Sodium 23
JF-Expert Member
- Sep 17, 2013
- 471
- 484
Habari wakuu,
Ningependa kujikita moja kwa moja kwenye mada. Hii ni kwa wazazi ambao huwapeleka watoto kwenye shule zinazofanya vizuri sana kwenye matokeo kuwa makini na uamuzi huo. Japo si shule zote ila wengi wao ndio walivyo.
Ni kweli watoto wanaosoma kwenye shule hizo hufanya vizuri kihalali lakini kwa gharama klubwa ya muda wao, hisia zao na utoto wao. Hapa nazungumzia shule za msingi japo na za sekondari zinahusika kiasi chake.
Maisha ya wanafunzi kwenye shule zinanazofaulisha ni magumu sana kwa watoto. Wanapata chakula kizuri, usafiri mzuri walezi wazuri ila wanakosa mambo muhimu zaidi ya haya niliyotaja.
Wanadhulumiwa muda wa kucheza na kufurahia utoto wao. Unakuta mtoto hana muda wa kucheza michezo ya kitoto hii catch and catch, hopscotch pamoja na michezo mingine ya kumuimarisha na kumjenga mtoto badala yake anatumia muda mwingi kusoma na kufanya mitihani.
Watoto wanapata msongo wa mawazo na ndio mwanzo wa matatizo ya afya ya akili kwa sababu wanatumia muda mwingi kuwaza fimbo atakazochapwa na mwalimu au mzazi kwa kuwa hajatimiza malengo ya shule au malengo ya wazazi ya kurudi nyumbani na A.
Watoto wanapoteza vipaji vyao hawapewi muda wa kutosha kujikita kwenye vipaji vyao wanapewa kipaji kipya cha kujibu mitihani.
Watoto wankosa muda wa kutosha kupumzika, chukulia kwa mfano mtoto anaamka saa 11 anaanza kusoma anapiga bandik bandua hadi saa 3 usiku. Hapo kuna mtu kweli. Mtoto hana muda wa kudiscuss, hana muda wa kutosha damu iflow vizuri muda wote ni bandika bandua.
Mtoto wa kike anakosa muda wa kujifunza kuwa yeye, yaani mtoto wa kiume anakosa muda wa kujifunza kwa baba (majukumu ya kiume) na mtoto wa kiume anakosa nafasi ya kujifunza kwa mama (majukumu ya kike).
Tunakua na watoto ambao hawawezi kuhusiana vizuri na wenzao, wengi wanakua introvert (wanaokua peke yao tu).
Kama unaduka mtoto anakosa nafasi ata ya kujifunza namna ya kufanya biashara, mzazi umekaa tu unasubiri mtoto aje na karatasi iliyojaa A. kwenye hizo A ata humkagui kuona kama kuna umahiri kwenye kile alichojifunza.
Mwalimu anakosa muda wa kujihusisha na jamii yake anakua mbali na familia yeye ni vipindi tu ata misiba hashiriki. Yaani bandika bandua yuko darasani.
Hiki kinachofanywa na mashule siyo kibaya kwa upande wao kwa sababu wao wanafanya kile wazazi ambao ndio wateja wao wakuu wanataka.
Serikali imeliona hilo ndio maana imeondoa mfumo wa ranking ili kupunguza hii vita ya ushindani wenye kuumiza watoto na inaleta mfumo bora kabisa wa upimaji.
Ila kwa bahati mbaya muda uliotengwa kwa vipindi kama dini na michezo unatumika pia kufundisha.
Ushauri wangu:
Ningependa kujikita moja kwa moja kwenye mada. Hii ni kwa wazazi ambao huwapeleka watoto kwenye shule zinazofanya vizuri sana kwenye matokeo kuwa makini na uamuzi huo. Japo si shule zote ila wengi wao ndio walivyo.
Ni kweli watoto wanaosoma kwenye shule hizo hufanya vizuri kihalali lakini kwa gharama klubwa ya muda wao, hisia zao na utoto wao. Hapa nazungumzia shule za msingi japo na za sekondari zinahusika kiasi chake.
