Wazee muhimu wasife na kuicha CCM peke yake

Hao wazee tuwaache wapumzike na washauri wakiweza.
Watu wenye nguvu ya kimwili na kiakili wawajibike kulinda taifa.
We must have a competent succession plan. ni msur

Hao wazee tuwaache wapumzike na washauri wakiweza.
Watu wenye nguvu ya kimwili na kiakili wawajibike kulinda taifa.
We must have a competent succession plan.
Wazee hawa ni msululu wa wa watanzania wenzetu ambao walihakikisha kuwa CCM haitoki madarakani litoke jua inyeshe mvua. Wanafanya hivyo huku wakifahamu kuwa sera za CCM kwa miaka zaidi ya 60 ya uhuru zimeshindwa:
1. kuwapatia maji wananchi, hadi leo watu na wanyama wanakunywa pamoja.
2. Kuwapatia matibabu watanzania wote
3. Kuinua Kilimo
4. Zimeua Elimu yetu, watu wanahangaika kupeleka watoto wao Kenya na Uganda
5. Zimeshindwa kupanga miji
6. Zimeshindwa kusafisha miji
7. zimeshindwa kulipa mishahara kwa watumishi. Kima cha chini hakizidi dola 120 kwa mwezi miaka 60 ya uhuru.
8. Hakuna hata soko la mahindi
Mwalimu alifanya kosa kubwa kutubadilishia kipande tu cha Katiba ili kuruhusu siasa ya vyama vingi... Kwa kweli mabadiliko haya yameghalimu maisha ya watanzania wengi mno hadi muda huu - mfumo huu umefanya watu kufa, kufilisiwa, kufungwa, kunyanyashwa nk

Mwalimu angetupatia katiba mpya kabla ya kughatuka, kwa kweli katuachia mzigo mkubwa mno kiasi cha kuligawa Taifa letu makundi mawili - wanaotaka mfumo wa mwaka 1977 ambao chama tawala ndicho kinachoshika hatamu ya uongozi mia kwa mia na wale wanaotaka mfumo wa kidemokrasia, taasisi za kutoa haki kuwa huru bila kuingiliwa na watawala.

Bado tupo katika giza nene, Mwalimu umetuachia mzigo mzito mno.
Mwl. Nyerere hata yeye alilijutia kosa hili. Alidhani baada ya kung'utuka angemuamrisha chakufunga na lakufanya yule aliyemuachia kijiti, lakini looo, haikuwa hivyo, ikamlazimu ashinde nyuma ya vipaza sauti akimkosoa mteule wake hadi akamuandikia kitabu cha kukosoa siasa na uongozi wake. Kabla hajageuka wenzake wakalifuta Azimio lake la Arusha na kuja na la Zanzibar. Wenzake wakawa matajiri wa kupindukia ghafla wakayauza mashirika yote na kuyabinafsisha mengine huku akiangalia kwa macho yake bila kuwa na la kufanya kwa mujibu wa katiba yake yeye mwenyewe. Twiga wakawa wanapanda ndege wazimawazima.

Wanakula bila kunawa na kila anaewakosoa Wana wivu wa kike.
 
Ukikumbuka yaliyotokea Zanzibar katika uchaguzi wa Mwaka 1995, namna ambavyo CUF wali-perform, nashindwa kukubaliana na wewe juu ya Nyerere na dhamira ya dhati ya mfumo wa vyama vingi.

Kaunda aliyekubali kushindwa, waiona nchi yake ikibadilisha vyama bila bughudha!
Mwl Nyerere ni muumini wa umoja wa Afrika, Sadc, Africa Mashariki na Muungano, Kosa kubwa la CUF wakati ule lilikuwa kuulaumu muungano wa Nyerere na karume na kuonyesha kuwa kama CUF ingeshinda ingeuvunja muungano. Hili ndio kosa kubwa la maalim seif. Hata zoezi la kupata katiba mpya lilikwamishwa pia na CUF juu ya aina ya Muungano.

Nyerere asingekubali kamwe muungano uvunjike mbele yake. Na hii inaifanya CCM itafute sababu ya kuendelea kubaki madarakani ili kuulinda muungano. Ili CUF na pengine hata wapinzani wote waachane na kuuchokonoa Muungano hata kidogo ili watoboe. Hata miuungano ya Marekani na uingereza Ina matatizo makubwa sana lakini vyama vyao vya siasa hakuna kinachoigusa miungano Yao, ni mwiko mkubwa kutaja muungano wa USA bila kupata kashikashi.
 
