Wazazi Wanaolalamika Wamefeli?

Wazazi Wanaolalamika Wamefeli?

bless on

JF-Expert Member
Joined
May 22, 2026
Posts
705
Reaction score
1,659
Kama wazazi wako huwa wanalalamika kuwa walijinyima sana kwa ajili yenu, basi umezaliwa na wazazi waliofeli vibaya sana. Watu hawapendi ukweli, yaani kuwaza tu hivyo wanaona tayari wanapata laana. Mtu anajinyimaje kugharamia matokeo ya furaha na starehe zake.

Watoto ni matokeo ya starehe zako, hakuna mtoto yoyote aliyeomba umzae. Halafu unakaa kabisa kumuambia mtoto eti niliuza shamba usome.

Wee shenzi nini🤣 Uza chochote aisee si ulitaka mwenyewe. Ungetuliza 'genye' unadhani huyo angekuwepo? Na wewe unahaha kwa mikopo kama mwehu kusomesha utitiri wa wadogo zako kisa eti mzazi alijinyima kwa ajili yako. Ulitaka nani ajinyime kwa ajili yako.

Watoto siyo biashara wala bima ya maisha, tunazaa tu kufurahia na siyo kuwafanya pensheni ya uzeeni. Achana na huu mtazamo uliosababisha turithishane umaskini kwenye jamii nyingi.
 
Wanufaika wakubwa wa huu muundo wa familia ni mke na watoto. Mwanaume usijinyime sana kwajili yao ukajisahau ukitegemea unafuu wa maisha badae.

Ukizeeka watamsikiliza, watawasiliana, watajali, watampa pesa mama yao kuliko wewe mwanaume. Kama uwezo wa kuwapa maisha mazuri upo, wape maisha mazuri. Kama hakuna usijinyime wape kilichopo
 
Kama wazazi wako huwa wanalalamika kuwa walijinyima sana kwa ajili yenu, basi umezaliwa na wazazi waliofeli vibaya sana. Watu hawapendi ukweli, yaani kuwaza tu hivyo wanaona tayari wanapata laana. Mtu anajinyimaje kugharamia matokeo ya furaha na starehe zake.

Watoto ni matokeo ya starehe zako, hakuna mtoto yoyote aliyeomba umzae. Halafu unakaa kabisa kumuambia mtoto eti niliuza shamba usome. Wee shenzi nini🤣 Uza chochote aisee si ulitaka mwenyewe. Ungetuliza 'genye' unadhani huyo angekuwepo? Na wewe unahaha kwa mikopo kama mwehu kusomesha utitiri wa wadogo zako kisa eti mzazi alijinyima kwa ajili yako. Ulitaka nani ajinyime kwa ajili yako.

Watoto siyo biashara wala bima ya maisha, tunazaa tu kufurahia na siyo kuwafanya pensheni ya uzeeni. Achana na huu mtazamo uliosababisha turithishane umaskini kwenye jamii nyingi.
Hahah umetuchana Sana, sema watoto ni Raha Sana lakini kwenye majukumu sasa Ni balaa
 
Maisha kusaidiana bhana


Kama kakupambania kuna umuhimu wa kumpambania na yeye

Kuna wengine wamezaliwa wakatelekezwa mpaka Leo hawana mbele wa nyuma vipi wewe uliyekuzwa na wazazi wako
 
Maisha kusaidiana bhana


Kama kakupambania kuna umuhimu wa kumpambania na yeye

Kuna wengine wamezaliwa wakatelekezwa mpaka Leo hawana mbele wa nyuma vipi wewe uliyekuzwa na wazazi wako
Sawa, Lakini kwanini mzazi asikitike au ajute kwa kitendo alichomfanyia mtoto wake ambacho kimsingi ulikuwa ni wajibu wake?
 
Kama wazazi wako huwa wanalalamika kuwa walijinyima sana kwa ajili yenu, basi umezaliwa na wazazi waliofeli vibaya sana. Watu hawapendi ukweli, yaani kuwaza tu hivyo wanaona tayari wanapata laana. Mtu anajinyimaje kugharamia matokeo ya furaha na starehe zake.

Watoto ni matokeo ya starehe zako, hakuna mtoto yoyote aliyeomba umzae. Halafu unakaa kabisa kumuambia mtoto eti niliuza shamba usome. Wee shenzi nini🤣 Uza chochote aisee si ulitaka mwenyewe. Ungetuliza 'genye' unadhani huyo angekuwepo? Na wewe unahaha kwa mikopo kama mwehu kusomesha utitiri wa wadogo zako kisa eti mzazi alijinyima kwa ajili yako. Ulitaka nani ajinyime kwa ajili yako.

Watoto siyo biashara wala bima ya maisha, tunazaa tu kufurahia na siyo kuwafanya pensheni ya uzeeni. Achana na huu mtazamo uliosababisha turithishane umaskini kwenye jamii nyingi.
Siku moja binti yangu wa pili aliniomba pesa, nikampa kidogo, akalalamika, nikamuonyesha bill nilizonazo! Alichoniambia sijakisahau mpaka leo!!!
" Aliniambia, Baba hayo ni majukumu yako, pambana", Kweli nikaongeza bidii ya kupambana.
 
Sawa, Lakini kwanini mzazi asikitike au ajute kwa kitendo alichomfanyia mtoto wake ambacho kimsingi ulikuwa ni wajibu wake?
Kujuta kunatokea pale ambapo alijitoa sana KWAAJILI yako halafu umekuwa unamuonesha dharau

Kwa mfano wewe umesema ushawahi kuzinguana na dingi wako so dingi IKABIDI akukumbushe hata wema aliokutendea ili urudi kwenye mstari Ila bro ukakaza

Sasa hapo atachaje kujuta ikiwa hela ya ada aliyotumia kukusomesha wewe kuna wengine kipindi hiko hiko walitumia kulia gambe na kutekeleza watoto wao
 
Kujuta kunatokea pale ambapo alijitoa sana KWAAJILI yako halafu umekuwa unamuonesha dharau

Kwa mfano wewe umesema ushawahi kuzinguana na dingi wako so dingi IKABIDI akukumbushe hata wema aliokutendea ili urudi kwenye mstari Ila bro ukakaza

Sasa hapo atachaje kujuta ikiwa hela ya ada aliyotumia kukusomesha wewe kuna wengine kipindi hiko hiko walitumia kulia gambe na kutekeleza watoto wao
Alitumwa kuzaa, yy ndiye anachangia huyo kiumbe kupata tabu hapa duniani ..Mnaishi kwa ujinga , usawa huu unajipa mamlaka ya kuzaa mpaka watoto wanne .

Baadaye, pesa zote zinaishia kuhudumia watoto huku ukiwa na matarajio lukuki .
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom