Watoto wa viongozi wa CCM hata wa primary wanaruhusiwa kufanya siasa majukwaani; wasomi wa vyuo vikuu siasa marufuku. Tumelogwa?

Resilience

JF-Expert Member
Jan 4, 2023
943
4,458
Chama cha mapinduzi baada ya kuona siasa zinazalisha viongozi shupavu kutoka vyuoni kilikuja na mbinu yakukataa siasa kwa wanafunzi wa vyuo. Ili watimize lengo lao wakapiga marufuku siasa wakishirikiana na wakuu wa vyuo na maprofesa na madaktari waliosimamia Katazo hili wakapewa uteuzi.

Leo chuo kikuu cha DSM hakuna mwamko wa fikra kwa sababu siasa za vyuo zilijikita katika makongamano na midahalo ya wazi ukitumika sana ukumbi wa Chuo kujadili hoja.

Ilifika wakati hata wanasiasa wakubwa wakitaka kujadili hoja muhimu wanakwenda kutumia kumbi za vyuo na hivyo kutoa fursa ya kuulizwa maswali na wanafunzi. Leo hii vyuo vimekuwa kama primary school

Chuo cha SAUT mwanza wakati wa Padre Kitima mjadala wa kupata viongozi ulikuwa mkubwa; wanafunzi wake hata ukiwaona leo unaona upeo mkubwa wa maarifa. Leo hii SAUT wanafundishwa kukariri siasa za nje kuliko kujadili maisha halisi ya mtanzania

Kinachosikitisha ni kuruhusiwa kwa watoto wadogo ambao baba zao ni mawaziri na maraisi kufanya siasa za majukwaani lakini watoto wa wengine ni marufuku. Leo watoto wa Kikwete , Mwigulu nk wapo majukwaani wanapiga kampeni za baba zao. Hakuna anayekataza na wizara ya elimu hakuna Sehemu imekemea.

Tunadhani kuwaandaa watoto wetu kwa kuwakataza watoto wengine kufanya siasa ni sahihi? Huu ubaguzi unaofanywa na awamu ya sita unalenga kulijenga Taifa au kulibomoa?
 
Chama cha mapinduzi baada ya kuona siasa zinazalisha viongozi shupavu kutoka vyuoni kilikuja na mbinu yakukataa siasa kwa wanafunzi wa vyuo. Ili watimize lengo lao wakapiga marufuku siasa wakishirikiana na wakuu wa vyuo na maprofesa na madaktari waliosimamia Katazo hili wakapewa uteuzi.

Leo chuo kikuu cha DSM hakuna mwamko wa fikra kwa sababu siasa za vyuo zilijikita katika makongamano na midahalo ya wazi ukitumika sana ukumbi wa Chuo kujadili hoja.

Ilifika wakati hata wanasiasa wakubwa wakitaka kujadili hoja muhimu wanakwenda kutumia kumbi za vyuo na hivyo kutoa fursa ya kuulizwa maswali na wanafunzi. Leo hii vyuo vimekuwa kama primary school

Chuo cha SAUT mwanza wakati wa Padre Kitima mjadala wa kupata viongozi ulikuwa mkubwa; wanafunzi wake hata ukiwaona leo unaona upeo mkubwa wa maarifa. Leo hii SAUT wanafundishwa kukariri siasa za nje kuliko kujadili maisha halisi ya mtanzania

Kinachosikitisha ni kuruhusiwa kwa watoto wadogo ambao baba zao ni mawaziri na maraisi kufanya siasa za majukwaani lakini watoto wa wengine ni marufuku. Leo watoto wa Kikwete , Mwigulu nk wapo majukwaani wanapiga kampeni za baba zao. Hakuna anayekataza na wizara ya elimu hakuna Sehemu imekemea.

Tunadhani kuwaandaa watoto wetu kwa kuwakataza watoto wengine kufanya siasa ni sahihi? Huu ubaguzi unaofanywa na awamu ya sita unalenga kulijenga Taifa au kulibomoa?
Wewe msomi umekatazwa na nani?
 
Ninachojua mtoto anapenda anachokiona kutoka kwa watu wake wa karibu( wazazi).Ndio system ya mababu zetu kabla ya hii elimu majununi muashi anazalisha muashi,mvuvi ivyo ivyo.
Suala la wengine kunyimwa sina cha kueleza.
 
Ninachojua mtoto anapenda anachokiona kutoka kwa watu wake wa karibu( wazazi).Ndio system ya mababu zetu kabla ya hii elimu majununi muashi anazalisha muashi,mvuvi ivyo ivyo.
Suala la wengine kunyimwa sina cha kueleza.
Kwanini wakifanya wakulima ni dhambi akifanya wa waziri iwe sawa? Leo kila mzazi akisimama na mtoto wake jukwaani utavumilia?
 
Yote kwa yote namshukuru sana rais Samia kwa mafuriko ya Rufiji.
 
Kwanini wakifanya wakulima ni dhambi akifanya wa waziri iwe sawa? Leo kila mzazi akisimama na mtoto wake jukwaani utavumilia?
Kuna qaila mtoto wa msanii iyo mmoja ninaemfahamu labda mtu akiwa bora anaonekana hata umfiche vip.
NB.
Ni huo mfano mmoja tuu ninao sina kingine mkuu.
 
Back
Top Bottom