Watu wawili wachomwa moto Tabata

Watu wawili wachomwa moto Tabata

Wachomwe tu aise,juzi nimekoswakoswa simu yng acha tu yani.Hivohivo na bodaboda na nisingekuwa nimeishika vizuri ingekuwa ndo basi tena.
 
Kuna kidada kimoja kizembe kiliwahi kumfanya jamaa na heshima zake achomwe moto,kilimuitia mwizi wakati wanaongozana sasa sijui kilitaka njia nzima kitembee peke yake?!

Raia tuache kuchukua sheria mikononi ni hatari sana.
 
Ajabu kweli watu mnashabikia tukio hili? Ni hukumu gani mtu akiiba achomwe moto? Mbona tunachukua majumu mazito?

utafiti, usemacho ni sahihi, hatuna mamlaka ua kuhukumu hasa wezi kwa kuwachoma moto, ingekuwa jambo la maana kuwatendea sharia yetu ua kukatwa mkono, lakini inakuwa hivyo sasa kutokana na askari wanavyofanya....
 
Last edited by a moderator:
Safi sheria imechukua mkondo wake.

Serikali inafanya ubishi wa ajabu.
Ivi ni kwanini sheria ya Kiislam juu ya mwizi isitumike?

Katika uislam mwizi hukatwa kiganja cha mkono. Na hakatwi na kila mtu,atakatwa na mamlaka husika hiyo inakuwa ni aibu yake ya kudum na jamii itamtambua kwa alama hiyo.

Hii ndio ndio njia sahihi ya kumuadabisha mwizi na sio kumuuwa.

Ni haram kumuuwa mtu eti kisa kaiba.
 
Acha tu wizi, utarudi salama
haya bana mkuu kwa hiyo mie mwizi.ila namaanisha hv,hata we unaweza kutoka kwako salama ila ukikutana nao tu anza kusali mana watakuchukulia ulicho nacho na kukuua juu.mie mwenyewe cku hz nikipishana na bodaboda yenye wanaume wawili kiukweli nachanganyikiwa kwa uoga
 
Hao hao wakiachwa kesho wanakomaa na kuibuka na mbinu mpya, baba wa watu wamemtoa roho mlimani city pale, yanauma ngoja yakukute tu ndio utajua jinsi gani yanavyouma. Ni haki yao kufa kwa kuwa wamepitiliza kwenye ubinadamu hawapo tena.

Mkuu sio kama hainiumi huyo mdada kuibiwa begi lake hapana inaniuma ila hao watu kuchomwa moto inaniuma zaidi. Hebu nikulize swali moja, simu inayouzwa laki 7 dukani akitokea mtu akiletea kwa laki 1 utaiacha? Utamuliza amepata wapi? Utafanya means umrudishie alieibiwa? Najua hutaiacha na zaidi utamwambia akipata nyengine akutafute. Ndio maana wizi hautaisha maana sisi niwatumiaji wakubwa sana wa bidhaa za wizi kuliko za halali, tunawahukumu bure kumbe "tumewatuma" wafanye hivyo
 
safi sana, wezi wamefanya nifukuzwe kazi yangu na mshahara wa laki 7 na allowance juu za kula, nilikuwa tanga site meeting kazi umeme, nikiwa na laptop na camera za picha za site walinivamia ubungo wakanipora, na kesho yake ndo kikao mawasiliano tower cha REA , nikawaelezea mabosi hawakunielewa wakanipa termination lettwr , bora wachomweee na Mimi ningekuwepo ningeongeza lita ya mafuta
 
Nasikia ni mwanamke na mwanaume sasa huyo mwanamke ni kawaida yake kukodi pikipiki na kupeleka ilipo timu ya wezo ni kundi lipo mahali dada akishafika wenzie wanapora wanakimbia kumbe jamaa wamemjua dada wamemuwekea mtego na jana ikawa mwisho wake .RIP wezi.
 
Nasikia ni mwanamke na mwanaume sasa huyo mwanamke ni kawaida yake kukodi pikipiki na kupeleka ilipo timu ya wezo ni kundi lipo mahali dada akishafika wenzie wanapora wanakimbia kumbe jamaa wamemjua dada wamemuwekea mtego na jana ikawa mwisho wake .RIP wezi.

