Waziri Makamba afanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Israel, Eli Cohen

benzemah

JF-Expert Member
Nov 19, 2014
1,504
3,034
Kupitia ukurasa binafsi wa mtandao wa X (Zamani Twitter) wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika. Mashariki, January Makamba ameandika ujumbe kuwa mapema leo amefanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Israel, Eli Cohen

Ujumbe huo umeeleza kuwa Waziri Cohen ameahidi Serikali ya Israel kuboresha juhudi za kuwatafuta
wanafunzi wawili wa Kitanzania ambao hawajulikani walipo tangu Oktoba 7.


Pia Waziri Makamba ameeleza kuwa Waziri Cohen amemfahamisha juu mtazamo wa Israel kuhusu mzozo unaoendelea hivi sasa huku yeye (Makamba) akisisitiza msimamo wa Tanzania kwamba kipaumbele kinapaswa kutolewa kwa:

(a) Kufuata sheria za kimataifa za kibinadamu, hasa ulinzi wa maisha ya raia
(b) Kusitisha operesheni za kijeshi ili kuruhusu juhudi za kibinadamu zisizo na vizuizi
(c) Kuanzisha upya mchakato wa amani ikiwa ndio suluhisho kwa mataifa mawili kama nguzo yake.

Screenshot 2023-11-07 at 14.28.35.png

Tulikubaliana kuendelea kuwasiliana.
 
Hiyo peace process hata mmarekani mwenyewe ameshindwa kumshawishi muisrael, ndio aje kuwa Makamba!
 
Bila Israel kukaa kwa amani, amani duniani haiwezi kuwepo kamwe kwa sababu Israel ni lango..........Kutoka 4:22 "Nawe umwambie Farao, Bwana asema hivi, Israeli ni mwanangu mimi, mzaliwa wa kwanza wangu"

kwa maana nyingine aina ya maisha au standard ya maisha na nyakati zake hapa duniani zinaamuliwa na standard ya maisha na nyakati zilizofungwa juu ya taifa la Israel, au kwa lugha nyingine ni kwamba survival ya uwepo wa dunia inategemea uwepo wa taifa la Israel.​
 
Atakuwa amezungumza na msaidizi wake, sidhani kama waziri wa Israel ana mda wa kuongea na akina makamba kipindi kama hiki
Siyo rahisi, unaona super powers wanavyopishana angani kwenda Israel eti leo huyu anayekula kwa urefu wa kamba yake akaongee na FM wa mayahudi?
 
Back
Top Bottom