WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi amekemea tabia ya kila mtu kuwa msemaji nchini hali inayopelekea utolewaji wa Matamko ambayo yamekua yakihatarisha hali ya Amani hapa nchini.
Ametoa kauli hiyo wakati wa Kikao na Uongozi wa Juu wa Jeshi la Polisi,Maafisa na Askari kilichofanyika jijini Dodoma.
“Kila Taasisi ina msemaji wake,hata katika familia kuna msemaji sasa inakuaje hapa nchini kila mtu akijisikia kusema anaongea tu," alisema Waziri Katambi.