Hapo kwenye bluu; let's be serious, Muungano ulizaliwa not more than three months baada ya Mapinduzi. Hii inamaanisha kwamba Zanzibar iliwahi kusimama yenyewe kama taifa huru (nje ya Muungano) kwa kipindi kisichozidi miezi mitatu tu! Kabla ya hapo Mamlaka ya Zanzibar yalikuwa chini ya Mkoloni (mwarabu) tangu 1840 - 12th Jan. 1964 yaani kwa miaka 124.
Hivyo, kusema kwamba "kabla ya muungano" Zanzibar iliishije; jibu ni rahisi; YALIKUWA MAISHA YA UKOLONI WA KIARABU, labda ndio aina ya maisha wengine mnayotamani kuishi. Vinginevyo nakubaliana na mleta mada kwamba nje ya Muungano Zanzibar inatakiwa "kuanza upya" kwani kabla ya hapo Zanzibar kama taifa huru "haikuwahi kuwa na chochote" na sio kutuletea majibu mepesi na ya kijinga eti "kabla ya muungano ilikuwaje" kana kwamba Muungano ulikuja muda mrefu baada ya Zanzibar kuwa taifa huru!
MKOLONI MWARABU? Mulipokwisha kupindua mkauza nchi kwa Tanganyika na bado mpaka leo mnalalamika na Mwarabu ukiwacha Mzee Karume kwani hao viongozi wa SMZ walisoma katika serikali ya nani hata wakafika Makerere na Oxford? Je kwanini baada ya hapo for the last 50 years wameshindwa kubadilisha maisha ya mwananchi wa kawaida yakawa bora kuliko yalivyokuwa wakati wa 'Mkoloni Mwarabu'
Huko Ngambo mpaka ukifika mashamba majumba ya watu binafsi ni yale yale tokea kabla ya mapinduzi ukiona majumba mapya ya kisasa basi ama ni ya wafanya biashara au mafisa wa ngazi za juu serikalini au ya Wazanzibari walioko nje.
Na hao wafanya Biashara ni wachache nao watu aina tatu mostly Wenye asili ya Kihindi, Waarabu au Wapemba na siku hizi Wazungu. Biashara kubwa kubwa zina wapemba, waarabu na wageni.
Na kwanini Serikali zote mbili zinategemea mikopo na misaada kutoka nje na hali zimerithi utajiri wa mali za asilia na akiba kubwa ya fedha za nje.
Kwani basi Serikali zote mbili zinaenda Arabuni kuomba misaada. Au Baniani mbaya Kiatu Chake Dawa?
Hivi karibuni Oman imewapa scholarship wanafunzi wengi wa Zanzibar nafasi za kusoma nje. Imeahidi kujenga Bandari ya Mtwara kwa kukidhi mahitaji ya kuendeleza biashara ya gesi asilia amabayo itawafaa wananchi wa Tanganyika zaidi. Juzi tu serikali ya Oman imetoa Dola za Marekani milioni 700 kujenga Chuo na Msikiti mkubwa kabisa katika EA.
Serikali ya Oman imetoa misaada mingi tu kusaidia Zanzibar.
Kwanini mwaka 2005 wagombea 11wa Urais wa SMZ walienda Oman kuomba msaada wa fedha za Kampeni?
Muingereza kwenu si Mkoloni au ndio Bwana mnaempenda?
Watoto wengi wa the so called wana mapinduzi wako nje hasa UK, Canada, Scandinavia na US wamejiripuwa as wasomali na sasa wamepata uraia wa nchi hizo na wamepata kusoma mpaka elimu ya juu kwanini SMZ imeshindwa kuwatunza baada ya vifo vya wazee wao?
KWANINI MAJUMBA YA MICHENZANI SASA YANAKALIWA NA MATAJIRI BADILI YA WALE WALALAHOI WALIOLENGWA NA.SERIKAL BAADA YA MAPINDUZI?