dolevaby
JF-Expert Member
- Aug 25, 2013
- 12,956
- 9,478
Uwepo wao unamsaada Gani kwa Nchi sindio hao wanataka Katiba ibadilike ili watoto wao waendelee kugawana mamlaka hao wazee wako ni Hasara kwa NchiWazee muhimu ninamaanisha wazee wenye akili nyingi, wenye hekima na wanaoifahamu vema Tanzania. Wazee hawa ni wale wote wenye hadhi ya Mzee Ali Hassan Mwinyi, Mzee Kikwete, Mzee Warioba, Butiku, Cleopa Msuya, Malecela, Msekwa, Karume, na wengine wa aina hii.
Kule Marekani na Ulaya wazee wazee wao wa aina hii kama vile George Washington na wengine kabla ya kufa walihakikisha kuwa wanaacha checks and balance za kisiasa kwenye mataifa yao kwa kuacha vyama zaidi ya kimoja vyenye nguvu sawa na katiba imara ili viwasaidie wananchi wao baada ya wao watakapokuwa hawapo tena duniani. Waliacha dira za mataifa yao na vyama na taasisi imara zitakazoshindana kwenye kuitekeleza dira yao wakati wao hawapo duniani tena.
Mwalimu Nyerere ilikuwa anaifahamu siri hii ya mataifa ya ulaya na Marekani, lakini alishindwa kuitekeleza yote kwa 100% kutokana na waliokuwa wanamzunguuka kushindwa kumuelewa kabisa, alijaribu lakini hakufua dafu. Mwl. Nyerere alifahamu kuwa baada ya yeye kufariki dunia ile checks and balance aliyokuwa ikiifanya yeye haitakuwepo kabisa kutokana na hurka na ufahamu wa watu waliokuwa wakimzunguuka. Hii ndiyo sababu iliyomsukuma Baba wa Taifa kukubali na kulazimisha Tanzania ikubali mfumo wa vyama vingi vya siasa mwaka 1992 ingawa wenzake walimpinga. Yeye alitaka kuwepo na vyama 2 vya siasa vyenye nguvu sawa ili vikosoane kwenye masuala ya nchi. Yaani vishindane hoja na sera katika kuitawala nchi, chama kimoja kikizembea na kuboronga chama cha pili kinarekebisha kama inavyotokea Marekani, Uingereza na nchi nyingine za ulaya.
Nyerere aliwafahamu sana watu wake na CCM yake, alifajua tu kuwa akiondoka yeye CCM itatunga sheria na kanuni za Kikaburu za kuumiza watu bila kujali, watakuwa madalili wa mali za wananchi, watajilimbikizia mali na madaraka bila kuhojiwa na wataendelea kubaki madarakani kwa nguvu za dola. Na kweli sasa hivi CCM haitegemei kupiga kampeni tu ili kushinda chaguzi, zipo sheria na taratibu kwaajili ya kuibakisha CCM madarakani sio kwa manufaa ya watanzania na wana CCM bali kwaajili ya viongozi na familia zao. Leo hii nafasi zote nzuri za ajira na uongozi zimejaa watoto wa viongozi na jamaa zao zao.
Hata wanaCCM walio wengi wanatoka kapa, wanaambulia t-shirts na kofia na posho wakti wa kampeni baaaasi.
Wazee wetu hawa muhimu kama wataondoka duniani na kuviacha vyama vya upinzani vyootenchini vimekufa au havina nguvu kabisa wajue kuwa wameliacha taifa lisokuwa na matumaini, watakuwa wameiacha Tanzania kwenye njia mbaya kabisa kuwahi kutokea. Wameliacha taifa bila ya mtu wala taasisi yoyote inayoweza kuhoji chochote kizuri au kibaya kama wanavyohoji akina Mzee Butiku na Warioba wakati mwingine. Kila atakayehoji kitu kibaya atatungiwa sheria ya kumthibiti kama walivyokuwa wakifanya makaburu. Taifa litaanza upya kutafuta uhuru na demokrasia kwa njia ngumu sana.
Nitoe wito kwa hawa wazee waone mbele kama wezao akina washington na Nyerere kuhusu mataifa yao. Wasiangalie matumbo yao ya kizee eti kwasababu watoto wao pia wamejumuishwa kwenye ulaji. Ulaji wa aina hii haudumu na sisalama kwa taifa, sio kwamba watu wote (raia na askari) wataendelea kuangalia hali hii iendelee milele.
Sent from my CPH2179 using JamiiForums mobile app