Wazanzibar muungano tutaununua...

Wazanzibar muungano tutaununua...

Status
Not open for further replies.
Ndugu zangu ambao si wazanzibar mnaochangia uzi huu tafadhalini nawaomba kwa lugha laini mnisaidie kuwaelimisha wazanzibar wenzangu umuhimu wa huu Muungano tulionao kwetu sisi kama wazanzibar pia kama nchi.

Kenge hasikii hadi atokwe damu masikioni! Hawa kwa ufedhuli na lugha zao chafu ni zaidi ya kenge; hawastahili kubeleza tena Mkuu.
 
Ni kweli, miezi miwili na nusu ya uhuru ilikuwa ngumu sana kwa marehemu Karume kushikilia dola ya visiwa viwili kama nchi moja - alishalemewa sana na hatari ya vita vya wenyewe kwa wenyewe - kama historia inavyoonesha. Lakini kwa sasa mazingira ni tofauti na wakati ule tulipohitaji msaada wa Watanganyika ili kuepuka balaa baada ya Mapinduzi matukufu. Sasa tunaweza kabisa kujisimamia kama nchi. Historia imebadilika, watu wamebadilika, mazingira ya ki-dunia yamebadilika. Tunawashukuru Wabara kwa kupita nasi kipindi kile kigumu, lakini shukrani na heshima hii itapungua na kubadilika iwapo mtaendelea kufikiri mtoto akishakua anahitaji tena kutunzwa na kusimamiwa na mzazi. Mzazi mwenye busara humpa mtoto heshima na uhuru wa kujitawala muda unapofika kufanya hivyo!

Haijawahikutokea wakati ambao labda visiwa viwili vya Zanzibar kuwa na uhusiano wa mashaka kama baada ya kuingia kwa CCM .
Suala la kulelewa na Bara halipo kwani tulipokuwa huru tulikuwa na maendeleo na sasa hayo maendeleo yaliletwa na huo ulezi yako wapi?
Tunahitaji kuwa huru tena na tuanze upya ili turudi kule tulikokuwepo kabla ya CCM kuttawala!
 
huu ni ujinga au nini? hivi tanganyika kabla haijapata Uhuru ilikuwa inaishi vipi? ilikuwa nanini? anzibar ilikuwa bora. Tanganyika iweze pamoja na kututawala Zanzibar isiweze kujitawala. Kasumba.
Uelewe Zanzibar ilipata Uhuru wake kutoka Mwingereza (rejea) kutoka mwingereza na siku ya Uhuru zanzibar ilisita kuwa Protectorate kama Kwa Tanganyika kuwa kolon lake

KLabla ya uhuru kulikuwa na vyama vikipigania Uhuru na katika hivyo vilituonya kama tuta fursa kutawala Zanzibar watatuuza kwa Tanganyika. na haya ndio yaliotokea. Kama ASP walikuwa haawezi kutawala Zanzibar kwa nini walipindua? Si wangemwachia Mohammed Shamte kuiongoza nchi. Kutuwaambia kuwa Zanzibar hatuwezi kuendesha nchi yetu ni tusi. Ni tusi kwa Mapinduzi na tusi kwa waasisi wa ASP na hasa Shirazi Association. Kumbukuka kuwa Shirazi Association ni chama cha akina Thabit Kombo,ameir Tajo na mohd Shamte

Ndugu yangu shika points"
Hapa wazanzibar tunaimba wimbo mmoja wa kuachana muungano lakini kule juu viongozi wa Zanzibar kila mmoja ana kibwagizo chake.
Ni kiongozi yupi ambae ana kuja na maelezo nchi itaendeshwaje kiuchumi baada ya kujitoa ktk muungano?
 
serekali y zanziabar ikiamuwa inaweza kusomesha watu ulaya mashariki na china na ikawa rahisi kuliko hapomtanganyika
 
Ni lini Zanzibar ilitangaza kutohitaji misaada ya kigeni Mkuu? Hebu acha upotoshaji; Zanzibar yenyewe ni tegemezi kwa Tanganyika kwa asilimia kubwa kuanzia ulinzi na mambo mengine kupitia mwamvuli wa muungano. Sijui nyuma unayoizungumzia wewe ni ipi au lini.

