Watu wa Tanga nawaita hapa

malisak

JF-Expert Member
Mar 16, 2006
694
772
OIP.jpg

Jamani ndugu zangu wa Tanga kwani alietuloga nani? fursa tunazisikia ila hata hatushtuki wanakuja walowezi wanajizolea fursa na sisi tupo hapa hapa kweli, zinatangazwa zabuni mpo kimya mnakuja kukurupuka dakika za majeruhi watu wameshasafirikutoka mikoani mbali huko kukimbilia fursa.

Na hata mkipewa nafasi hamchangamkii mpk mnawapa watu nafasi ya kujipandikiza na kuwahia nafasi kupitia wachahce wenye nazo ambao ni waroho na wenye tamaa ya pesa. Halafu mnalalamika mji unazidi kufa wakati pesa zimekuja na zinaondoka kurudi mikoa mingin. Mradi wa ujenzi wa Jetty ungekuwa umetangazwa vizuri na vyombo vya habari vya hapa tanga na serikali kwa ujumla.

Huu mradi ungerudisha hadhi ya mkoa wetu kwa jinsi ulivyo na tija ila cha kusikitka hata wale waliofidiwa baada yakupisha eneo la ujenzi badala ya kuzungusha mrdini pesa wengi wamekwenda kuoa kuongeza wake wengine eeeehh Mungu baba. Nini shida?

Kunahaja kupaza sauti kurudisha mkoa kwenye chati yake, fikiria mkoa umeshakuwa jiji lkn ni kheri hata kipindi ulipokuwa mji. Wana Tanga tuamke jamani hali tete inaumiza. Viwanda vimebaki kama magofu, wagosi wa kaya wamechoka kupiga kelel wameamua kujiajiri nchi imewekwa bond.
 
Ongezea na Kupenda Ngono

Ni Mkoa pekee umebarikiwa kuwa na Mawaziri Karibia 4.Lakini sinahakika kama wanaumia kwa kudorora kwa uchumi wa Mkoa(sipendi kuita Jiji)

1.January
2.Ummy
3.Juma
4.Khamisi
Hawajali wao wapo Dodoma muda wote wakishangilia ujinga ukiwanyima kura wanaiba
 
Mahali palipo na uchawi na uganga ni ngumu sana watu kuwa na maendeleo...
Hakuna kitu kama hicho hakunamahali pana uchawi kama dar es salaama maana kuna mvurugiko wa makabila kila mtu anajihami
 
Ongezea na Kupenda Ngono

Ni Mkoa pekee umebarikiwa kuwa na Mawaziri Karibia 4.Lakini sinahakika kama wanaumia kwa kudorora kwa uchumi wa Mkoa(sipendi kuita Jiji)

1.January
2.Ummy
3.Juma
4.Khamisi
Ngono ni hulka ya mtu haihusiani na uasilia
 
Maamuzi yote ya serikali nyingine mbwembwe tu wala hamna cha maana basi mbona Dodoma inakuwa kwa kasi?

Acheni ushamba kuna watu wanaishi Dar huko kwao wamekimbia, waha kibao ni wafanyabiashara hapa Dar kwao kigoma choka mbaya ila ni wachapakazi na wana pesa hapa mjini.

Watu wanafuata fursa bila ya bandari na mashamba ya mkonge pengine pasingekuwa na mkoa wa Tanga, sasa hivyo kama base ya mkoa vimekufa unatakaje sasa?😅

Peleka fursa sehemu, ukiangalia sehemu nyingi majengo ni sehemu za biashara kama mahotels, malls za kisasa, kumbi za mikutano, vyuo, sehemu za huduma za kijamii kama hospital, ofisi za kupangisha pamoja na majengo ya wizara mbali, je uliona wapi mkoa ulioendelea hapa bongo pakawa hata na storey buildings za floor 5 ambazo ni nyumba ya mtu binafsi? Labda zipe apartments za biashara. Hao majengo ndo yanaletq mvuto kwenye miji yote hapa Tanzania wala sio life standard ya watu kwa nyumba mtu binafsi.

Unaweza kwenda kweny mji umeendelea ukakuta jengo kubwa ni ofisi ya posta 😅😅au hotel eti ndio maendeleo ya Bongo.
 
Alietuloga na alaaniwe kutoka tanga ya viwanda mpk tanga ya magofu inaumiza sana
...Inahuzunisha Sana ! Ukikumbuka Tangold iliyotoa Juisi ya Embe iliyokuwa Nzito na Tamu Sana!
Kiwanda Cha Sabuni kilichotoa Mbuni na Gardenia.
Kiwanda Cha Chuma.
Kiwanda Cha Mbolea
Kiwanda Cha Plastiki Amboni zilikotoka ndoo na mabeseni Bora vya Plastiki.

...vyote vimebaki Historian TU.

Tanga kunani palee ?
 
...Inahuzunisha Sana ! Ukikumbuka Tangold iliyotoa Juisi ya Embe iliyokuwa Nzito na Tamu Sana!
Kiwanda Cha Sabuni kilichotoa Mbuni na Gardenia.
Kiwanda Cha Chuma.
Kiwanda Cha Mbolea
Kiwanda Cha Plastiki Amboni zilikotoka ndoo na mabeseni Bora vya Plastiki.

...vyote vimebaki Historian TU.

Tanga kunani palee ?

Duh nimetoka Tanga mwaka 2003 mpaka leo naona malalamiko ni hayo hayo tatizo ni nini? Au Siasa !!!
 
Duh nimetoka Tanga mwaka 2003 mpaka leo naona malalamiko ni hayo hayo tatizo ni nini? Au Siasa !!!
Tanga hakuna project ya maana ya serikali. Mimi nilienda 2019, yaani hawana chochote wanajenga tangu Nyerere alimaliza. Mkoa zimebaki alama tu kwamba palikuwa na bandari. Yenyewe juzi hapa Magufuli ndio kaifufua.
 
...Inahuzunisha Sana ! Ukikumbuka Tangold iliyotoa Juisi ya Embe iliyokuwa Nzito na Tamu Sana!
Kiwanda Cha Sabuni kilichotoa Mbuni na Gardenia.
Kiwanda Cha Chuma.
Kiwanda Cha Mbolea
Kiwanda Cha Plastiki Amboni zilikotoka ndoo na mabeseni Bora vya Plastiki.

...vyote vimebaki Historian TU.

Tanga kunani palee ?
Yaani Gofu juu Industrial Area imebaki Magofu magofu matupu kama jina lake labda jila limeleta laana sasa wanafanya ofisi za baadhi ya taasisi za serikali kama TANroads, Temesa etc yaani ni huzni kubwa
umesahau kiwanda cha sabuni ya mbuni
Kiwanda cha mablkanket
MAmlaka ya mkonge ndio inafufuka sasa
Kiwanda cha foma
Kiwanda cha mashuka cha CIC na somaia Group
Vyote vilikuwa na tija na vilitoa ajira nyingi sana. Kiwanda cha mbolea kimeuzwa imekuwa Depot ya mafuta ya Kampuni ya GBP ni huzuni kitambo sijaja nimekuja naona mtu mmoja unakutana nae mjini mara sita kwa siku jinsi ambavyo hakuna watu
 
Back
Top Bottom