Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 22,606
- 29,754
Nachelea kuita ONYO kwa CCM.
Angalizo hili linaweza likawa la mwisho yaani msipoangalia kuna dalili mbaya sana ambayo itawagharimu na kutikisa Afrika.
Kuendelea kukumbatia Katiba inayopigiwa kelele na wananchi kuwa haifai kwa mfumo wa siasa za vyama vingi, ni sawa na kulalia kitanda cha misumari huku godoro liliwa ni kipande cha gunia.
Nimeona, yes nimesikia masikioni kwangu. Inawezekana sauti hii ilikuwa kutoka upande wa pili wa ukuta ambapo sijaweza asilani kufahamu nani alikuwa mzungumzaji. Lakini sauti inasema kuwa KIPIMO KILE MLICHOWAPIMIA WENGINE NDICHO MTAKACHOPIMIWA NA KUJAZWA KWA KUFURIKA.
Katiba hii tuliyonayo sasa ambayo mnaamini ndiyo ulinzi wa Taifa letu ni Katiba inayotoa maelekezo na maagizo muhimu (japo kwa uchache) ya maongozi ya nchi hususani kwenye Haki na Wajibu. Bahati mbaya sana mmeweka pamba masikioni na kujiweka kwenye daraja la kuwa wenye akili na ufahamu kuliko raia wote wa nchi hii. Maamuzi mengi mnayoyafanya (CCM) ni kwa maslahi mapana ya chama na walioshika madaraka.
Siku hazigandi, kwa sababu baada ya kiangazi huja mvua, mvua inaweza kugharikisha na kuporomosha milima kwa nguvu itokanayo na matone ya maji yaliyojikusana sehemu moja na kusaka njia ya kupita.
Haya fanyeni jambo la akili sasa. Mchakato wa kupata Katiba Mpya uanze mapema kabla ya uchaguzi ujao 2025 ili kuepusha yanayoepukika. Angalizo kwenu ni kwamba Katiba hii itakapokuja kutumia dhidi yenu hakika hakuna jiwe litakalosalia juu ya jiwe kwenye ghorofa la barafu mlilolijenga tangu uhuru hadi sasa.
Sauti ya tindo za wajenzi imezidi sauti za waombolezao. Fahamuni kwamba waliao na kusugua maogti kwa nchi hii siyo wale mnaowapandisha kwenye majukwaa yenu ya kisiasa na kiserikali wakiwaombea kwa mbwembwe na ufahari wa kufaidi juisi ya watawala.
Ni mtu wa kawaida sana tena mdogo.
Sina jipya zaidi ya kufikisha ujumbe niliousikia kwa masikio yangu mawili bila kumuona mnenaji
CC Mshana Jr
Angalizo hili linaweza likawa la mwisho yaani msipoangalia kuna dalili mbaya sana ambayo itawagharimu na kutikisa Afrika.
Kuendelea kukumbatia Katiba inayopigiwa kelele na wananchi kuwa haifai kwa mfumo wa siasa za vyama vingi, ni sawa na kulalia kitanda cha misumari huku godoro liliwa ni kipande cha gunia.
Nimeona, yes nimesikia masikioni kwangu. Inawezekana sauti hii ilikuwa kutoka upande wa pili wa ukuta ambapo sijaweza asilani kufahamu nani alikuwa mzungumzaji. Lakini sauti inasema kuwa KIPIMO KILE MLICHOWAPIMIA WENGINE NDICHO MTAKACHOPIMIWA NA KUJAZWA KWA KUFURIKA.
Katiba hii tuliyonayo sasa ambayo mnaamini ndiyo ulinzi wa Taifa letu ni Katiba inayotoa maelekezo na maagizo muhimu (japo kwa uchache) ya maongozi ya nchi hususani kwenye Haki na Wajibu. Bahati mbaya sana mmeweka pamba masikioni na kujiweka kwenye daraja la kuwa wenye akili na ufahamu kuliko raia wote wa nchi hii. Maamuzi mengi mnayoyafanya (CCM) ni kwa maslahi mapana ya chama na walioshika madaraka.
Siku hazigandi, kwa sababu baada ya kiangazi huja mvua, mvua inaweza kugharikisha na kuporomosha milima kwa nguvu itokanayo na matone ya maji yaliyojikusana sehemu moja na kusaka njia ya kupita.
Haya fanyeni jambo la akili sasa. Mchakato wa kupata Katiba Mpya uanze mapema kabla ya uchaguzi ujao 2025 ili kuepusha yanayoepukika. Angalizo kwenu ni kwamba Katiba hii itakapokuja kutumia dhidi yenu hakika hakuna jiwe litakalosalia juu ya jiwe kwenye ghorofa la barafu mlilolijenga tangu uhuru hadi sasa.
Sauti ya tindo za wajenzi imezidi sauti za waombolezao. Fahamuni kwamba waliao na kusugua maogti kwa nchi hii siyo wale mnaowapandisha kwenye majukwaa yenu ya kisiasa na kiserikali wakiwaombea kwa mbwembwe na ufahari wa kufaidi juisi ya watawala.
Ni mtu wa kawaida sana tena mdogo.
Sina jipya zaidi ya kufikisha ujumbe niliousikia kwa masikio yangu mawili bila kumuona mnenaji
CC Mshana Jr