Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,900
- 944
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro ameilekeza Bodi ya Filamu nchini ishirikiane na Sekta binafsi katika kuhakikisha filamu za Tanzania zinakua bora zaidi na zinapata soko la uhakika.
Dkt. Ndumbaro ametoa agizo hilo Oktoba 12, 2023 alipofanya ziara katika Bodi hiyo, ambapo ameitaka iendelee kudhibiti na kufanya uhakiki wa ubora wa Filamu ili kulinda Mila na desturi za Tanzania.
Ameitaka Bodi hiyo ibadilike na kwenda na wakati Ili kupanua wigo wa kuwahudumia wadau wake kibiashara na kuongeza mapato.
Dkt. Ndumbaro ametoa agizo hilo Oktoba 12, 2023 alipofanya ziara katika Bodi hiyo, ambapo ameitaka iendelee kudhibiti na kufanya uhakiki wa ubora wa Filamu ili kulinda Mila na desturi za Tanzania.
Ameitaka Bodi hiyo ibadilike na kwenda na wakati Ili kupanua wigo wa kuwahudumia wadau wake kibiashara na kuongeza mapato.