Ngedere akila sana, iko siku ya kujuta.
Kujuta kujuta sana,mwenye shamba akistuka. Mtego atawekewa, tunduni aje kunaswa.
Wamenyonya vya kutosha, sasa lazima walipe.
Huruma sikuonei, hata kama kwa mtutu.
Halali yangu ulimi, wala situmii sumu.
Nitaitumia akili, kudai kilicho changu.
Ero umenichosha kweli, mtetezi nimempata.
Kelele tulizipiga, jamani mnatunyonya.
Masikio mkaziba, mkiendelea kula bata.
Dharau mkazileta, eti baki au nenda.
Mungu sio mdhalimu, leo katusikiliza
Tunayo mengi madai, Ero wanatunyanyasa.
Laki mbili na ushee,eti ndio mshahara.
Ukiumwa kafe mbele, hapa simu kwenda mbele.
Tutazamacho ubao, sifuri level ni mwiko.
Anzia moja hadi tisa, ni kuimba na wateja.
Hatuna cha sikukuu, siku zote jumatatu.
Tuko hapa sita siku, nani akupe pumziko.
Hata mwili ukichoka, lazima uusukume.
Vinginevyo ukikacha, kazi tena ndi basi.
Waziri kaza msuli, kuondoa unyonyaji.
Kina Ero na wenzake, funzo hili walipate.
Usije legeza kamba, ndegere ataponyoka.
Ili hili liwe funzo, hata kwa vizazi vyetu.
Wenzangu Tutulizane, mechi ndio imeanza.
Lazima tupate bingwa,hata kama kwa penati.
Waziri ni refa wetu,huyu hatatuangusha.
Ero na mama Kabaka, ni nani tabeba kombe.
Ngedere akila sana, iko siku ya kujuta.
Kujuta kujuta sana,mwenye shamba akistuka. Mtego atawekewa, tunduni aje kunaswa.
Wamenyonya vya kutosha, sasa lazima walipe.
Huruma sikuonei, hata kama kwa mtutu.
Halali yangu ulimi, wala situmii sumu.
Nitaitumia akili, kudai kilicho changu.
Ero umenichosha kweli, mtetezi nimempata.
Kelele tulizipiga, jamani mnatunyonya.
Masikio mkaziba, mkiendelea kula bata.
Dharau mkazileta, eti baki au nenda.
Mungu sio mdhalimu, leo katusikiliza
Tunayo mengi madai, Ero wanatunyanyasa.
Laki mbili na ushee,eti ndio mshahara.
Ukiumwa kafe mbele, hapa simu kwenda mbele.
Tutazamacho ubao, sifuri level ni mwiko.
Anzia moja hadi tisa, ni kuimba na wateja.
Hatuna cha sikukuu, siku zote jumatatu.
Tuko hapa sita siku, nani akupe pumziko.
Hata mwili ukichoka, lazima uusukume.
Vinginevyo ukikacha, kazi tena ndi basi.
Waziri kaza msuli, kuondoa unyonyaji.
Kina Ero na wenzake, funzo hili walipate.
Usije legeza kamba, ndegere ataponyoka.
Ili hili liwe funzo, hata kwa vizazi vyetu.
Wenzangu Tutulizane, mechi ndio imeanza.
Lazima tupate bingwa,hata kama kwa penati.
Waziri ni refa wetu,huyu hatatuangusha.
Ero na mama Kabaka, ni nani tabeba kombe.