Watumishi wa serikali mliwezaje kutoboa, mbona mimi naenda kushindwa

Watumishi wa serikali mliwezaje kutoboa, mbona mimi naenda kushindwa

Kwenye hiyo laki nanusu ongeza mboga za nafaka maharage kama choroko na dagaa ikiwezekana kma mnatumia

Nimeishi kijijini sikuwa natumia hata Laki na nusu Kwa mwezi Yani kilakitu na nilisurvive now Niko mjini nakula nachotaka Sina stress saa bajet inaongezeka ila nikiamua inakaa sawa so kilakitu ni wewe unavoamua Kuishi kulingana na kipato chako kma unamalengo jibane
Wengine hata 100k msosi wa mwezi haifiki, licha ya kuwa na access ya kutumia zaidi.
 
Habari za jioni.

Nimeshindwa kupata usingizi kutokana na wimbi la mawazo.

Wakuu Take home yangu 613K Mimi ajira mpya mwaka jana ila nimekuwa na wimbi la mawazo na kuona kama sitaweza kutoboa labda nIpate washauri wengine wa maisha labda.

Nnafanya kazi mkoani,ila kadri siku zinavyoenda ninaona maisha magumu ilhali Mimi ni ajira mpya tu wa mwaka jana.

Nina mahitaji ya lazima mengi sana Nina familia ya mke na mtoto mmoja na ndugu wananitegemea.

Kila mwezi lazima.
Nitume nyumbani laki 1.
Nanunua chakula laki 150K.
Nampa mke wangu 150K ya matumizi na bills nyingine.
Kodi nimepanga chumba sebule 100K.
Sijaweka dharura Wala other charges.

Huu ni mwezi wa sita kazini sijanunua shati Wala Chochote juu ya familia yangu. Nimekuwa mtu wa mawazo na ninayeona nakuwa maskini kabisa.

Kazi yangu Ina posho ila ofisini wanatudhulumu tu hivyo hatuna Constant.

Jamani wazoefu naombeni mnishauri kama naona naenda kufeli mapema jamani.

Wengine mmewezaje?
Achana nayo. Security wakati unakufa njaa.
 
Mshahara huo na dharura na laki nanusu mna mifugo kma Kodi unalipa,laki nanusu bills gani mkeo analipia maji na umeme?

Hebu kaeni chini elezeaneni uhalisia wa maisha
Na mkeo nae kama sio mlemavu akatafute Hela ajitume wanawake mjini wanauza maandazi wanauza chakula aende shule za jirani auze ice cream natamni kungekuwa na voice note aisee😀
Hivi Una mchumba?😆😊
 
Ninyi ni waninga sana yaani mnakubaliana tuu kuwa mtakuwa mnatuma laki nyumbani bila sababu!? Vipato vyenu Vinafana, tuma endapo kuna dharura au ugonjwa tuu mwisho sio kila mwezi. Gombana na hao ndugu zako ndipo utaendelea. Watu ni wakongwe kazini lakini hatuna huo utaratibu wa kutuma kila mwezi bali ni penye uhitaji, dharura na wakati ambao mwenyewe nafsi yangu imeamua tuu niwakumbuke wazazi.
Kipato changu siwezi kukubaliana na mtu yeyote zaidi ya mke namna ya kutumia.
Nunua friji, weka nyama kwenye friji, chemsha maharage ya kutosha wela kwenye friji, nyanya unaweza kuziweka pia kwenye friji tena ukazigandisha, mimi kwangu nyanya zinakaa zaidi ya mwezi, kila kitu unaweza kukifanyia package ukaweka kwenye friji.
Ukinunua nyama wapime kwenye ujazo wa nusu kilo ili utumie ile inayohitajika tuu.
Ukiweza ichemshe yote gawa kwenye vi kontena weka kwenye friji.

Wekeni ratiba ya chakula na mboga na muifuate hakuna kuishi maisha ya kiswahili swahili na ya kishamba yasiyo na mpangilio.

Kisha weka malengo ya wazi ukimshirikisha mkeo kuwa, mwezi huu laki moja tutanunua vyombo, mwezi unao kiti, mwezi ujao nguo, mwezi ujao tutaanza kulipia kidogokidogo tv mwezi next and next mtakuta ndani ya mwaka mmoja mmepiga hatua.

