Waziri Mkuu Majaliwa: Tumsaidie Rais Samia kupata wasaidizi waadilifu

benzemah

JF-Expert Member
Nov 19, 2014
1,504
3,034
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na viongozi na waumini waliohudhuria mashindano ya kitaifa ya kuhifadhi Quran tukufu yaliyoandaliwa na taasisi ya Aisha Sururu Foundation (ASF) jijini Dar es Salaam amesema Rais Samia Suluhu Hassan anaguswa na suala la maadili hasa kwa vijana.

"Tunapowahifadhisha Quran vijana wetu, tuhakikishe jambo hilo jema linakwenda sambamba na ujenzi wa misingi imara ya malezi itakayowafanya wawe raia wema, waadilifu na wazalendo kwa nchi yao. Tukiwa wazazi, walezi na walimu wa Quran, nitoe rai kwam-ba tunapotoka hapa hebu tujiulize ni kwa kiasi gani tunaizingatia hi Quran tukufu katika mwenendo mzima wa maisha yetu ya kila siku," amesema na kuongeza;

"Pia tutamsaidia Mheshimiwa Rais kupata wasaidizi wacha Mungu na waadilifu katika kutekeleza majukumu yao ya kuwahudumia wananchi. Majaliwa alihimiza viongozi wa dini kila wanapopata nafasi kwenye mimbari wakemee ukatili wa kijinsia na wale wanaoenda kinyume na maadili na desturi za Kitanzania.

"Nitoe rai kwa viongozi wetu wa dini muendelee kutoa elimu kwa umma kuhusu umuhimu wa kulinda mila, desturi na tamaduni za Kitanzania hususan katika kipindi hiki tunachokabiliwa na wimbi kubwa la mmomonyoko wa maadili," alisema.

Majaliwa alisema Tanzania inakabiliwa na tatizo la mmomonyoko wa maadili na pia kumeibuka wimbi la vitendo vingine ambavyo vinakwenda kinyume na dini, mila, desturi na tamaduni za kitanzania.

WhatsApp Image 2023-04-02 at 19.40.13.jpeg
 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na viongozi na waumini waliohudhuria mashindano ya kitaifa ya kuhifadhi Quran tukufu yaliyoandaliwa na taasisi ya Aisha Sururu Foundation (ASF) jijini Dar es Salaam amesema Rais Samia Suluhu Hassan anaguswa na suala la maadili hasa kwa vijana.

"Tunapowahifadhisha Quran vijana wetu, tuhakikishe jambo hilo jema linakwenda sambamba na ujenzi wa misingi imara
Viongozi waadilifu anatafuta au anatafutiwa yeye si ndo anayewachagua au anakuwa amejitoa ufaham wakati anateua watu kama akina Makamba na nape
 
Hii kauli imejaa unafiki na udini wakati Siku hz Viongozi wengi ni wa mchongo.
 
Kwa bahati mbaya nchi haina viongozi waadilifu, na pm analijua hilo
 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na viongozi na waumini waliohudhuria mashindano ya kitaifa ya kuhifadhi Quran tukufu yaliyoandaliwa na taasisi ya Aisha Sururu Foundation (ASF) jijini Dar es Salaam amesema Rais Samia Suluhu Hassan anaguswa na suala la maadili hasa kwa vijana.


Wenda kauli yake inamaana ila sasa unawatoa wapi kupitia chama chake ? Ile chama imejaa vile wachumia tumbo tu
 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na viongozi na waumini waliohudhuria mashindano ya kitaifa ya kuhifadhi Quran tukufu yaliyoandaliwa na taasisi ya Aisha Sururu Foundation (ASF) jijini Dar es Salaam amesema Rais Samia Suluhu Hassan anaguswa na suala la maadili hasa kwa vijana.
Waadilifu tupo ila tukienda interview mnatukata mnachukua mnaowajua

Dah ujobless ni shida
 
Wenda kauli yake inamaana ila sasa unawatoa wapi kupitia chama chake ? Ile chama imejaa vile wachumia tumbo tu

Si wapo tayari, kama yule mama wa songea hakuna kitu kila siku anabadilishwa wizara, hivi tunaomba Mungu atusaidiaje pale. Mtu anafahamika ni incompetent yet anapewa wizara tena nyeti kama utumishi.
 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na viongozi na waumini waliohudhuria mashindano ya kitaifa ya kuhifadhi Quran tukufu yaliyoandaliwa na taasisi ya Aisha Sururu Foundation (ASF) jijini Dar es Salaam amesema Rais Samia Suluhu
Kwani hapo kuna UVCCM? Kama wapo Majaliwa unapoteza Muda
 
Si wapo tayari, kama yule mama wa songea hakuna kitu kila siku anabadilishwa wizara, hivi tunaomba Mungu atusaidiaje pale. Mtu anafahamika ni incompetent yet anapewa wizara tena nyeti kama utumishi.
Mhagama kichwani ni MWEUPEEEE
 
Si wapo tayari, kama yule mama wa songea hakuna kitu kila siku anabadilishwa wizara, hivi tunaomba Mungu atusaidiaje pale. Mtu anafahamika ni incompetent yet anapewa wizara tena nyeti kama utumishi.
Labda anayechachagua huwa anajitoa ufahamu .kama swala la kawaida tu raisi kushimdwa kuchagua watu wenye weledi hayo mengine atayaweza ? Makamba , nape na mhagame wameshaawahi kufanya lolote la maana mpaka waweko hapo
 
Huu ni ujinga na kuwafanya watanzania wote kuwa wajinga.

Tunamsaidiaje Rais kupata watu waadilifu, ilihali kuna kikundi cha watu wachache wanaohusika kufanya vetting?.
Na hawa wenyewe sio waadilifu ndio maana hawawezi kuteua watu waadilifu.
Rais aunde kamati mpya ya vetting, yenye waadilifu.
 
Unaweza vipi kumsaidia mtu kutafuta wasaidizi watakaomfaa ili kutimiza majukumu yake?

Unamaanisha kichwani kwake hamna kitu, hayajui majukumu yaje, hivyo hawajui hata wale wanaofaa kumsaidia?

Unazidi kuthibitisha vile tulivyo na kiongozi asiyejielewa..
 
Back
Top Bottom