Wavulana mna matatizo gani??

Wavulana mna matatizo gani??

Yaani naona uvivu hata kuwaza. Ila wanaume wa siku hizi wamekuwa hopeless kama role models wao (baba zao). Kama kijana amekua akimsikia mamake akilalamika kuhenya na ada, chakula and everything while baba anakula na kutoka kama mzingani? Majuzi nililalamikiwa na shosti kuhusu mumewe nikamjambia kazi yako ni kuua hii chain. Mumeo yuko kama babake. Make sure your son comes out differently.

Wababa wa jf, mmekuwaje role models kwa watoto wenu wote wa kike na wa kiume? Unamdharau mkeo, na bintiyo ataona sawa kudharauliwa na bf wake na huku kijana wako akiona ni sawa kumdharau mwanamke. Mna kesi ngumu sana ya kujibu

Unasemaaaa????????????
 
Bujibuji juzi alileta uzi juu ya kijana mmoja asie na haya....eti anaenda kaa kwa dada yake anayemegwa na mshkaji,,si wachumba na hawajaona,
dogo wa sister anaenda kaa kushuhudia dada yake akila mpini.

Huo ni mfano na iko mingi.. Ifike mahali wazazi wawashauri vijana maisha ya kwenye tamthilia wayaache hukohuko,...

Nikiwa na toto la namna hiyo yaani nitajihisi mwenye mkosi wa kutisha....

Mwanamume uwe hivyo kweli na useme kwamba wewe ni mwanamume???

I love my old days....

Babu DC!!
 
Hivi mtoto kulelewa na mama vibaya?

Hakuna aliyesema kuwa ni vibaya
Hata huyo uliyem quote hajasema hivyo

Kuna mambo ambayo kijana hatakiwi kuongozana na mama yake kia wakati
Mtoto wa kiume yuko darasa la tano lakini analilia kwenda sokoni na mama yake...!!!!
Kama hiyoi sio laana basi itakuwa ni zaidi ya laana

Na wewe mama kama unaona sawa utakuwa na mpango wa kifedhuli kwa huyo mtoto wako!!
 
yeh teh teh uzi mtamu sana huu... last wiki nilikutana na kavulana kakangu mkubwa analia nae nikamwambia uje kwangu ukiwa mwanaume sio wakiume ndio tuongee!
 
Na hizo haki zao ziishie huko huko!!!!!!!


Kweli mkuu,

Hivi mtu utajisikiaje ukikuta toto lako liko linachezewa na kabinti pale mtaani kwako??

You feel like ukalinyonge....

Enzi zetu baba akibahatisha kukuona unamwaga sera kwa kibinti cha jirani yenu anakimbia nyumbani kumsimulia mke wake na kutamba alivyotema cheche kwa kuleta kidume duniani....

Yaani wazazi wa vitoto vya leo wamebeba majanga matupu aisee....

Babu DC!!
 
Siku hizi ulegevu wameupa jina wanaita sharobalo sasa unategemea nini. Kijana hajiwezi hata kunyanyua ndoo ya maji. Malezi yanachangia kwa kiasi kikubwa sana tumemodenaizi kila kitu kiasi kwamba mengine hata wazungu hawayafanyi. Hushangai mtoto wa kiume anaamka saa mbili na baada ya hapo yuko fb habari hapati , hajiwezi hata kuchukua jembe aondoe majani machache yaliyoko uwanjani anangoja dada wa kazi afanye hayo. Huko mbele watapigwa mpaka makofi hawa.
 
Hakuna aliyesema kuwa ni vibaya
Hata huyo uliyem quote hajasema hivyo

Kuna mambo ambayo kijana hatakiwi kuongozana na mama yake kia wakati
Mtoto wa kiume yuko darasa la tano lakini analilia kwenda sokoni na mama yake...!!!!
Kama hiyoi sio laana basi itakuwa ni zaidi ya laana

Na wewe mama kama unaona sawa utakuwa na mpango wa kifedhuli kwa huyo mtoto wako!!

Tunahitaki kubalance information mkuu.....

Hata enzi zetu tulitumwa sana sokoni...ila tulienda na wazee wetu ili tukajifunze kubargain badala ya kwenda kuomba vitu kama zile story za kwenye wimbo wa mpemba....

