Mgodi wa tulawaka na resolute muda wao ulishakwisha kipindi cha kuvuna dhahabu sasa hivi wanakuambia wanamalizia malizia tu masalia.
Mfano mgodi wa tulawaka ulikuwa unategemea udumu kwa miaka mitano tu na usifikiri hao jamaa wanaondoka kwa sababu za kisiasa wameshaona kuwa siku za karibuni hawatakuwa wanapata tena dhahabu nyingi kama walivyokuwa wanazipata kupitia migodi hiyo na ndio wanaamua kuuza hisa kwenye hiyo migodi.
Migodi mingine kama GGM au KMCL ya kakola na NorthMara, bado wanavuna dhahabu za kutosha huko na kamwe hawawezi kuuza au kuondoka, chunguza vizuri kwenye hiyo migodi wanayoondoka production imeshuka sana sasa hivi na target yao ilishatimia siku nyingi.
Kitu ambacho kinawaondoa hawa jamaa, kama ni kweli nadhani ni suala la kodi. Hawataki kabisa kulipa kodi. Huu ni wizi kwa nchi yetu.