Waziri Mkuu ateta na Rais wa benki ya AfDB

Waziri Mkuu ateta na Rais wa benki ya AfDB

Zack Abdul

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2026
Posts
474
Reaction score
472
WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amefanya mazungumzo na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Dkt. Sidi Ould Tah kando ya Mkutano wa 61 wa Mwaka wa Bodi ya Magavana wa Benki ya Maendeleo ya Afrika unaofanyika leo Jumanne Mei 26, 2026 katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Kintele (Kintele Congress Centre) jijini Brazzaville, Jamhuri ya Kongo.

Mazungumzo hayo yalijikita katika masuala mbalimbali ya maendeleo pamoja na ushirikiano wa kiuchumi kati ya Tanzania na taasisi hiyo.

Dkt. Mwigulu anamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mkutano huo unaowakutanisha viongozi mbalimbali wa Afrika pamoja na wadau wa maendeleo kujadili masuala ya uchumi, uwekezaji na maendeleo ya bara la Afrika.
IMG-20260526-WA0098.jpg
IMG-20260526-WA0099.jpg
IMG-20260526-WA0100.jpg
IMG-20260526-WA0101.jpg
IMG-20260526-WA0103.jpg
IMG-20260526-WA0102.jpg
IMG-20260526-WA0104.jpg
 
Back
Top Bottom