#COVID19 Waziri Gwajima: Tanzania maambukizi yafikia watu 47 toka 14 kwa siku

Mkuu hebu fafanua kauli nzito sna hii
Hawezi kusema uongo ambao hata zombie atashituka.
Yaani Kati ya Watanzania 10 wanaokufa na Corona 7 hawajachanjwa.
Kwa mahesabu ya darasa la pili waliochanjwa hawafiki 1.5m ya Watanzania 60m.
Maiti zingeokotwa barabarani maana wangekuwa wanakufa Watu wengi Sana.
 
Hawezi kusema uongo ambao hata zombie atashituka.
Yaani Kati ya Watanzania 10 wanaokufa na Corona 7 hawajachanjwa.
Kwa mahesabu ya darasa la pili waliochanjwa hawafiki 1.5m ya Watanzania 60m.
Maiti zingeokotwa barabarani maana wangekuwa wanakufa Watu wengi Sana.
Daaah aise
 
Halafu wale waliochanjwa wanakufa kwa magonjwa nyemelezi siyo Corona.

Hata walitengeneza chanjo hawawezi kuukubali uongo huu.

Wala hagusii Omicron inayoua hata waliochomwa booster dose.
Mhuni huyu mama.
Mama amejibu kitaalamu wewe unakuja na maneno ya korosho tu,
 
WAZIRI DK DOROTHY GWAJIMA AZINDUA MPANGO WA JAMII HARAKISHI NA SHIRIKISHI WA CHANJO YA COVID -19 AWAMU YA PILI

===
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima amezindua Kampeni Harakishi na Shirikishi kwa Jamii awamu ya pili na kusema, changamoto za uwepo wa UVIKO 19 ni changamoto kwa maendeleo ya dunia nzima ikiwemo na Tanzania.

Dkt. Gwajima, ameyasema hayo leo Desemba 22, 2021, mkoani Arusha, ambapo Hafla hiyo imefanyika na kuhudhuriwa na Viongozi wa Serikali, Dini pamoja na Jamii sambamba na Wananchi wa Arusha na Mikoa ya Jirani.

Akizindua Mpango huo, Dkt. Gwajima, amesema, katika kipindi cha kuanzia Mwezi Disemba, 2021 nchi yetu pia imeshuhudia kuendelea kuongezeka kwa maambukizi mapya ya UVIKO-19 kutoka maambukizi 14 kwa siku hadi 47 miongoni mwa wasafiri kwa takwimu za vipimo vya maabara kuu ya taifa.

"Mafanikio ya mapambano haya yanategemea zaidi jinsi gani Wakuu wa Mikoa na vyombo vyenu mmeendelea kujipanga kila siku, kwa kuboresha mikakati ya kuwafikia wananchi hadi ngazi ya mitaa, vijiji na vitongoji ili waelimike wajikinge na wapate huduma ya chanjo. Alisema Dkt. Gwajima.

Kampeni ya kaya kwa kaya ya kuwashirikisha viongozi wa mitaa, vijiji na vitongoji inadhamira ya kuona mikoa mingine inafanya na kupata mafanikio makubwa zaidi kama Mwanza, Kagera na Ruvuma ilivyofanikiwa.

Dkt. Gwajima ametumia fursa hiyo, kuwaomba, Viongozi wa Mikoa na Halmashauri wanakua bega kwa bega ili kufikia azma yakuchanja watu wapatao 4000 hadi 5000 kwa Mkoa na watu 80,000 hadi 100,000 kwa nchi nzima kila siku.

Akitoa taarifa wakati wa hafla hiyo, Katibu Mkuu Wizara ya Afya Prof. Abel Makubi alisema, kwa sasa wameanza kufanya utafiti wa chanjo na wataendelea kutoa taarifa wapi tumefikia kwenye Chanjo hiyo, aidha "kwa sasa nchi ina mitambo ya kufua hewa ya Oksijeni kwenye hospitali zetu, hii itasaidia kuokoa maisha kwa wahitaji wa hewa kama watoto njiti na wagonjwa wengine mahututi" Prof.Makubi.

Akiongea kwa niaba ya Wakuu wa Mikoa, Mwenyekiti wa Wakuu wa Mikoa, nchini ambaye pia ni Mkuu wa Arusha, John Mongella, alisema, wamejipanga kutekeleza maelekezo ya Serikali.

"Mhe Waziri, sisi ni Wasaidizi wa Mhe. Rais, hii ajenda ameibeba mwenyewe Rais, kwa kuanza kuchanja, na sisi wengine baada yakuona amechanja, Wakuu wa Mikoa wote tukachanja, hii ni kuonesha kuunga mkono mapambano haya" alisema Mongela.

Naye Prof. Riziki Shemdoe, Katibu Mkuu Tamisemi, akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Ummy Mwalimu, alisema, Mpango Harakishi na Shirikishi ni Mpango unaosimamiwa na Wizara zote ndio maana katika Kampeni hiyo wanashirikiana pamoja hasa ikizingatiwa kuwa Wizara hiyo ndio iliyo karibu zaidi na Wananchi.

Akitoa Salaam za Kamati ya Bunge, Mwenyekiti, Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi Mhe. Fatma Tofiq, amesema wanaihakikishia Serikali, kuwa bega kwa bega katika kusukuma ajenda ya Chanjo. Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii Mhe. Dkt. Stanslaus Nyongo amempongeza Wizara ya Afya kwa namna ilivyoweza kutekeleza Maekezo ya Serikali pamoja na yale ya Bunge

^Mhe. Waziri kwaniaba ya Kamati ya Bunge, niwapongeze sana kwa jinsi mnavyotekeleza Maelekezo ya Bunge, lakini pia ya Serikali, niahidi kwaniaba ya Kamati kuendelea kukupa Ushirikiano wakati wote na kuwashauri inavyopaswa" Alisema Mhe. Nyongo.

Katika Hafla.hiyo, Waziri wa Afya, Dkt. Dorothy Gwajima aliitaja Mikoa vinara kwa Chanjo yaani iliyofanya vizuri katika Chanjo mpaka sasa kuwa ni Ruvuma, Mwanza, Dodoma, Kagera na Mara. huku akiitaka Mikoa mingine kuongeza bidii

View attachment 2053776



View attachment 2053779

View attachment 2053780

View attachment 2053781

View attachment 2053783
Gwajima anafanya kazi nzuri sana aise
 
Wadau na Wakuu heshima yenu,
Naomba Kuuliza maswali ya Mtu nisielewa Kuhusu Afya na Kirusi,
Naomba Msinicheke...
Nahitaji Elimu wandugu.

Naomba Kuuliza kwa wataalam:
Hivi Kama Mtu hajachanjwa Mpaka sasa,
1. Je akiugua Corona sasa hivi atakuwa ameugua corona ipi? Ile ya Kwanza, Ya Pili ya Tatu au hii Omicroni?

2. Je ina Maana Zile Corona na Mwanzo Hazipo? Kama Zipo Zina Nguvu ya Kuwashambulia watu wasiochanjwa?
Kama Hazina Nguvu sasa Wasiochanjwa wamepata Kinga ya Mwili?

3.Hii Omicron na Yenyewe Kuna watu wamepata Mafua na Homa za Hapa na Pale na Wanaendelea Ku recover na Hawajachanjwa sasa Baadae Wakihitajika Kuchanjwa? Wanachanjwa kwa ajili ya wimbi lipi?
Kuanzia La Kwanza? Au hili la Sasa hivi?
Naomba Majibu wataalam

Hakuna anaeweza kukujibu mkuu! Maana wanapita kimya kimy
 
WAZIRI DK DOROTHY GWAJIMA AZINDUA MPANGO WA JAMII HARAKISHI NA SHIRIKISHI WA CHANJO YA COVID -19 AWAMU YA PILI

===
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima amezindua Kampeni Harakishi na Shirikishi kwa Jamii awamu ya pili na kusema, changamoto za uwepo wa UVIKO 19 ni changamoto kwa maendeleo ya dunia nzima ikiwemo na Tanzania.

Dkt. Gwajima, ameyasema hayo leo Desemba 22, 2021, mkoani Arusha, ambapo Hafla hiyo imefanyika na kuhudhuriwa na Viongozi wa Serikali, Dini pamoja na Jamii sambamba na Wananchi wa Arusha na Mikoa ya Jirani.

Akizindua Mpango huo, Dkt. Gwajima, amesema, katika kipindi cha kuanzia Mwezi Disemba, 2021 nchi yetu pia imeshuhudia kuendelea kuongezeka kwa maambukizi mapya ya UVIKO-19 kutoka maambukizi 14 kwa siku hadi 47 miongoni mwa wasafiri kwa takwimu za vipimo vya maabara kuu ya taifa.

"Mafanikio ya mapambano haya yanategemea zaidi jinsi gani Wakuu wa Mikoa na vyombo vyenu mmeendelea kujipanga kila siku, kwa kuboresha mikakati ya kuwafikia wananchi hadi ngazi ya mitaa, vijiji na vitongoji ili waelimike wajikinge na wapate huduma ya chanjo. Alisema Dkt. Gwajima.

Kampeni ya kaya kwa kaya ya kuwashirikisha viongozi wa mitaa, vijiji na vitongoji inadhamira ya kuona mikoa mingine inafanya na kupata mafanikio makubwa zaidi kama Mwanza, Kagera na Ruvuma ilivyofanikiwa.

Dkt. Gwajima ametumia fursa hiyo, kuwaomba, Viongozi wa Mikoa na Halmashauri wanakua bega kwa bega ili kufikia azma yakuchanja watu wapatao 4000 hadi 5000 kwa Mkoa na watu 80,000 hadi 100,000 kwa nchi nzima kila siku.

Akitoa taarifa wakati wa hafla hiyo, Katibu Mkuu Wizara ya Afya Prof. Abel Makubi alisema, kwa sasa wameanza kufanya utafiti wa chanjo na wataendelea kutoa taarifa wapi tumefikia kwenye Chanjo hiyo, aidha "kwa sasa nchi ina mitambo ya kufua hewa ya Oksijeni kwenye hospitali zetu, hii itasaidia kuokoa maisha kwa wahitaji wa hewa kama watoto njiti na wagonjwa wengine mahututi" Prof.Makubi.

Akiongea kwa niaba ya Wakuu wa Mikoa, Mwenyekiti wa Wakuu wa Mikoa, nchini ambaye pia ni Mkuu wa Arusha, John Mongella, alisema, wamejipanga kutekeleza maelekezo ya Serikali.

"Mhe Waziri, sisi ni Wasaidizi wa Mhe. Rais, hii ajenda ameibeba mwenyewe Rais, kwa kuanza kuchanja, na sisi wengine baada yakuona amechanja, Wakuu wa Mikoa wote tukachanja, hii ni kuonesha kuunga mkono mapambano haya" alisema Mongela.

Naye Prof. Riziki Shemdoe, Katibu Mkuu Tamisemi, akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Ummy Mwalimu, alisema, Mpango Harakishi na Shirikishi ni Mpango unaosimamiwa na Wizara zote ndio maana katika Kampeni hiyo wanashirikiana pamoja hasa ikizingatiwa kuwa Wizara hiyo ndio iliyo karibu zaidi na Wananchi.

Akitoa Salaam za Kamati ya Bunge, Mwenyekiti, Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi Mhe. Fatma Tofiq, amesema wanaihakikishia Serikali, kuwa bega kwa bega katika kusukuma ajenda ya Chanjo. Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii Mhe. Dkt. Stanslaus Nyongo amempongeza Wizara ya Afya kwa namna ilivyoweza kutekeleza Maekezo ya Serikali pamoja na yale ya Bunge

^Mhe. Waziri kwaniaba ya Kamati ya Bunge, niwapongeze sana kwa jinsi mnavyotekeleza Maelekezo ya Bunge, lakini pia ya Serikali, niahidi kwaniaba ya Kamati kuendelea kukupa Ushirikiano wakati wote na kuwashauri inavyopaswa" Alisema Mhe. Nyongo.

Katika Hafla.hiyo, Waziri wa Afya, Dkt. Dorothy Gwajima aliitaja Mikoa vinara kwa Chanjo yaani iliyofanya vizuri katika Chanjo mpaka sasa kuwa ni Ruvuma, Mwanza, Dodoma, Kagera na Mara. huku akiitaka Mikoa mingine kuongeza bidii

View attachment 2053776



View attachment 2053779

View attachment 2053780

View attachment 2053781

View attachment 2053783
Atupe maelekezo tuliochanja J and J tunaweza kuchanjwa Moderna au Pfizer naona Israel wanachanja mpaka chanjo ya 4 wengine sio wafuasi wa tapeli Askofu Gwajima
 
Tanzania ni kichwa cha mwendawazimu kinachotembea.
 
Hawezi kusema uongo ambao hata zombie atashituka.
Yaani Kati ya Watanzania 10 wanaokufa na Corona 7 hawajachanjwa.
Kwa mahesabu ya darasa la pili waliochanjwa hawafiki 1.5m ya Watanzania 60m.
Maiti zingeokotwa barabarani maana wangekuwa wanakufa Watu wengi Sana.
Mkuu Waziri alisema kati ya WAGONJWA kumi waliolazwa, saba hawajachanjwa.
 
Wadau na Wakuu heshima yenu,
Naomba Kuuliza maswali ya Mtu nisielewa Kuhusu Afya na Kirusi,
Naomba Msinicheke...
Nahitaji Elimu wandugu.

Naomba Kuuliza kwa wataalam:
Hivi Kama Mtu hajachanjwa Mpaka sasa,
1. Je akiugua Corona sasa hivi atakuwa ameugua corona ipi? Ile ya Kwanza, Ya Pili au ya Tatu au hii Omicroni?

2. Je ina Maana Zile Corona na Mwanzo Hazipo? Kama Zipo Zina Nguvu ya Kuwashambulia watu wasiochanjwa?
Kama Hazina Nguvu sasa Wasiochanjwa wamepata Kinga ya Mwili?

