Kiboko ya Jiwe
JF-Expert Member
- Apr 7, 2020
- 12,702
- 36,141
Hi!
Si Wajasiriamali wote kwamba wana maisha mazuri kuliko Watumishi wa Umma ila nataka kusema kuwa wapo Wajasiriamali wengi tu ambao hata leseni ya biashara hawana, Kodi hawalipi kabisa na Serikali haiwatambui lakini wana pesa kuliko wenye maduka ambao hulipa Kodi kwa VAT.
Kuna Jamaa anauza Ugali nyama choma, huyu bwana akiondoa gharama zote za uendeshaji anapata faida ya TZS 200,000/- mpaka TZS 300,000/- kwa siku. Maana yake huyu kwa mwezi amefeli amepata faida ya TZS 5,000,000/-. Pesa ambayo wanalipwa Watumishi Waandamizi Wizarani. Hapo ameshatumia pesa ya kutosha ndani ya huo mwezi mwisho wa mwezi ana TZS 5,000,000/- .
Mtumishi Mwandamizi akipata hiyo TZS 5,000.000/- ndipo aanze kutumia, atasave Million Moja au Laki 5 tu. Kuna dogo anauza chips Mwenge kwa siku analaza Laki 3.5. Huyu baada ya matumizi yake yote mwisho wa mwezi akichungulia akiba yake hakosi Milioni 7. Faida ya Milioni 7 kwa mwezi ni Watumishi wa Umma wangapi wanaipata? Labda majizi tu ambayo hawana amani maana jela inawaita kila siku.
Kuna muuza chips Keko kwa siku anapata faida ya Laki 4 . Na jinsi alivyo bahiLi yule kwa mwezi analaza mpaka Milioni 10. Halipi kodi hata mia, kajenga mjengo Madale nahisi hata baadhi ya Wabunge hawana Nyumba kama ile.
Tisidharauliane ndugu. Kuna Watumishi wengi tu wa chini wamewazidi maisha mabosi zao.
Mimi ni Mwajiriwa ila nakiri kuwa utajiri nitasikilizia redioni tu. Kwa mishahara hii tusubiri kifuta machozi cha kustaafu labda au tuibe tunawiri na mwisho tukafungwe.
Si Wajasiriamali wote kwamba wana maisha mazuri kuliko Watumishi wa Umma ila nataka kusema kuwa wapo Wajasiriamali wengi tu ambao hata leseni ya biashara hawana, Kodi hawalipi kabisa na Serikali haiwatambui lakini wana pesa kuliko wenye maduka ambao hulipa Kodi kwa VAT.
Kuna Jamaa anauza Ugali nyama choma, huyu bwana akiondoa gharama zote za uendeshaji anapata faida ya TZS 200,000/- mpaka TZS 300,000/- kwa siku. Maana yake huyu kwa mwezi amefeli amepata faida ya TZS 5,000,000/-. Pesa ambayo wanalipwa Watumishi Waandamizi Wizarani. Hapo ameshatumia pesa ya kutosha ndani ya huo mwezi mwisho wa mwezi ana TZS 5,000,000/- .
Mtumishi Mwandamizi akipata hiyo TZS 5,000.000/- ndipo aanze kutumia, atasave Million Moja au Laki 5 tu. Kuna dogo anauza chips Mwenge kwa siku analaza Laki 3.5. Huyu baada ya matumizi yake yote mwisho wa mwezi akichungulia akiba yake hakosi Milioni 7. Faida ya Milioni 7 kwa mwezi ni Watumishi wa Umma wangapi wanaipata? Labda majizi tu ambayo hawana amani maana jela inawaita kila siku.
Kuna muuza chips Keko kwa siku anapata faida ya Laki 4 . Na jinsi alivyo bahiLi yule kwa mwezi analaza mpaka Milioni 10. Halipi kodi hata mia, kajenga mjengo Madale nahisi hata baadhi ya Wabunge hawana Nyumba kama ile.
Tisidharauliane ndugu. Kuna Watumishi wengi tu wa chini wamewazidi maisha mabosi zao.
Mimi ni Mwajiriwa ila nakiri kuwa utajiri nitasikilizia redioni tu. Kwa mishahara hii tusubiri kifuta machozi cha kustaafu labda au tuibe tunawiri na mwisho tukafungwe.