Themann
JF-Expert Member
- Apr 15, 2022
- 3,844
- 16,095
- Thread starter
- #61
Tapeli yupo kazini na matapeli Wana umoja sana pale k/koo wanajuana vibaya sana, na wanalindana sana akishatapeli anatafuta hifadhi sehemu nyingine yaan Wana magoli ya kutosha wanayofanyia utapeli ukisikia tu ngoja nikakuchekie duka letu lingine hapo mbele maaan fumbua macho hapo amemaanisha ngoja nikuingize kwenye dunia ya matapeli ukiweza potea kabisa Wala usimsubiri pia kuna mafundi wa simu na laptop wale ndio balaa la dunia ni wezi wa vipuli ogopa ukimpa kifaa chako anang'oa vya ndani anaweka anavyovijua yeye
Daah na ukienda polisi wanatoka fasta
Mimi nilivopigwa ile simu kesho yake nikarudi lakini nilipita kwa mishe zingine huwezi amini sikumkuta hata mmoja kwenye lile duka kati ya wale niliowakuta jana hata yule alieniuzia kama unavosema wale jamaa wakishajua wamekuingiza mjini wana
Maduka tofauti kesho ukienda humkuti hili jambo tusilifumbie macho
Watu wanalizwa kila siku ya Mungu..
Kuna poti mmoja wabhuku mtaani alienda duka moja fulani pale uhuru
Kununua simu alivaa kiraia tu siku hiyo wakambambikizia simu mbovu kama kawaida yao wakajua ni raia mwenzao yule afande kufika nyumbani aanze kuikagua sasa simu
Ina overheat kinoma na haikai chaji
Alivorudi kesho yake anawaambia wanaleta dharau anawauliza aliemuuzia yuko wapi wanasema hajanunua hapo iyo simu akaondoka
Alivorudi alikuja na defender imejaa wajomba walibebwa wote pale dukani
Na duka likafungwa.