Maisha ya wanafunzi kwenye shule zinanazofaulisha ni magumu sana kwa watoto. Wanapata chakula kizuri, usafiri mzuri walezi wazuri ila wanakosa mambo muhimu zaidi ya haya niliyotaja.
Wanadhulumiwa muda wa kucheza na kufurahia utoto wao. Unakuta mtoto hana muda wa kucheza michezo ya kitoto hii catch and catch, hopscotch pamoja na michezo mingine ya kumuimarisha na kumjenga mtoto badala yake anatumia muda mwingi kusoma na kufanya mitihani.
Watoto wanapata msongo wa mawazo na ndio mwanzo wa matatizo ya afya ya akili kwa sababu wanatumia muda mwingi kuwaza fimbo atakazochapwa na mwalimu au mzazi kwa kuwa hajatimiza malengo ya shule au malengo ya wazazi ya kurudi nyumbani na A.
Watoto wanapoteza vipaji vyao hawapewi muda wa kutosha kujikita kwenye vipaji vyao wanapewa kipaji kipya cha kujibu mitihani.
Watoto wankosa muda wa kutosha kupumzika, chukulia kwa mfano mtoto anaamka saa 11 anaanza kusoma anapiga bandik bandua hadi saa 3 usiku. Hapo kuna mtu kweli. Mtoto hana muda wa kudiscuss, hana muda wa kutosha damu iflow vizuri muda wote ni bandika bandua.
Mtoto wa kike anakosa muda wa kujifunza kuwa yeye, yaani mtoto wa kiume anakosa muda wa kujifunza kwa baba (majukumu ya kiume) na mtoto wa kiume anakosa nafasi ya kujifunza kwa mama (majukumu ya kike).
Tunakua na watoto ambao hawawezi kuhusiana vizuri na wenzao, wengi wanakua introvert (wanaokua peke yao tu).
Kama unaduka mtoto anakosa nafasi ata ya kujifunza namna ya kufanya biashara, mzazi umekaa tu unasubiri mtoto aje na karatasi iliyojaa A. kwenye hizo A ata humkagui kuona kama kuna umahiri kwenye kile alichojifunza.
Mwalimu anakosa muda wa kujihusisha na jamii yake anakua mbali na familia yeye ni vipindi tu ata misiba hashiriki. Yaani bandika bandua yuko darasani.
Hiki kinachofanywa na mashule siyo kibaya kwa upande wao kwa sababu wao wanafanya kile wazazi ambao ndio wateja wao wakuu wanataka.
Serikali imeliona hilo ndio maana imeondoa mfumo wa ranking ili kupunguza hii vita ya ushindani wenye kuumiza watoto na inaleta mfumo bora kabisa wa upimaji.
Ila kwa bahati mbaya muda uliotengwa kwa vipindi kama dini na michezo unatumika pia kufundisha.
Ushauri wangu:
- Serikali ikaze hapo hapo ili tunusuru hawa vijana wa Kitanzania wasije kua na A ambazo haziwasaidii kwenye kupambana na maisha.
- Wazazi waache ulimbukeni wa kukimbilia shule zinazofaulisha badala yake waangalie sehemu ambako kuna chakula kizuri, ambako watoto hawasongamani, ambako idadi ya watoto ni ya wastani ili usimamizi uwe mzuri. Pia wazazi wawe tayari pale watoto wao wasipofanya vizuri waendelee kuwasaidia taratibu hiiya kuwadrill itawafanya watoto wawachukie wazazi.
- Shule ziwekeza kwenye matumizi sahihi ya muda, ratiba zifuatwe muda wa kucheza wacheze vizuri akili zichangamke.
- Kama mtizamo wa wazazi ukibadilika shule pia zitabadilika na mambo yataenda vizuri kabisa.
- Ya kwangu ni hayo nawasilisha.