Kampeni ya kutoa huduma ya chakula kwa wazee wanaokumbwa na tatizo la maisha imefanyika katika eneo la Luyang mjini Hefei, China. Migahawa 36 imefunguliwa katika eneo hilo, na kila mzee anaweza kupata ruzuku yuan 100 hadi 200 (sawa na dola 14 hadi 28 za kimarekani) kwa mwezi kulingana na hali halisi ya maisha yake.
Wazee hao wanaweza kufurahia huduma ya chakula kwenye migahawa hiyo, na gharama ya kila mlo inaweza kupunguzwa kwa yuan 4 hadi 5 (sawa na dola 0.6 hadi 0.7 za kimarekani).