beth,
Mkoa wa Geita unahitaji budget kubwa au Special request kwa ajili ya kuwafungia au kusambaza umeme kwenye migodi ya wachimbaji wa madini ya dhahabu.
Ombi letu kwa MH Waziri, wachimbaji na wazalishaji wa dhahabu mkoa wa Geita hawana na hawajafungiwa umeme ili waweze kufanya uchimbaji wa dhahabu kwa ufanisi mkubwa ambapo wangechangia mapato ya serikali ikiwa ni pamoja na Tanesco kuongeza mapato.
Changamoto iliyopo mkoa wa Geita ni kwamba Kuna miradi ya REA, ila miradi hiyo inatekelezwa kwenda kwa wananchi ambapo madini hayachimbwi kwa wananchi kuliko na REA, matokeo yake migodi karibu yote hawana na hawapatiwi umemekwa sababu hakuna REA.
Jambo la pili, kupeleka umeme kwenye maeneo ya migodi gharama ni kubwa hivyo wizara inabidi isaidie kuongeza budget ya mkoa wa Geita ili mkoa uweze kutoa huduma husika kwa wakati.
Meneja wa Tanesco mkoa wa Geita anafanya kazi usiku na mchana ikiwa ni pamoja na wafanyakazi anaowaongoza, changamoto ansyoipata na kushindwa kumsaidia kupeleka umeme kwenye maeneo ya migodini ni ufinyo wa budget au kukosa fedha za miradi hiyo,tunaomba awezeshwe kazi anaiweza kwa asilimia 100.
Tutashukuru iwapo kilio cha wachimbaji wa dhahabu kitasikilizwa na kupatiwa uvumbuzi wa haraka wa kupatiwa umeme ili waweze kuzalisha dhahabu kwa kutumia vifaa vya kisasa vinavyotumia umeme na kurahisisha muda kwa kuongeza uzalishaji na ukizingatia soko la kisasa tunalo,sambamba na wananchi waweze kupata ajira, kuchangia Pato la Taifa na Tanesco kupata fedha za kujiendesha kwa faida.