Mimi leo naweza kuisaidia familia na wategemezi kwenye masuala muhimu tuu kwa sababu nilikataa kata kata kuishi maisha ya kimaskini ya eti kuchangia sijui sh ngapi kila mwezi no no no. Hata misaada ya kijinga jinga kutoka kwa ndugu acha kabisa huo ujinga mtabaki wote maskini.
Jitafute wewe kwanza na mkeo, jengeni familia yenu kwanza baadaye automatically mtakuwa na uwezo wa kusaidia wengine tena sio kwa laki bali kwa milioni. Otherwise utaishia jela nakuambia wewe mtumishi wa umma.
Safi.
 
Mshahara huo na dharura na laki nanusu mna mifugo kma Kodi unalipa,laki nanusu bills gani mkeo analipia maji na umeme?

Hebu kaeni chini elezeaneni uhalisia wa maisha
Na mkeo nae kama sio mlemavu akatafute Hela ajitume wanawake mjini wanauza maandazi wanauza chakula aende shule za jirani auze ice cream natamni kungekuwa na voice note aisee😀
Huna mdogo ako wa kike mwenye akili kama wewe? unipasie
 
Habari za jioni.

Nimeshindwa kupata usingizi kutokana na wimbi la mawazo.

Wakuu Take home yangu 613K Mimi ajira mpya mwaka jana ila nimekuwa na wimbi la mawazo na kuona kama sitaweza kutoboa labda nIpate washauri wengine wa maisha labda.

Nnafanya kazi mkoani,ila kadri siku zinavyoenda ninaona maisha magumu ilhali Mimi ni ajira mpya tu wa mwaka jana.

Nina mahitaji ya lazima mengi sana Nina familia ya mke na mtoto mmoja na ndugu wananitegemea.

Kila mwezi lazima.
Nitume nyumbani laki 1.
Nanunua chakula laki 150K.
Nampa mke wangu 150K ya matumizi na bills nyingine.
Kodi nimepanga chumba sebule 100K.
Sijaweka dharura Wala other charges.

Huu ni mwezi wa sita kazini sijanunua shati Wala Chochote juu ya familia yangu. Nimekuwa mtu wa mawazo na ninayeona nakuwa maskini kabisa.

Kazi yangu Ina posho ila ofisini wanatudhulumu tu hivyo hatuna Constant.

Jamani wazoefu naombeni mnishauri kama naona naenda kufeli mapema jamani.

Wengine mmewezaje?
Mama anaupiga mwingi
 
N

NIlianza hivyo mwanzoni ila nikaona kama namtesa mke wangu ila ilinisaidia.

Nilipoacha nimejikuta kwenye madeni Hela hazikai.

Mpaka nahisi nimelogwa itabidi nirudi Tena

Kwanza anayekwamisha maendeleo yangu ni huyu mke wangu

Maana kuna kipindi nilimwambka aniambie kiasi chake Cha siku Kwa chakula maana vitu vya muhimu vyote viko ndani akawa ananijibu upuuzi nilitamani nimpige.

Maana Mimi niliwahi kujitolea sehemu nilikuwa nalipwa laki 3 na ilinitosha yeye hana bajeti mwezi hauishi Hela inaisha yaani ana rough bajeti mpaka kuna muda nimeamua nikae na Hela niwe nampa kila asubuhi.
Pole sana Mkuu.
Ushauri wangu ni kuwa
1.Simamia manunuzi yote mara upatapo mshahara,nakusudia nunua nyama,samaki,maharage weka kwenye friji katika vifurushi vidogo vidogo
Mfano:
Mchele 10kgs, Sembe 6kg
Nyama 4kgs weka parcels 12
Samaki wa 30,000, weka parcels 10
Maharage 3kg chemsha yote kwa mkaa aweke parcels 9 hadi 10. Umeme 20,000. Usiku kuleni vyakula vyepesi ndizi,viazi. Bana matumizi kiasi kwamba bills zote zisizidi 250,000.

Wazee watumie 50k. Achana na kulipia visimbuzi vya TV. Weka akiba 150k. Hii akiba ni lazima. Matibabu najua mna bima ya Afya.

Kila la kheri Mkuu
 
Sasa kama ndio unaanza kazi, unapata 613,000 unalia,

Siku ukikopa ukaanza kupata mshahara wa laki na nusu kwa mwezi mbona utajiua kabisa.

