Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,812
- 11,987
Baraza la Usimamizi na Utunzaji Mazingira Nchini NEMC imetoa mwezi mmoja kwa viwanda vinavyozalisha chupa za plastiki zenye rangi kuweka utaratibu wa kukusanya na kuhifadhi chupa za rangi ambazo zimekuwa zinachafua mazingira kwa kuzagaa maeneo mbalimbali.
Mkurugenzi wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Dkt. Samweli Gwamaka amewataka wamiliki wa viwanda hivyo kuweka utaratibu wa ambavyo vinatumia chupa za rangi kuweka utaratibu wa kurejeleza chupa hizo ili kuepuka uchafuzi wa mazingira
Dkt. Gwamaka amesema NEMC itafungia lile eneo tu linalofanya uzalishaji wa chupa za rangi mpaka watakapoweka mpaka wa kurejereza chupa hizo kwa ajili ya kutunza mazingira.
DKT. SAMWELI GWAMAKA - Mkurugenzi Mkuu NEMC
Kuhusu chupa za rangi kuchafua mazingira hasa pale zinapotupwa kwenye mitaro ya maji hasa katika maeneo mbalimbali hasa jiji la Dar es salaam, Baadhi ya wananchi wamesema wamiliki wa viwanda wanalo jukumu la kulinda mazingira kwa kutengeneza chupa ambazo ni rafiki kwa mazingi.
Utupaji wa chupa za rangi au plastiki katika mazingira unatajwa kama uchafuzi wa mazingira ambao unaweza ukaleta atahari kwa jamii kama vile mlipuko wa magonjwa na Ili kuendelea kutunza na kuhifadhi mazingira dhidi ya taka hizo jamii imezitaka mamlaka kuhakikisha wamiliki wa viwanda wanazalisha chupa rafiki.
Katika hatua nyingine Dkt. Gwamaka ametoa tahadhari kwa wachimbaji wa madini ambao wanamiliki visima vya tope sumu kuchukua tahadhari mapema ili kuepuka madhara yanayoweza kujitokeza pindi mabwawa yatakapojaa hasa kipindi hiki cha mvua ambazo zinaendelea kunyesha.
DKT. SAMWELI GWAMAKA - Mkurugenzi Mkuu NEMC
Mkurugenzi wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Dkt. Samweli Gwamaka amewataka wamiliki wa viwanda hivyo kuweka utaratibu wa ambavyo vinatumia chupa za rangi kuweka utaratibu wa kurejeleza chupa hizo ili kuepuka uchafuzi wa mazingira
Dkt. Gwamaka amesema NEMC itafungia lile eneo tu linalofanya uzalishaji wa chupa za rangi mpaka watakapoweka mpaka wa kurejereza chupa hizo kwa ajili ya kutunza mazingira.
DKT. SAMWELI GWAMAKA - Mkurugenzi Mkuu NEMC
Kuhusu chupa za rangi kuchafua mazingira hasa pale zinapotupwa kwenye mitaro ya maji hasa katika maeneo mbalimbali hasa jiji la Dar es salaam, Baadhi ya wananchi wamesema wamiliki wa viwanda wanalo jukumu la kulinda mazingira kwa kutengeneza chupa ambazo ni rafiki kwa mazingi.
Utupaji wa chupa za rangi au plastiki katika mazingira unatajwa kama uchafuzi wa mazingira ambao unaweza ukaleta atahari kwa jamii kama vile mlipuko wa magonjwa na Ili kuendelea kutunza na kuhifadhi mazingira dhidi ya taka hizo jamii imezitaka mamlaka kuhakikisha wamiliki wa viwanda wanazalisha chupa rafiki.
Katika hatua nyingine Dkt. Gwamaka ametoa tahadhari kwa wachimbaji wa madini ambao wanamiliki visima vya tope sumu kuchukua tahadhari mapema ili kuepuka madhara yanayoweza kujitokeza pindi mabwawa yatakapojaa hasa kipindi hiki cha mvua ambazo zinaendelea kunyesha.
DKT. SAMWELI GWAMAKA - Mkurugenzi Mkuu NEMC