Sishangaii wewe kushangaa hayo! Umtoto mdogo usiejuwa lolote kuhusu Zanzibar unaongozwa na chuki na dharau, laiti ungewauliza wakubwa zako usingebisha.
Nikiupe kubwa nyengine basi! Zanzibar ilikuwa mbele kutowa misaada kwa nchi za Afrika Mashaariki kama Kenya.

Ukweli utabaki ukweli na usitafute mengi pengine hao Wazanzibari unaowadharau ndio waliokufundisha mengi tu.
 
Ndoa haiwi ndoa bila tendo la ndoa. Gubu likizidi hamu ya tendo la ndoa inakwisha hivyo dhana nzima ya ndoa inapotea hivyo ndoa haipo tena. Hivyo, kwa ufupi hakuna chochote Tanganyika inachofaidika nacho kutokana na Muungano hata hiyo ndoa uliyotaka kutuaminisha haipo! Nitajie hata jambo moja ambalo Tanganyika inafaidika nalo kutokana Zanzibar.

Kutawala! Ili mjilabu!
 
Na wanavyozaliana ovyo kwenye kale ka nchi sijui wataishije warudi tu kwao kwa kweli.
 
Hicho kifaru kimoja sijui hata kama wanajua bei yake sembuse huo utitiri wa magari ya deraya na madege ya kijeshi. Sijui kama wanajua thamani ya kisiwa cha Witu na Chumbwini kwa pamoja hununui kifaru! Jasho la mTanganyika hilo linatumika ndivyo sivyo!

Nimekwambia wewe hujui kitu kuhusu mambo ya muungano huu? Kawaulize wakubwa zako vita vya Iddi Amini vifaa zilipatikana wapi?
 
Ndio hivyo inaonekana wanaomba wasichokijua.

Maana mpaka gwaride litapigwa na Watanganyika........


Pengine kuthibitisha kuwa hakuna cha maana kwa muungano huu! Yaani vifaru vya maonyesho na baadae virudi vinakohitajika. Hatuhitaji vifaru kwani hatuna wa kujilinda dhidi yake!
 
"Haa! hivi kwani kabla ya huu muungano tulikuwa tukijiendeshaje? tumetimiza miaka 50 ya uhuru na mapinduzi, hivi lengo la yote hayo tuyasalimu mamlaka yetu kwa nchi nyengine atuendeshee?

Unavyoongea ni kam Mh Nahodha, kisha anaunyemelea Urais wa Zanzibar wakati tayari hajiamini kiulinzi wala kiuchumi. Wapo wanoweza na ndio tutowaweka madarakani 2015"


Miaka 50 unaihesabu namna gani wakati karibia miaka 50 uko ndani ya muungano ndugu! Watakapojitoa watanganyika utaanza kuamini hayo maoni ya Makamee.
Halafu sijatambua vigezo gani unatumia kumtaja mleta mada kama ni Nahodha, kama ni ubashiri hebu wataje na wachangiaji wengine.
 
Hii ni changamoto kwa pande zote mbili lakini kwa Zanzibar na Wazanzibari ni zaidi.

Katika Political Islam wanazuoni wanatutanabahishia aina mbili za reactions ambazo Muislamu anatakiwa daima azizingatie katika mapinduzi.

Aina ya kwanza na pale wakati wa kutokea tukio, na ya pili ni baada ya tukio.

Mfano wa siku za karibuni ni Somalia na Iraq: (Wazanzibari wachukue hili kuwa ni fundisho ili yasije yakawakuta yaliyoyakuta Somalia na Iraq).Allah aepushilie mbali.