Najua wewe ni CO, na hiyo ndio tske home.

Mimi napata salary 260 000.

Nilikuwa na mshahara kama wako.

Nilikopa bank, nikaenda kununua viwanja nikatapeliwa.

Sasa hivi nalipa deni na kiwanja sina. Nimepambana lakimi nchi hii huwezi kupata haki, unadhulumiwa na aliyekudhulumu yupo anadunda na huna cha kumfanya.

Na nina mke na mtoto.

Na sijafa. Nipo tu natuliza moyo maisha mengine yaendelee.

Ushauri wangu.

Kama 613,000 take home haikutoshi, usije kukopa tena mkopo wa muda mrefu, maana bank za sasa zinakopesha mpaka mika 10, utakufa kabisa, maana utaanza kupata 200,000 wakati deni lako la bank halitaisha.

Na kama una passion ya biashara na uko mkoa mzuri au mkeo jichange ufanye kitu. Au kama una passion ya kilimo na mkoa unaruhusu lima.

Mimi niko Kilimanjaro, huku huwezi kulima hata bustani, kufuga wala biashara.

Naishi hivyo hivyo na 260,000 changu kwa kujibana.

Na usije ukawa na matumizi makubwa, sana, kadi yako ya bank itaishia kwa wakopeshaji wahuni wa mtaani, utashindwa kulipa kodi ya nyumba, itaonekana daktari njaa kali kinomaaa.

Na option ya madaktari huwa ni kuanza kupiga dili haramu, kama kutibu wagonjwa nje ya mfumo, kutoa mimba, na kuuza dawa kimchongo maisha yaende.

Utakuha kuanza kypata migogoro na wakuu wa wilaya, waganga wafawidhi, waganga wakuu wa wilaya na TAKUKURU. Utaanza kuhamishwa hamishwa vituo vya kazi kwa adhabu na Utapoteza focus na utaona kazi chungu.

Option kwa kipato kidogo huwa ni 2:
  • Kubana matumizi ya kipato ulicho nacho (njia rahisi) au
  • Kuongeza kipato chako (njia ngumu)

Pambana kujibana katika matumizi yako.
 
Nikapata mshahara nanunua chakula kama 150 hapo nimeweka gas,Michele,unga,mafuta,mkaa.

Namkabidhi waifu 150K Kwa kigezo Cha kutumia elfu 5 Kila siku ya mboga na hapa nishagombana nae maana unakuta mwezi hauishi Hela imekata.

Mpaka hapo nakuwa nimeshatumia laki 3.

Laki Moja natuma nyumbani kila mwezi nabakiwa na laki nne.

Kodi nalipa laki Moja uwa nasave maana nalipa miezi mitatu.

Mpaka hapo laki 5.

Mimi nabaki na hiyo laki Moja nayo kuna muda nakuta imeisha hata sielewi inaenda wapi
Hapo hutoboi, nunua chakula mda huu wa mavuno mahindi gunia 60k, mpunga gunia 60k x 2 = 120 hapo utakula mwaka mzima. Nunua mboga kama dagaa na maharagwe weka ndani wife kazi yake iwe kupika tu mtafutie na kijishughuli kimshughulishe kwenye hiyo 300k ya chakula umpaka hapo ushaokoa 200k hom tuma 50k na zinazobaki save ufungue biashara
 
Asante boss mawazo mazuri sana mkuu nimeyapokea
Shukrani.
Tupo pamoja.
Nyongeza:-
Siyo lazima kuchangia kila shughuli hasa za harusi na send-off.
Sehemu ya kutembea kwa miguu usipende kutumia usafiri wa kukodi au wa umma, tembea kwa miguu.
Kwa kipato chako usijipe majukumu ya kuhudumia nyumba ndogo. Michepuko ina gharama.
Usinunue chakula cha kwenda kupima kwa kilo kila siku au baada ya siku chache.
Kama unanunua sembe chukua kiroba cha 25kg bei ya jumla utaokoa pesa ya nyanya.
Ukifika wakati wa mavuno nunua mchele, maharagwe, kunde, choroko au mbaazi nyingi bei ikiwa ndogo tunza ndani.
Mafuta ya kula pia usinunue ya kupima kanunue kidumu cha Lita 3 au 5 utapumzika muda mrefu.
 
Back
Top Bottom