Wazanzibar walianza kumiliki Runinga kabla ya Tanganyika, tutegemee maendeleo makubwa kwa Rais Samia

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,968
141,977
Katika issue ya maendeleo wazanzibar waliwahi tena ni " wajanja" kuliko Watanganyika.

Wakati sisi tunasimuliwa mambo na wanasiasa wa zama zile Wazanzibar walikuwa wanayashuhudia kwa macho Runingani.

Kadhalika katika swala la kujiamini wazanzibar wanajiamini zaidi kuliko watanganyika ndio maana Tundu Lisu alipopigwa risasi ni mzanzibari Turky aliyekodi chopa kumpeleka Nairobi hospital na hata wanaccm walioenda kumjulia hali ni Wazanzibar watupu yaani mama Samia na mstaafu Mwinyi.

Sasa basi Watanzania kwa umoja wetu tumpe ushirikiano wote Rais Samia Suluhu Hassan ili atuvushe tuifikie nchi ya asali na maziwa.

Leo tutapata mwelekeo wa serikali ya awamu ya 6 ikiwemo vipaumbele vya Rais mpya mama yetu Samia katika hotuba yake kwa taifa kupitia bunge.

Mungu mbariki Rais Samia

Mungu ibariki Tanzania

Ramadhan Kareem
 
Kwa kweli tumpe ushirikiano wote na tusimlishe maneno. Kwa Rehma zake Mola atatufikisha nchi ya ahadi.
 
Na Traffic Light za kwanza kabisa zilisimikwa Huko huko Zenjibar...!!

Mama atawale bila kikomo! Atake Asitake Tutamlazimisha!
 
Back
Top Bottom