Siad Barre alikuwa ni dhalimu na alipoondoka Wasomali walifurahia (hii ni reaction ya kwanza pale tukio linapotokea) na ni nature ya mwanadamu, sasa angalia reaction ya pili; muulize Msomali leo wakati wa Barre na sasa hivi ni upi bora? wengi watakwambia bora Barre! pamoja na udhalimu wake tulikuwa na amani, tulikuwa tukiweza kutoka nje ya nyumba zetu na kwenda kutafuta rizki, tulikuwa, tulikuwa tulikuwa.

Ukija Iraq; Saddam Hussein naye alikuwa dhalimu na alipoondolewa Wa-Iraq walifurahi lakini waulize sasa hivi; mnauonaje wakati wa saddam na leo? wengi watakwambia ni bora wakati wa Saddam pamoja na udhalimu wake lakini tulikuwa na utulivu , tulikuwa tukiwapeleka watoto wetu shule bila ya wasiwasi, tulikuwa tukihudhuria swala za jamaa Misikitini...

Yote haya inaonyesha kuwa Somalia na Iraq walikuwa hawajajitayarisha na maisha bila ya Barre na Saddam!
Kwa Zanzibar bado hawajachelewa nafasi ya kujiandaa na maisha bila ya Tanganyika ipo, waanze kujipanga sasa.

Watanganyika nao wanaweza kusaidia kwa kuwaachia Wazanzibari wenyewe bila ya kuwaingilia katika mambo yao, kuchafuka kwa Zanzibar hakuna faida yoyote kwa Tanganyika kama nchi.

*Bado ninashikilia maoni yangu kuwa muungano uvunjwe haraka iwezekanavyo! kila la kheri Zanzibar.
 
Mleta hii thread sijui alikuw amekaa sehemu gani lakini nataka nimkosoe hapo anaposema "tutaununua" namwambia Muungano hauuzwi dukani wala sokoni.
Ukiisha vunjika baasi. Tanganyika sasa wamejua kumbe Wazenji hawana shukrani kabisa. Tumewabeba mgongoni kwa mbeleko, tumewastahi hata pale mlipo taapikia mabegani mwetu. Sasa mnaleta jeuri?? Ama kweli hii ni ndama jeuri. Mfugaji yeyote anajua, ukiinywesha ndama maziwa mengi, hukuburuta chini uendapo kuifunga.
Zanziba haitoshi wilaya ya Temeke, haikuwa na chochote ila karafuu, leo kwa fedha yetu mnajitafutia mafuta, kuona dalili tu tayari mmejiona Quatar? Ama kweli, masikini akipata... hulia mbwataa.
Nendeni zenu tu, ila muwangojee hao waliojipatia mashamba na viwanja na vijibiashara huku bara. Sio utani, siku nikishika dola, hao ndio wa kwanza kufukuza huku kwetu. Tena waache hapa vyote. Mwl. aliwapa nini walowezi? Mugabe aliwapa nini? Tegemeeni hayo hayo mkakamuane huko huko


Mnakaribishwa kuirejesha Tanganyika yenu baada ya kukumbushwa kuwa mtu chake!
 
hawa kina makame hata siwaelewi wanachotaka

Kweli kabisaa!
Mpu.uzi kama Makame hauwezi kumuelewa!
...
Ni mbaya sana kuona Mwanaume hajiamini na hayuko pamoja na wenzie kuvunja chawa!
...
Hizo hoja zake za kipu.uzi hazina mashiko yoyote!
Labda Makame nikuulize:
kwa mujibu wa maelezo yako, Zanzibar isingeungana na Tanganyika mwaka 1964 kusingekua na raia wa wazanzibar?
Si ndio! Wote wangekufa na ukame! Si ndio?
...
Hao Watanganyika wamejipanga kwa lipi?
Kama wamejipanga nini kinawafanya wang'ang'anie Muungano?
...
Hivi ili Zanzibar iendelee ni lazima iungane na Tanganyika?
...
Nakuomba Makame unijibu maswali yangu!
...
Nimeskitika kuona Mzanzibari anafikiri kama kalewa, wakati ulevi si tamaduni yetu!
 
Ndugu zangu wazanzibar,Ni muda mrefu sasa tumekua ktk manung'uniko kwamba serikali ya Muungano(Tanganyika) wanatunyonya.

Kumekua na rai nyingi sana za kutaka mamlaka kamili ya nchi Zanzibar ili tujiendeshe kama nchi nje ya Jamhuri ya Muungano.

Wapo wazanzibar walofika mbali zaidi na kusema sasa Muungano basi.

1.Napenda niwaulize ndugu zangu wazanzibar kabla hatujapaza yowe la kuukataa muungano huu je tumejiandaaje kujiendesha kama nchi kamili nje ya Muungano.

2.Niwajuze wazanzibar wenzangu kelele na manung'uniko yetu yamewaamsha watanganyika sasa wako mbioni kupata nchi yao nje ya muungano.wao wamejipanga tayari kwa hilo.

3.Ndugu zangu wazanzibar kama tulikua tunafanya utani wenzetu wapo serious,kiuchumi,kisiasa.
Wamejiimarisha ktk nyanja nyingi muhimu kama nchi.JE sisi tumejiandaaje!

Rai yangu kwenu mdundo huu wa kuvunja muungano usituleweshe naona mwisho wake tutakuja kuwapigia magoti watanganyika turudiane kuungana.

Upepo wa mabadiko
Upepo wa kisiasa
Lazima tuangalie tuna vyuo vikuu,vyanzo vya mapato zanzibar,ajira,n.k
Malalamiko na manung'uniko yasio na tija hayafai.

Enhe hebu nipe story kidogo, KISONGE pale mnakuwa mnalipwa ngapi? Mana naskia wenzenu lumumba wanalipwa buku 7 nyie ngapi? Maana maskani yenu pale kwa mipasho, kama Khadija Kopa.

1- Zanzibar haina haja ya kujiandaa kuiendesha nchi yake, tangu muungano unaanza visiwa ivi vinaserikali, sasa sijui kujiandaa vipi na sijui nani anatakiwa kujianadaa kati ya mwenye serikali na alokuwa hana ata wizara!

2- eti kelele zetu zimewaamsha watanganyika, labda zimewaamsha wana jf, sijasikiapo maandamano Bara wakidai nchi yao, naona maneno JF tu vitendo Zero. Kisha kauli ya watanganyika wapo mbioni kupata nchi yao, sio sahih, ulitakiwa useme wazanzibari wapo mbioni kutaka nchi yao, wao ndio walioamka, na wakawaamsha hao wenzako, wazanzibar ndio wanaodai nchi huru mpaka ndani wakawekwa, kwaiyo unatakiwa useme znz ipo njiani kupata uhuru wake!

3- wamejiimarisha vipi kiuchumi, kisiasa ata useme wapo serious? Siasa zenyewe sasa ivi zishachafuka, 2015 apo pana kumwagika damu, sisi tumeacha upuuzi wa kumwagana damu tulipoleta serikali ya mseto, tumepiga hatua, sasa wenzetu wanarudi nyuma, wakipigana mabomu mikutanoni, wakitukanana, sasa sijui nani wapo serious. Ukisema uchumi itabidi nikushangae, haya userious wao uko wapi? Tanzania ni ya kuwa maskini kweli? Almasi, dhahabu, tanzanite, gesi, maliasili tele kisha uchumi bado mbovu, na bado wanayataka mafuta ya zanzibar, heh, hii nchi kama ina laana vile, sasa sijui wameimarisha vipi, na obstacle kwa zanzibar kuendelea ni huu muungano hasa, kwamba kila kitu kimefanywa cha muungano. Habari ndo hiyo, haya kachukua chaki ukaandike ubaoni kwenu mipasho yenu.
 
Katiba mpya imetoka na neno Tanganyika sasa mnasuasua, mmeona we mean business.

Well, too late now, we've had this conversation for eons, not anymore, just go your merry way, please, tumechoka kuwabeba, to hell na Zanzibar yenu.

Kaanzisheni Taifa lenu, mjiunge IOC, mpitishe sheria za uhamiaji za kudhibiti Watanganyika kuingia Zanzibar ku corrupt the moral values of Zanzibari children na kuchukua kazi zenu kwenye utalii, mpitishe sheria za kupiga marufuku kuuza na kunywa pombe, kuvaa vimini, milegezo, bikini na jeans, ili kusiwe na haja ya kumwagiana tindikali kwa ajili ya mavazi.

To hell with that good-for-nothing, grungy little island.

tehe hee. Kubeba bunduki kuuwa mbu? To hell with your bully giantness !
 
Ndugu zangu ambao si wazanzibar mnaochangia uzi huu tafadhalini nawaomba kwa lugha laini mnisaidie kuwaelimisha wazanzibar wenzangu umuhimu wa huu Muungano tulionao kwetu sisi kama wazanzibar pia kama nchi.

Kama undani ya familia basi mzazi wetu kazaa mtoto si ..........!
 
Ndugu zangu wazanzibar,Ni muda mrefu sasa tumekua ktk manung'uniko kwamba serikali ya Muungano(Tanganyika) wanatunyonya.

Kumekua na rai nyingi sana za kutaka mamlaka kamili ya nchi Zanzibar ili tujiendeshe kama nchi nje ya Jamhuri ya Muungano.

Wapo wazanzibar walofika mbali zaidi na kusema sasa Muungano basi.

1.Napenda niwaulize ndugu zangu wazanzibar kabla hatujapaza yowe la kuukataa muungano huu je tumejiandaaje kujiendesha kama nchi kamili nje ya Muungano.

2.Niwajuze wazanzibar wenzangu kelele na manung'uniko yetu yamewaamsha watanganyika sasa wako mbioni kupata nchi yao nje ya muungano.wao wamejipanga tayari kwa hilo.

3.Ndugu zangu wazanzibar kama tulikua tunafanya utani wenzetu wapo serious,kiuchumi,kisiasa.
Wamejiimarisha ktk nyanja nyingi muhimu kama nchi.JE sisi tumejiandaaje!

Rai yangu kwenu mdundo huu wa kuvunja muungano usituleweshe naona mwisho wake tutakuja kuwapigia magoti watanganyika turudiane kuungana.

Upepo wa mabadiko
Upepo wa kisiasa
Lazima tuangalie tuna vyuo vikuu,vyanzo vya mapato zanzibar,ajira,n.k
Malalamiko na manung'uniko yasio na tija hayafai.

Nakuona itakua hukufanya tathimini vizur, iwe sisi Waznz tumewaamsha watanganyika waliokua wakishindwa hata kuidai Tanganyika yao iwe bora wao walikwisha jipanga, au wanataka kujipanga sasa.

Na ukizungumza kuhusu uchumi wa Tanganyika ndo ni kichekesho zaid, hakuna barabara za uhakika, umeme wa uhakika, afya ndio usiseme, hebu tuambie usibabaishe watu nani ataanza kujipanga?

Zanziba ikijitoa Leo itakuwa ni wenyeji na Tanganyika ndo mgeni wetu.
 
1- Zanzibar haina haja ya kujiandaa kuiendesha nchi yake, tangu muungano unaanza visiwa ivi vinaserikali, sasa sijui kujiandaa vipi na sijui nani anatakiwa kujianadaa kati ya mwenye serikali na alokuwa hana ata wizara!
Usibweteke!
Serikali iliyopo ni katika muundo wa muungano wa serikali mbili, zikipita serikali tatu au muungano kuvunjika basi serikali ya Zanzibar itakumbana na aina nyingine za changamoto.

Jitayarisheni.

*BTW nipo neutral katika hili suala kwa sababu serikali zote mbili ni za kisekula wakati mimi ninazitambua Shariah za Allah pekee.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom