokea linalohitaji maamuzi mazito ya pamoja kwani kwa sasa ombwe ni kubwa kuliko wakati wowote!
Eti kwenye kumseti JK alimuambia .." Tumeamua kikata wote wenye miaka 60 kuja juuu...bora wangetangaza Mapema wasichukue fomu"
Umri haumaanishi afya bora kwakuwa hata Huyu Magufuli ni compromise ndio lakini hakupita security vetting ya Ngazi ya Urais ...waliomfuatilia HAWAKUWEZA KUPATA TAARIFA ZA UHAKIKA ZA ASILI YA BABA YAKE ....zaidi mamma yake ndie ambaye kizazi chake hadi cha pili kiliweza kuwa traced ...kwa kuwa Sasa kapata ..ndio usalama wako busy kufuatilia lineage ya baba yake Magufuli ...
Kuhusu afya ...aliwahi KUPATA mshtuko wa moyo akatibiwa ujerumani kwa kuwekewa ..kifaa Maalum cha kusupport mapigo ya moyo ..wakati huko ilisadikika Kapewa hujuma ...hivyo ni Kati ya Vitu vilimfanya asipende Siasa ZA Ndani ya Chama