Kwa hiyo, watoto wa kiume wanaweza kufanya kazi za aina zote (mimi sijui kama kuna kitu sikifahamu) ila wafanye katika misingi ya kidume dume....

Siyo toto la kiume nalo linataka kukaangiza limekaa kwenye kigoda....

Babu DC!!
 
Alaaaaaa!hao ke wanaolalamika wako wapi ?yaani nawatafuta sana ,ma"SIMBA" bado tupo hapa
 
Tunahitaki kubalance information mkuu.....

Hata enzi zetu tulitumwa sana sokoni...ila tulienda na wazee wetu ili tukajifunze kubargain badala ya kwenda kuomba vitu kama zile story za kwenye wimbo wa mpemba....

Kwa hiyo, watoto wa kiume wanaweza kufanya kazi za aina zote (mimi sijui kama kuna kitu sikifahamu) ila wafanye katika misingi ya kidume dume....

Siyo toto la kiume nalo linataka kukaangiza limekaa kwenye kigoda....

Babu DC!!

Ni kweli mkuu

Ndio maana nikasema kuwa kwenda sokoni na akina mama mwishowe itakuja kuwa tabu

Kwenda sokoni ni sawa lakini wanakwendaje ndio suala!
 
Siku hizi ulegevu wameupa jina wanaita sharobalo sasa unategemea nini. Kijana hajiwezi hata kunyanyua ndoo ya maji. Malezi yanachangia kwa kiasi kikubwa sana tumemodenaizi kila kitu kiasi kwamba mengine hata wazungu hawayafanyi. Hushangai mtoto wa kiume anaamka saa mbili na baada ya hapo yuko fb habari hapati , hajiwezi hata kuchukua jembe aondoe majani machache yaliyoko uwanjani anangoja dada wa kazi afanye hayo. Huko mbele watapigwa mpaka makofi hawa.

"Where is no vision people perish"
 
Kweli mkuu,

Hivi mtu utajisikiaje ukikuta toto lako liko linachezewa na kabinti pale mtaani kwako??

You feel like ukalinyonge....

Enzi zetu baba akibahatisha kukuona unamwaga sera kwa kibinti cha jirani yenu anakimbia nyumbani kumsimulia mke wake na kutamba alivyotema cheche kwa kuleta kidume duniani....

Yaani wazazi wa vitoto vya leo wamebeba majanga matupu aisee....

Babu DC!!

Kwanza mtoto wa kiume hadi akakwaruzane na vibinti mtaani atakuwa anatafuta nini huko kwa hivyo vibinti?
Nikikuta ameshikana mashati na vivulana vyenzie hapo nitafarijika kuwa nami nina kidume lakini nimkute na vibinti wallah lazima nitafute adhabu ambayo hataisahau kabisa!!!!!!!!!!!!!!
 
Shikamoo Serikali...
Zamani zetu wakati mzee wetu mchonga meno akiwa le Prezidaa tulikuwa tunalelewa kiukakamavu sana...nakumbuka kauli mbiu ya bi mkubwa wangu enzi hizo,kwamba utatambua jinsia yako once ukiwa unakoga tu,kwake hakuwa na mtoto mayai!

Nakumbuka enzi hizo almost kila jioni kwenye seek and hide almaarufu kama Kombolela,hapo hata bint awe na shingo ngumu vipi lazima aingie kingi tu...but look...what the've done! Wewe dada unayejifanya wa kisasa,daily kumsifia mwanao wa kiume kwamba amekufanana,na unadiriki hata kwenda one step ahead kwa kumsifia umahiri wake wa kutikisa wesere kama wewe....ptuuuuuh! eti ohh em mwangalieni mwanagu shingo imekatika kama yangu! Na kila mara unamkokota kukusindikiza saluni utadhani mtaani hakuna watoto wa rika lake acheze nao! Hivi kesho ukamkuta anakatikia viuno wanaume wenzie utamlaumu?

Kwa muktadha huu,hii sera ya wavulana kuolewa na wanaume wenzao naona miaka ya usoni itatimia tu...ngojea! Juzi kati mvulana mmoja 'jina linahifadhiwa' almanusura ajikwae akikimbilia duka la dawa kisa kila GF wake akija kwao analegeza macho na kuwa mlegevu,kwa kuwa yeye si expert kwenye haya makitu akadhani labda mtoto kapatwa homa!
 
Back
Top Bottom