KWA UFUPI kuhusu hiyo film ya DISCOUNT OUR LIVES:
1. Kwanza wanaanza kwa kuingiza Wabunge wengi sana Bungeni na hata kuweka Mawaziri au Rais. Hili waweza kuliona kwa sababu Rostam Azziz ndivyo alivyofanya kwa kuweka Serikali yake hapo mwaka 2005 ambayo hadi leo ndiyo wanatutawala.
2. Wakishaweka Serikali yao, ndipo wanaanza kuwaambia watu wao waandike sheria ambazo zitawalinda wao na huo wizi wao. Maadamu wengi hatujui sheria, wakati Wabunge wanajadili, hata hatujui nini kinaendelea. Labda hapo awepo mtu kama Tundu Lissu. Ila na yeye atatukanwa na watu kama Serukamba (Mzee wa F*ck you) na kutemwa na watu kama Mwigulu Nchemba. Atakalishwa chini na Naibu Spika Ndungay au Mama Spika mwenyewe na mwisho hata Ikulu watasema anajua sana Sheria ila anachanganya mambo na kuwachanganya wenzake.
3. Kwenye Mitandao nako watakuja hawa watu wao na kumtukana kila anayejaribu kuhoji kwa nini iko hivyo.
4. Sheria ikishapitishwa na wakasubiri ipoe poe kidogo, ndipo wanaanza sasa huo wizi wao. Mkianza kulalamika, unakuta kwamba mbona sheria zinaruhusu na hii ilishapitishwa miaka mingi na hamkulalamika? Wakati huo sasa unakuta kwamba, kwenye Board ya Vodacom, wanakuja kukaa washikaji zake Rais, Waziri Mkuu na wale wote waliokuwa wakipigia debe hiyo sheria. Utashangaa watu hao hulipwa fedha nyingi sana kwa kazi ambayo hata hawaifahamu na hawaifanyi ila ukweli ni kuwa mwisho wa siku, 2/3 ya hizo fedha, zinakwenda kwa Rais aliyepitisha sheria, Waziri Mkuu na Mawaziri wengine wahusika na wabunge walioipigia debe na kuifanya iwe sheria.
Nafikiri hapa ndiyo wengine inabidi wajiulize, fedha za Lowassa zinatoka wapi na akishashika madaraka, hayo makampuni yaliyomsaidia, yatataka asante ya kiasi gani? Ndiyo maana naipenda hiyo TITTLE ya film ya Wafaransa: DISCOUNT OUR LIVES au TUPUNGUZE BEI YA MAISHA YETU kwa maneno mengine, sisi wenyewe tunajishusha bei yetu wenyewe kwa kufurahia fedha za muda mfupi huku mbele yetu ni giza nene linatanda.
Nani wa kulaumu? Tuwalaumu wao au sisi wenyewe? Kwani wamekuja kwa nguvu kama zamani? Kwani wanatutawala? Kwani wanatuibia kwa nguvu? Kwani...... Hapana. Ni kama Trojan Horse ambapo sisi wenyewe na njaa zetu/tamaa zetu tunawafungulia mlango na kuwaingiza ndani kwa mikono miwili huku tukifurahia Pipi zao. Kesho wakianza kuchukua malipo yao ya hizo Pipi, tusianze kulialia kama watoto maana wenyewe tulitaka.
Wao kama wafanya biashara, wanataka faida na faida zaidi. Sisi na njaa zetu/tamaa zetu tuna DISCOUNT OUR LIVES.
CC:
Pasco Mtanzania @Mwanakijiji Fundi Mchundo Nyani Ngabu @JokaKuu FairPlayer faiza Foxy .....
Film:
NOS VIES DISCOUNT. - YouTube