Acha waendelee kuchomwa labda na wenzao wataacha, TZ inakoelekea kwa ujambazi sio imekuwa too much!
 
Nimesoma kwamba vijana wawili wameuawa kwa kuchomwa moto kule Tabata Liwiti. Kisa cha vijana kuuawa ni baada ya kuiba pochi ya mwanamke mmoja.

Nimesikitika sana kuona jinsi wananchi walivyochoshwa na utendajikazi wa jeshi la polisi kiasi kwamba wanajichukilia sheria mikononi.

Wizi wa pochi unakatisha uhai wa mwanadamu.

Itafika mahala hata viongozi wa serikali ambao wanaiba mali ya umma nao watakuja fanyiwa haya haya. Kwasasa wanadhani haya yataishia huku uswazi na ndo maana hawachukui hatua za kuboresha jeshi la polisi.

Itafika muda wezi wakubwa watatendewa hivi hivi. Tunao wezi kama vile

- Vibali vya kuua tembo
-Twiga waliopelekwa Qatar na ndege ya kijeshi
-Pesa za rada
-Epa
-Kagoda
 
yaani huo muda wa kuwachoma hao wezi wakubwa wala hauko mbali very soon kitaeleweka
 
ngoja tuone ikiwafikia hao vigogo nao maana ni miaka mingi tumekuwa tukisubiria......
 
ngoja tuone ikiwafikia hao vigogo nao maana ni miaka mingi tumekuwa tukisubiria......


Tena hao ni rahisi sana kuwanasa kwenye mashangingi yao wakiwa kwenye foleni, vinginevyo waanze kutumia nyungo

Piga picha mzee wa vijisenti akiwa ungoni
 
Nimesoma kwenye Michuzi blog ya leo tarehe 24 August, 2014 kwamba vijana wawili wameuawa kwa kuchomwa moto kule Tabata Liwiti. Kisa cha vijana kuuawa ni baada ya kuiba pochi ya mwanamke mmoja.

Nimesikitika sana kuona jinsi wananchi walivyochoshwa na utendajikazi wa jeshi la polisi kiasi kwamba wanajichukilia sheria mikononi.

Wizi wa pochi unakatisha uhai wa mwanadamu.

Itafika mahala hata viongozi wa serikali ambao wanaiba mali ya umma nao watakuja fanyiwa haya haya. Kwasasa wanadhani haya yataishia huku uswazi na ndo maana hawachukui hatua za kuboresha jeshi la polisi.

Itafika muda wezi wakubwa watatendewa hivi hivi. Tunao wezi kama vile

- Vibali vya kuua tembo
-Twiga waliopelekwa Qatar na ndege ya kijeshi
-Pesa za rada
-Epa
-Kagoda

Mkuu Incredible, nikukumbushe masikitiko juu ya kisa cha mtindo huu, kwanza nikusahihishe kuwa vijana hawa wameiba pochi hawajaiba bali wamepora kwa kukwapua. Huyu dada alikuwa akitembea kando ya barabara kisha wakatokea hao majambazi wakiwa ktk pikipiki boxer wakakwapua mkoba na kukimbia. Style hii iliwahi kumkumba raia wa nchi za Scandnavia akiwa kabeba pack yale mabegi ya watalii eneo la Upanga, barabara ya Umoja wa Mataifa, kwa kuwa lile pack alikuwa amejifunga nalo mwilini yule jambazi alipokwapua halikumtoka mwilini yule mzungu na jambazi hakuliachia, pikipiki ikiwa kwenye mwendo mkali, yule dada aliburuzwa kuanzia S/M Muhimbili hadi maeneo ya Fire, Morogoro Road, alikuwa amefariki huku akiwa ameburuzwa baadhi ya sehemu ya mwili wake mifupa ikiwa nje. Nadhani umepata picha fulani ambayo hata dada huyu wa Tabata angeweza kukumbana nayo ikiwa tu hangeachia mkoba wake. Binafsi nimefurahi kuwa yaliyowakuta maana idadi ya majambazi imepungua.
 
Back
Top Bottom