3.Hii Omicron na Yenyewe Kuna watu wamepata Mafua na Homa za Hapa na Pale na Wanaendelea Ku recover na Hawajachanjwa sasa Baadae Wakihitajika Kuchanjwa? Wanachanjwa kwa ajili ya wimbi lipi?
Kuanzia La Kwanza? Au hili la Sasa hivi?
Naomba Majibu wataalam
Japo siyo mtaalam wa afya ila ninajitahidi kusoma na kuuelewa huu ugonjwa. Ngoja nikushirikishe nilichoelewa:

1. Corona ni aina ya ugonjwa unaosababishwa na kirusi. Kirusi hiki (kama kawaida ya virusi) huendelea kuishi kwa kujibadilisha ili kikabiliane na kinga ya mwili. Kinga ikiwa imara mtu anaweza akapambana nao na kukishinda nguvu kirusi. Sasa wakati wa mapambano kirusi kinauwezo wa kujibadilisha na unapomuambukiza mtu mwingine, unakuta kile kirusi kinaenda kwake na nguvu nyingine. Ndio maana baada ya muda kunakuwa na aina mbalimbali ya kirusi kile kikiwa na mabadiliko ya nguvu na mashambulizi. Sasa hivi ukiugua inategemea umeambukizwa kirusi kipi. Inawezekana ni Omicron au Delta au hata ukute kilishabadilika tena. Mpaka maabara wafanye utafiti wa kirusi ulichonacho ndio wajue ni aina gani.

2. Sifahamu ni variants gani zipo wapi kwa sasa ila Omicron imepewa uzito kwasababu ndio aina mpya iliyozaliwa hivi karibuni. Kuna uwezekano mkubwa sana kwamba zile variant/aina nyingine bado zipo. Kama umechanjwa kinga yako imeongezewa uwezo wa kupambana nao. Yaani virusi havitakudhuru sana kama mtu asiye na kinga yakutosha. Ndio maana wanasisitiza wenye magonjwa nyemelezi au wenye kinga hafifu wachanje. Sasa, tatizo linakuja pale ambapo kirusi kinapoendelea kuambukizana hata kwa watu wenye chanjo kinazidi kujizatiti na mwisho kinajifunza jinsi ya kupambana na kinga za mwili. Kinapozaliwa kingine kinakuwa na uwezo zaidi wa kupambana na kinga hata ile iliyoongezewa kwenye chanjo. Ndio maana wanazungumzia booster shot, yaani chanjo inaimarishwa kudhibiti aina mpya zinazozaliwa. Sasa kirusi chochote tabia yake nikuongezeka kwa kasi, kujizatiti na kusambaa kwa kasi. Ndio maana watu wanatakiwa wachanje kwa wingi ili kupunguza kasi za maambukizi na kusambaa kwa kirusi ili kisipate nafasi ya kujibadili kwa haraka. Chanjo inapunguza kasi ya kusambaza na kuugua sana.

3. Unapo pata chanjo ni kwaajili ya kuuongezea mwili kinga ya kupambana na kirusi pindi ukikipata, pamoja na kupunguza kasi ya maambukizi. Ndio maana unashauriwa kupima kwanza kabla ya kuchoma chanjo. Kama ukikutwa na kirusi cha korona, wanashauri upone kwanza ndio uchome. Kama umeshapata corona na ukapona, mwili hubaki na kumbukumbu ya kinga mpaka miezi mitatu. Yaani ukiambukizwa tena ndani ya miezi mitatu, kinga itakumbuka jinsi ya kukabiliana na kirusi hicho. Chanjo nyingi hukaa hadi miezi sita (kwa taarifa za hivi karibuni), ndio maana nyingine unachoma mara mbili na sasa kuna ya tatu. Kila unapochomwa, chanjo huwa inaboreshwa kukabiliana na aina mpya zinzoibuka. Changamoto ni kwamba, wanasayansi wanaona mabadiliko makubwa kwa kipindi kifupi tofauti na aina nyingine na virusi kama influenza. Kwa wenzetu ambao wanaishi kwenye baridi kali huwa wanachoma booster za chanjo ya influenza kila mwaka, hasa kwa wazee na wenye magonjwa ya kupunguza kinga ya mwili.

Natumaini maswali yako yamejibika. Wataalam wanaweza kuja kuongezea au kukosoa.
 
Nilimsikiliza alisema wanaokufa siyo waliolazwa,
Ni muongo kupindukia huyu mama.
Nimecheki kwenye ukurasa wa Wizara ya afya huko Twitter, naona waziri aliteleza labda...
1640250689300.png
 
Corona ni futa, ukijifukizisha katika 100 digrii sentigredi linapasuka paaah, unapona sasa mnaogopa nini ?
 
Back
Top Bottom