benzemah
JF-Expert Member
- Nov 19, 2014
- 1,504
- 3,034
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na viongozi na waumini waliohudhuria mashindano ya kitaifa ya kuhifadhi Quran tukufu yaliyoandaliwa na taasisi ya Aisha Sururu Foundation (ASF) jijini Dar es Salaam amesema Rais Samia Suluhu Hassan anaguswa na suala la maadili hasa kwa vijana.
"Tunapowahifadhisha Quran vijana wetu, tuhakikishe jambo hilo jema linakwenda sambamba na ujenzi wa misingi imara ya malezi itakayowafanya wawe raia wema, waadilifu na wazalendo kwa nchi yao. Tukiwa wazazi, walezi na walimu wa Quran, nitoe rai kwam-ba tunapotoka hapa hebu tujiulize ni kwa kiasi gani tunaizingatia hi Quran tukufu katika mwenendo mzima wa maisha yetu ya kila siku," amesema na kuongeza;
"Pia tutamsaidia Mheshimiwa Rais kupata wasaidizi wacha Mungu na waadilifu katika kutekeleza majukumu yao ya kuwahudumia wananchi. Majaliwa alihimiza viongozi wa dini kila wanapopata nafasi kwenye mimbari wakemee ukatili wa kijinsia na wale wanaoenda kinyume na maadili na desturi za Kitanzania.
"Nitoe rai kwa viongozi wetu wa dini muendelee kutoa elimu kwa umma kuhusu umuhimu wa kulinda mila, desturi na tamaduni za Kitanzania hususan katika kipindi hiki tunachokabiliwa na wimbi kubwa la mmomonyoko wa maadili," alisema.
Majaliwa alisema Tanzania inakabiliwa na tatizo la mmomonyoko wa maadili na pia kumeibuka wimbi la vitendo vingine ambavyo vinakwenda kinyume na dini, mila, desturi na tamaduni za kitanzania.
"Tunapowahifadhisha Quran vijana wetu, tuhakikishe jambo hilo jema linakwenda sambamba na ujenzi wa misingi imara ya malezi itakayowafanya wawe raia wema, waadilifu na wazalendo kwa nchi yao. Tukiwa wazazi, walezi na walimu wa Quran, nitoe rai kwam-ba tunapotoka hapa hebu tujiulize ni kwa kiasi gani tunaizingatia hi Quran tukufu katika mwenendo mzima wa maisha yetu ya kila siku," amesema na kuongeza;
"Pia tutamsaidia Mheshimiwa Rais kupata wasaidizi wacha Mungu na waadilifu katika kutekeleza majukumu yao ya kuwahudumia wananchi. Majaliwa alihimiza viongozi wa dini kila wanapopata nafasi kwenye mimbari wakemee ukatili wa kijinsia na wale wanaoenda kinyume na maadili na desturi za Kitanzania.
"Nitoe rai kwa viongozi wetu wa dini muendelee kutoa elimu kwa umma kuhusu umuhimu wa kulinda mila, desturi na tamaduni za Kitanzania hususan katika kipindi hiki tunachokabiliwa na wimbi kubwa la mmomonyoko wa maadili," alisema.
Majaliwa alisema Tanzania inakabiliwa na tatizo la mmomonyoko wa maadili na pia kumeibuka wimbi la vitendo vingine ambavyo vinakwenda kinyume na dini, mila, desturi na tamaduni za kitanzania.