Angel Msoffe
JF-Expert Member
- Jun 21, 2011
- 6,781
- 1,639
Habari zilizotufikia jioni hii zinasema kwamba Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Celina-Ompeashi-Kombani (pichani), amefariki dunia leo huko India alikokuwa akipata matibabu ya saratani.-
Taarifa kutoka ofisi za Bunge zimethibitisha kifo hicho na kueleza kwamba mwili wa marehemu unategemewa kuwasili Dar es salaam siku ya Jumatatu, ambapo Bunge na Serikali zitasimamia maandalizi yote ya maziko na kumsafirisha kwa mazishi nyumbani kwa marehemu huko Mahenge ambako alikuwa Mbunge wa jimbo la Ulanga.-
bbc wametangaza mwili utaletwa jumamosi