Umeandika vizuri sana. Ila hao wazee uliowataja katika vipindi vyao nao walikuwa hovyoo hovyoo tuu..kama jk na msuyaa.. kidogo kina warioba waliofanya kazi na mwalimu. Cha msingi hapo ni kwamba nchi hii haiwez kombolewa na mikono ya hao wazee uchwara bali ni jukumu la wananchi wenyewe kuikomboa nchi yao!
Wananchi kivipi mkuu??? Wananchi wa hii inchi niwaoga kinoma na tumefundishwa uwoga kwa makusudi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hao wazee tuwaache wapumzike na washauri wakiweza.
Watu wenye nguvu ya kimwili na kiakili wawajibike kulinda taifa.
We must have a competent succession plan. ni msur

Hao wazee tuwaache wapumzike na washauri wakiweza.
Watu wenye nguvu ya kimwili na kiakili wawajibike kulinda taifa.
We must have a competent succession plan.
Wazee hawa ni msululu wa watanzania wenzetu ambao walihakikisha kuwa CCM haitoki madarakani litoke jua inyeshe mvua. Wanafanya hivyo huku wakifahamu kuwa sera za CCM kwa miaka zaidi ya 60 ya uhuru zimeshindwa:
1. kuwapatia maji wananchi, hadi leo watu na wanyama wanakunywa pamoja.
2. Kuwapatia matibabu watanzania wote
3. Kuinua Kilimo
4. Zimeua Elimu yetu, watu wanahangaika kupeleka watoto wao Kenya na Uganda
5. Zimeshindwa kupanga miji
6. Zimeshindwa kusafisha miji
7. zimeshindwa kulipa mishahara kwa watumishi. Kima cha chini hakizidi dola 120 kwa mwezi miaka 60 ya uhuru.
8. Hakuna hata soko la mahindi
 
Natamani sana siku moja JWTZ washike nchi hii na kuwakamata viongozi wote hawa wanaolihujumu taifa kwa tozo za wizi kwa raia wake. Jeshi la wananchi linatakiwa kuwalinda wananchi wake toka mikononi mwa makaburu weusi na huenda likitokea hili likasaidia wanaofata kutuheshimu raia dhidi ya wezi wa mali zetu za taifa
 
Natamani sana siku moja JWTZ washike nchi hii na kuwakamata viongozi wote hawa wanaolihujumu taifa kwa tozo za wizi kwa raia wake. Jeshi la wananchi linatakiwa kuwalinda wananchi wake toka mikononi mwa makaburu weusi na huenda likitokea hili likasaidia wanaofata kutuheshimu raia dhidi ya wezi wa mali zetu za taifa
Huko wenzanko ndio wanakula Maisha first class.

Unajuwa mshahara wa koplo tu ni kiasi gani kwa mwezi?
 
Huko wenzanko ndio wanakula Maisha first class.

Unajuwa mshahara wa koplo tu ni kiasi gani kwa mwezi?
Kinachotosha ni maisha Bora kwa kila mtanzania; maji, barabara, pembejeo, masoko, matibabu, tozo ndogo za miamala, riba ndogo za mikopo, na upatikanaji wa mikopo na haki za raia.

Labda askari mpuuzi TU ndiye atakae furahia mshahara mnono ambao hautoshi kuwasaidia wazazi, na ndugu zake wote. Kuwa na mshahara mkubwa peke yako kwenye ukoo maskini ni kazi bure.
 
Mwalimu alifanya kosa kubwa kutubadilishia kipande tu cha Katiba ili kuruhusu siasa ya vyama vingi... Kwa kweli mabadiliko haya yameghalimu maisha ya watanzania wengi mno hadi muda huu - mfumo huu umefanya watu kufa, kufilisiwa, kufungwa, kunyanyashwa nk

Mwalimu angetupatia katiba mpya kabla ya kughatuka, kwa kweli katuachia mzigo mkubwa mno kiasi cha kuligawa Taifa letu makundi mawili - wanaotaka mfumo wa mwaka 1977 ambao chama tawala ndicho kinachoshika hatamu ya uongozi mia kwa mia na wale wanaotaka mfumo wa kidemokrasia, taasisi za kutoa haki kuwa huru bila kuingiliwa na watawala.

Bado tupo katika giza nene, Mwalimu umetuachia mzigo mzito mno.
Usemayo ni kweli kabisa,sijui alikwama wapi?

Sent from my VF-795 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom