Wazanzibar muungano tutaununua...

Wazanzibar muungano tutaununua...

Status
Not open for further replies.
Nilishasema wazi siku muungano unavunjika sherehe yangu nitatembea kwa miguu kuanzia Posta hadi kibaha maili moja!! Wazanzibar wamemtukana Baba wa taifa vya kutosha pamoja na fadhira zote alizotoa!!
 
Ndugu ukubwa wa eneo ktk nchi ama wingi wananchi si hoja madhubuti ya kuiona nchi haiwezi kujitawala.
Zipo nchi zenye wakazi chini ya milion 1 na zina utawala kamili kama nchi.
Hoja hapa Wazanzibar huu si muda wa malalamiko tu, ni wakati pia ma kuweka mikakati tunajipangaje kama nchi kua nje ya muungano?
Naamini huu moto tuliouwasha sisi kwa makele wenzetu watanganyika wanajiandaa kimyakimya.

nimekupenda hapa,inawezekana Tanganyika ikawa ndo kisiwa cha Amani
 
Ndugu zangu wazanzibar,Ni muda mrefu sasa tumekua ktk manung'uniko kwamba serikali ya Muungano(Tanganyika) wanatunyonya.

Kumekua na rai nyingi sana za kutaka mamlaka kamili ya nchi Zanzibar ili tujiendeshe kama nchi nje ya Jamhuri ya Muungano.


Wapo wazanzibar walofika mbali zaidi na kusema sasa Muungano basi.

1.Napenda niwaulize ndugu zangu wazanzibar kabla hatujapaza yowe la kuukataa muungano huu je tumejiandaaje kujiendesha kama nchi kamili nje ya Muungano.

2.Niwajuze wazanzibar wenzangu kelele na manung'uniko yetu yamewaamsha watanganyika sasa wako mbioni kupata nchi yao nje ya muungano.wao wamejipanga tayari kwa hilo.

3.Ndugu zangu wazanzibar kama tulikua tunafanya utani wenzetu wapo serious,kiuchumi,kisiasa.
Wamejiimarisha ktk nyanja nyingi muhimu kama nchi.JE sisi tumejiandaaje!

Rai yangu kwenu mdundo huu wa kuvunja muungano usituleweshe naona mwisho wake tutakuja kuwapigia magoti watanganyika turudiane kuungana.

Upepo wa mabadiko
Upepo wa kisiasa
Lazima tuangalie tuna vyuo vikuu,vyanzo vya mapato zanzibar,ajira,n.k
Malalamiko na manung'uniko yasio na tija hayafai.

Hivi kumbe kelele zote hizo watu hawajui wanakotoka wala wanapoenda?
 
Baada ya muungano kuvunjika, Pemba nao watataka kuwa nchi ili kujitenga na Unguja.
Hapo sisi watanganyika yetu macho.
Pili ni vyema ndugu zetu wa unguja na pamba wakaanza kuhamisha mali zao kwenda kwao. Ardhi mliyonunua anzeni kuiuza wakati huu mtapata bei nzuri
Mkija kuondoka kwa mtindo wa operation kimbunga, watanganyika waichukua bure

Huo wimbo wa taifa kuwa Pemba itadai kujitenga tushausikia zamani, ivyo mliambiwa na nani kama Pemba na Unguja zilikuja kuunganishwa ni huu muungano kwa hivyo ukivunjika na hizi sehemu mbili za Zanzibar zitajijenga, umesima shule ya kijiji cha ujamaa wewe rudi kibugumo kama utaweza kulima hata mahindi, ardhi.zote mumewauzia matajiri sasa mumebaki kufanya kazi za umachinga wakubwa wenu wanafanya dili za meno ya tembo na.kuuza vitalu vya madini.
Tayari mnauwana Mwanza, Arusha na Mtwara na mnapromote siasa za majimbo ukabila na dini jee sababu umevunjika.Muungano?

Wapemba walonunua ardhi na majumba na biashara kubwa kubwa Kariakoo ni sawa na wenzao Wakinga mkiwafukuza ni haki yenu lakini itabidi muwalipe kila kitu chao mnachitaka akiwache. Nchi ina sheria haiendeshwi na mbwa mwitu. Msisahau kama kuna macho ya dunia yanawaangalia.
 
wazanzibari hasa wapemba walizoe vitu vya bure, mawazo yao wanajua wakibaki wenyewe waarabu wataleta vitu kama walivyokuwa wanawatawala, wakae wakijua hii ni karne nyingine kabisa hamna cha bure,
 
Usijidanganye. Tu nchi na tutaendelea kuwa nchi. Muda ndio utakaojieleza kuwa hamko sahihi!
Pengine hukunielewa.
Najua Zanzibar ni Nchi fika, na ndivyo waZanzibari wengi wanavyotaka nadhani.

Tunachosema waTanganyika, ukiwa nchi usiwe tegemezi basi, tusiwalipie mishahara wafantyakazi wenu wala kuwalipia bili za umeme-inabidi mjitegemee.
Na ndio maana Tanganyika yetu tumesituka, tumewabeba siku nyingi mno-mjitegemee.
Tunasapoti serikali tatu ili kila nchi ijitegemee.
 
"Haa! hivi kwani kabla ya huu muungano tulikuwa tukijiendeshaje? tumetimiza miaka 50 ya uhuru na mapinduzi, hivi lengo la yote hayo tuyasalimu mamlaka yetu kwa nchi nyengine atuendeshee?

Unavyoongea ni kam Mh Nahodha, kisha anaunyemelea Urais wa Zanzibar wakati tayari hajiamini kiulinzi wala kiuchumi. Wapo wanoweza na ndio tutowaweka madarakani 2015"

na kweli mpewe nchi yenu kwa sababu mmetunyonya sisi watanganyika sana...sisi wenyewe tunaitaka sana Tanganyika yetu
 
Ni bora nionekane msaliti lakini yale ya ukweli nayasema.
Ukweli wa hili ni kama mwarobaini, ni mchungu lakini dawa.
Hivi kwanini wazanzibar wenzangu hamtaki tujikubali?
Kuna wanasiasa wameweka jambo hili kama mtego hawana dhamira njema,kama hamuamini tusubiri mengi yatakuja nje ya muungano.
 
Duh! "Ardhi si suala la Muungano" hapa ndipo watakapoumia zaidi ndugu zetu wazenji kwahiyo wenye mashamba yao na nyumba huku bara watalazimika either kuukana uzanzibari au kuachia ardhi na kwenda kujibana kwao. Nahofia sana kuzuka kwa machafuko ya kunyanyaswa wazanzibari na kufanyiwa hujuma na wabara katika Aedhi baada ya kuundwa kwa serikali tatu.
 
Ndugu zangu wazanzibar,Ni muda mrefu sasa tumekua ktk manung'uniko kwamba serikali ya Muungano(Tanganyika) wanatunyonya.

Kumekua na rai nyingi sana za kutaka mamlaka kamili ya nchi Zanzibar ili tujiendeshe kama nchi nje ya Jamhuri ya Muungano.

Wapo wazanzibar walofika mbali zaidi na kusema sasa Muungano basi.

1.Napenda niwaulize ndugu zangu wazanzibar kabla hatujapaza yowe la kuukataa muungano huu je tumejiandaaje kujiendesha kama nchi kamili nje ya Muungano.

2.Niwajuze wazanzibar wenzangu kelele na manung'uniko yetu yamewaamsha watanganyika sasa wako mbioni kupata nchi yao nje ya muungano.wao wamejipanga tayari kwa hilo.

3.Ndugu zangu wazanzibar kama tulikua tunafanya utani wenzetu wapo serious,kiuchumi,kisiasa.
Wamejiimarisha ktk nyanja nyingi muhimu kama nchi.JE sisi tumejiandaaje!

Rai yangu kwenu mdundo huu wa kuvunja muungano usituleweshe naona mwisho wake tutakuja kuwapigia magoti watanganyika turudiane kuungana.

Upepo wa mabadiko
Upepo wa kisiasa
Lazima tuangalie tuna vyuo vikuu,vyanzo vya mapato zanzibar,ajira,n.k
Malalamiko na manung'uniko yasio na tija hayafai.

pumba sana ww, ungekuwa hapa ningekunusa mdomo wk., Ivi kwani huo muungano miaka 50 sasa ni kitu gani cha muungano kimeisadia uchumi wa Zanzibar? zaidi ya kuinyonya zanzibar?
 
na kweli mpewe nchi yenu kwa sababu mmetunyonya sisi watanganyika sana...sisi wenyewe tunaitaka sana Tanganyika yetu

mgekuwa kweli munaitaka tanganyika yenu ilipotoka rasimu ya kwanza tungeona mishe mishe zenu kuondoa neno Tanzania Bara mukaweka Tanganyika. Wazanzibar ndio waliopiga kelele mpaka ikarudi tanganyika kwenye rasimu., na mpaka imetajwa kwenye rasimu hakuna mtanganyika aliyesherehekea wala kuonekana kulipokea jina la Tanganyika
 
Nilishasema wazi siku muungano unavunjika sherehe yangu nitatembea kwa miguu kuanzia Posta hadi kibaha maili moja!! Wazanzibar wamemtukana Baba wa taifa vya kutosha pamoja na fadhira zote alizotoa!!

Fadhila za baba wa taifa kwa Zanzibar ni kufanya hila na kufanikiwa kuimarisha ukiristo-ukafiri kutoka bara wakaanza kujenga makanisa na kuimba kwaya.,
 
wazanzibari hasa wapemba walizoe vitu vya bure, mawazo yao wanajua wakibaki wenyewe waarabu wataleta vitu kama walivyokuwa wanawatawala, wakae wakijua hii ni karne nyingine kabisa hamna cha bure,

huonekani kama hata elimu ya msingi ulipitia., upo upo tu iam sorry my brother, go to school baadae uje hapa upambanue mambo
 
Fadhila za baba wa taifa kwa Zanzibar ni kufanya hila na kufanikiwa kuimarisha ukiristo-ukafiri kutoka bara wakaanza kujenga makanisa na kuimba kwaya.,
Kama hujui Historia ya Zanzibar bora ukae kimya makanisa yalikuwepo kabla hata ya muungano. na huo ukafiri unaousema ndio unawapa kula bila makafili kuja zanzibar kuangalia makanisa yao hamuendi chooni wala watoto wenu hawaendi shule..Kodi za Makafili wa Tanganyika ndio zimewabeba hadi leo!! Mlikua mnabeep kuvunja muungano sasa tumewapigia subilieni katiba mpya ije tuwape notsi masaa 48 mtaondoka na vikapu vyenu kurudi pemba
 
Kama wewe ni goigoi basi bakia hukohuko Tanganyika, ila kuhusiana na Zanzibar itakuwaje hilo hatuna hofu nalo ,kama historia inajirudia basi Zanzibar ina historia ya kujitegemea na hata kufikia kutoa misaada kwa nchi za Scandnavia wakati huo,utajiri uliopo Zanzibar ambao ni m'bichi bado hata haujaguswa ni mkubwa sana sana kushinda maelezo ,waulize wanaoulinda muungano kwa nguvu zao zote wanaweza kukupatia jibu.

Zanzibar raia wasio na ajira watalipwa kila mwezi ,dogo hilo? Sasa fikiria hilo tu ,huko Tanganyika wataliweza ? Muungano na ufe halafu tuone kama atakufa njaa mtu ,nyie vipi ? usifikiri Zanzibar hakuna dhahabu,usifikiri ZANZIBAR hakuna almasi,usifikiri hakuna uranium ,vyote hivyo vipo na vya uhakika mbali ya black gold (mafuta). mpoooo?
 
mgekuwa kweli munaitaka tanganyika yenu ilipotoka rasimu ya kwanza tungeona mishe mishe zenu kuondoa neno Tanzania Bara mukaweka Tanganyika. Wazanzibar ndio waliopiga kelele mpaka ikarudi tanganyika kwenye rasimu., na mpaka imetajwa kwenye rasimu hakuna mtanganyika aliyesherehekea wala kuonekana kulipokea jina la Tanganyika

Naona kuna jambo unashindwa kuelewa!Kurudisha neno 'Tanganyika' badala ya 'Tanzania Bara' ni mwanzo wa kuvunja muungano,na rasimu ilikuwa inajaribu kuliepuka hilo!Au umesahau kuwa waliopewa jukumu la kuunda tume hiyo ni wasomi waliobobea?

Mna kazi!


Usizungumze jambo ambalo hulijui!
 
Fadhila za baba wa taifa kwa Zanzibar ni kufanya hila na kufanikiwa kuimarisha ukiristo-ukafiri kutoka bara wakaanza kujenga makanisa na kuimba kwaya.,

Katika fikra za watu kama hawa,naiona Zanzibar ya wamwagiaji tindikali,magaidi na maswahiba wa Alshabaab na Alqaida.

What a waste!!!
 
Siamini kama wee in Mzanzibar kweli...hayo maswali yako hayaana uzito hata kidogo ktk wala daima hatutayafikiria maana Wazanzibar tuliweza na tutaweza...
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom