Waziri Makamba aivunja bodi ya Baraza la Taifa la Mazingira(NEMC)

Wakazi wa vingunguti wamelalamika weeeeee kuhusu uchavuzi wa mazingira, leo ndo waziri anaamka?
 
Bodi iliyovunjwa ndio hii ya apa chini?, naona lugha zina nichanganya
IMG_20170105_125002.jpg
 
Akizungumza na Clouds FM hivi punde, waziri wa mazingira na Muungano ktk ofisi ya Makamu wa Rais, January Makamba amesema ameivunja bodi ya usimamizi ya mazingira NEMC kwa kuwa imekithiri kwa Rushwa
 
Waziri Makamba ameivunja Bodi ya Baraza la Taifa la Mazingira (NEMC) kwa tuhuma za rushwa, ucheleweshwaji kibali cha ukaguzi na lugha mbovu.

'Sababu za mabadiliko ya Bodi ya NEMC ni ucheleweshwaji wa vibali vya ukaguzi wa mazingira na tuhuma za rushwa kwenye usimamizi.

Watendaji wa NEMC wamesaidia watu wenye maslahi nao na tuliwataka watueleze jinsi wanavyofanya kazi lakini hawajafanya hivyo.

Sasa kutokana na mapungufu makubwa ndani ya NEMC, tumeamua kuivunja bodi hii kuanzia leo na viongozi wengine tutawatangaza leo

Wapo pia baadhi ya watendaji wa NEMC tuliowasimamisha kazi ili ufanywe uchunguzi wa tuhuma zinazowakabili kabla kuchukua hatua

Na kuanzia sasa muwekezaji akikamilisha kutoa taarifa ya ujenzi wa kiwanda, ruhusa ya ujenzi itatoka ndani ya siku tatu

Tathmini ya mazingira itafanyika wakati ujenzi wa kiwanda husika unaendelea bila kusubiri cheti cha uthibitisho cha mazingira

Wawekezaji wanaokwenda NEMC wanatakiwa kuanzia kwa washauri elekezi ili kuondoa uhusiano wao na watu wa Baraza la NEMC'

Tutapima maeneo yote yanayofaa ili muwekezaji akipatikana asipate shida ya kutafuta eneo lake, yeye ataona maeneo yakiwa tayari'

'Wote tuliowachukulia hatua leo uchunguzi wa awali ulitosheleza kuwachukulia hatua stahiki, hatua nyingine zitafuata baadaye'

Tutatoa gharama elekezi kwa washauri elekezi wote ili wawekezaji wasilipie gharama kubwa kufanya uwekezaji popote nchini'

Kuna gharama tutazipunguza au kuziondoa kabisa kwenye mchakato wa uwekezaji, tunashindana na nchi nyengine kuvutia wawekezaji.

Kwa hisani ya Millard Ayo.
Jambo jema sana lililochelew*
Ubinafzi umethidi NEMC. Kazi zinaenda kwa viongosi na vikampuns vyao badala ya wataalamu waliondikishwa na wanaolipa ada kubwa @ mwaka (aibu) sababu uthibiti dun.

Nini hii : Kiwanda cha Nyama ya Punda Dodoma kinachofuta nguvu kazi ya punda
Kuzalisha nishati ya umeme kwa misitu kisiwa cha Mafya. etc..
 
Ni Kweli wanachelewesha sana kibali mpaka utoe rushwa ndiyo upewe kibali na siku zote hawakutembelei kutoa ushauri wa mambo mbalimbali ya kitaalamu wanasubiri ukosee ndiyo wanakuja kuomba rushwa na kukupiga kafaini kakishikaji ili waonekane wanafanya kazi na wanaandamana na waandishi wa habari ili kupata sifa

Guys, try to think big please. Sababu za kuvunja hii Bodi ya NEMC si issue ya Uwekezaji baali ni baada ya Mahakama wilaya ya Hai kumtia hatiani DC kwa kuharibu shamba la Mhe. Mbowe kwa kisingizio cha kuharibu Mazingira huku NEMC wakimkana DC kuwa hawakumtuma!! Kwanini Bodi ivunjwe sasa baada ya tukio la Hai na siyo kabla???
 
Kila Waziri anatafuta sifa
Migodi na viwanda ikitiririsha sumu mnaanza kulalama serikali haifanyi kazi haijali wananchi wake..

Inapoamua kuchukua hatua kwa kuwalinda wananchi wake mnasema anatafuta sifa.

Kweli Tanzania tunastahili namba moja kwa unafiki Duniani.
 
Guys, try to think big please. Sababu za kuvunja hii Bodi ya NEMC si issue ya Uwekezaji baali ni baada ya Mahakama wilaya ya Hai kumtia hatiani DC kwa kuharibu shamba la Mhe. Mbowe kwa kisingizio cha kuharibu Mazingira huku NEMC wakimkana DC kuwa hawakumtuma!! Kwanini Bodi ivunjwe sasa baada ya tukio la Hai na siyo kabla???
You are right mkuu
 
Migodi na viwanda ikitiririsha sumu mnaanza kulalama serikali haifanyi kazi haijali wananchi wake..

Inapoamua kuchukua hatua kwa kuwalinda wananchi wake mnasema anatafuta sifa.

Kweli Tanzania tunastahili namba moja kwa unafiki Duniani.
Nilijua tu CCM ni ya wajinga na masikini (TWAWEZA)
 
Lile Biff la NW na Waziri wake limeisha?? Nasikia amewekewa NW kanda maarum iw rahisi kumdhibiti je ni kweli??? Maana huyu kijana ndio alikuwa msiri wa JK.....kama alivyo Bashite kwa sasa! Yeye ndio anatafuta waganga na kuwalipa!! Kazi ipo watoto pendwa wa awamu 4 na ya 5
Mashuuuz jazz band at its best
 
Jamaniii this can only happen in Tz. Hivi linawezekana kufanya eia wakati mradi uko under construction?

Suppose eneo la mradi ni vulnerable and so ikatolewa project alternatives kwamba mradi usiwepo inakuwaje?

Project ninatakiwa intake off once eia report imekàmilika na faults zimeshatafutiw uvumbuzi. Naona kilio kingine exactly kama kile cha KTM na wakazi wa kizuiani.

Let's wait and see

Sent from my Royale A1 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom