Ngwananzengo
JF-Expert Member
- Jul 28, 2012
- 1,911
- 1,322
Kuna kijana yeye ni jirani yangu na ni injinia.
Kapanga mwaka kesho atavuta jiko.
Kwa unyenyekevu mkubwa alimfuata mjomba wake kwa ushauri.
Pamoja na Mengi aliyoshauriwa aliambiwa kama huyo binti familia yake wameokoka basi amchunguze kwa umakini kwani sehemu hii imekuwa kichaka cha kuficha waovu.
Baada ya kupewa ushauri huo alikuja kunipa taarifa kwa kuniambia, "inashangaza mawazo yako yamekuwa na mlengo sawa na mjomba wangu".
Binafsi nimekuwa nikijipambanua kutokuwa upande wa wale wote wanaojifanya kuzishika "IMANI" za dini barabara.
Tafsiri yangu huu ni sawa na ulevi mwingine kwa maana hiyo ni vizuri tahadhari ikachukuliwa.
Nimefarijika kuona kumbe Kuna wengine wenye fikra kama zangu.
Kapanga mwaka kesho atavuta jiko.
Kwa unyenyekevu mkubwa alimfuata mjomba wake kwa ushauri.
Pamoja na Mengi aliyoshauriwa aliambiwa kama huyo binti familia yake wameokoka basi amchunguze kwa umakini kwani sehemu hii imekuwa kichaka cha kuficha waovu.
Baada ya kupewa ushauri huo alikuja kunipa taarifa kwa kuniambia, "inashangaza mawazo yako yamekuwa na mlengo sawa na mjomba wangu".
Binafsi nimekuwa nikijipambanua kutokuwa upande wa wale wote wanaojifanya kuzishika "IMANI" za dini barabara.
Tafsiri yangu huu ni sawa na ulevi mwingine kwa maana hiyo ni vizuri tahadhari ikachukuliwa.
Nimefarijika kuona kumbe Kuna wengine wenye fikra kama zangu.