Waziri Aweso aingia kati tatizo la maji Mwanza, atoa maagizo mazito

saidoo25

JF-Expert Member
Jul 4, 2022
602
1,407
Waziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema jitihada zinafanyika ili kurejesha huduma ya maji kwa wakazi wa Jiji la Mwanza wanaoishi katika maeneo ya miinuko baada ya mtambo wa Mabatini kupata hitilafu.

Waziri Aweso ameyasema hayo, Julai 22, 2022 baada ya kutembelea kituo cha uzalishaji maji Mabatini ambacho kwa takribani wiki tatu kimesababisha uzalishaji maji kupungua kutoka lita milioni 95 hadi lita milioni 80 kwa siku.


 
Waziri ashughulike na mifumo,

Asikimbie huko na huko "Kuzimu moto"
 
Back
Top Bottom