Ndugu,
Wewe endelea kuamini unachokiamini lakini na mimi ninacho kile ninachokifahamu kwa sababu CCM imeanza kujiandaa kwenye uchaguzi huu baada ya uchaguzi wa 2010 kumalizika.
Hii ni sawa na mwanafunzi ambaye amejiandaa vizuri kwa miaka minne kukabiliana na mtihani wa kidato cha nne ambao anategemea kufanya baada ya mwezi mmoja.
Kauli yangu iko palepale, Lowassa hashindi huu uchaguzi.
Mwanadiwani
Kama Lowasa hashindi huu uchaguzi si mtulie. Mnahangaika nini sasa? Kila kuchikicha Lowasa Lowasa. Nadhani hata usiku mkilala huwa mnaweweseka kwenye ndoto Lowasa Lowasa!
Ukweli mnaujua kuwa Lowasa ndiye rais ajae ila imekuwa ngumu kumeza ukweli huu.
La msingi hapa, nashauri wewe na wana sisiemu wenzako muanze kujiandaa kisaikologia na zaidi muanze kuhamisha makorokoro yenu pale magogoni mapema kabla Oct 25